Power G
JF-Expert Member
- Apr 20, 2011
- 3,886
- 1,194
Wapenzi wa JF, kwa muda mrefu wakati nikiwa nyumbani Tz nimekuwa nikisikia na kuona watu wengi wakipendelea kula nyama ya kuku wa kienyeji. Hata katika maeneo yale tunayokamata moja baridi moja moto, bei ya kuku wa kienyeji huwa kubwa kuliko ya kuku wa kisasa. Nilishawahi kusikia watu wakisema wanaogopa kula kuku wa kisasa kwani wanaume wanahofia kuota matiti na akina mama wanahofia kuota ndevu. Ukweli wa jambo hili siujui ingawa nimekuwa nikichukua tahadhari ya kutotumia nyama ya hao kuku wa kisasa.
Tatizo linalonikabili kwa sasa ni kwamba niko ughaibuni. Huku wale kuku wanaotafuta mende, funza na panzi mitaani hawapo kabisaaa. Na wala ukisema kuku wa kienyeji ni msamiati ambao ni mgumu kwa wenyeji wa hapa kuufahamu. Kuku wote waliopo ni wale wa kisasa. Nyama ya kuku ndiyo kitoweo kinachopatikana kwa urahisi na kwa bei nafuu. Jamani mwenye uhakika wa madhara ya hawa kuku wa kisasa aniambie maana naogopa kurudi Tz nikiwa nimeota matiti!! Wakati huo huo ndiyo kitoweo ambacho gharama yake ni ndogo na kinaweza kunisaidia ku-save vi-dola kidogo kwa ajili ya matumizi ya ndugu na jamaa huko Tz.
Tatizo linalonikabili kwa sasa ni kwamba niko ughaibuni. Huku wale kuku wanaotafuta mende, funza na panzi mitaani hawapo kabisaaa. Na wala ukisema kuku wa kienyeji ni msamiati ambao ni mgumu kwa wenyeji wa hapa kuufahamu. Kuku wote waliopo ni wale wa kisasa. Nyama ya kuku ndiyo kitoweo kinachopatikana kwa urahisi na kwa bei nafuu. Jamani mwenye uhakika wa madhara ya hawa kuku wa kisasa aniambie maana naogopa kurudi Tz nikiwa nimeota matiti!! Wakati huo huo ndiyo kitoweo ambacho gharama yake ni ndogo na kinaweza kunisaidia ku-save vi-dola kidogo kwa ajili ya matumizi ya ndugu na jamaa huko Tz.