Kujadili wagombea Uraisi 2015 wakati Raisi wa sas katushinda ni UPUNGUANI

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
Hii mijadala inayoibuliwa huku ya mara Lowassa for 2015, Prof Mwandosya kugombea 2015, Membe anafaa 2015 mara Sitta na mbio za uraisi 2015 ni upunguani!

Tunaongelea 2015 wakati 2011 inatushinda. Hao tunaowasema wamekaa tu nchi inateketea tunawajadili eti watagombea 2015. Watagombea ili nini? Sasa hivi wanatusaidiaje? Dowans wanalipwa, IPTL, TRC, Loliondo, Wizi kwenye Halmashauri na mengineyo bado tunapoteza muda kuwafikiria. Kwani kukemea maovu mpaka 2015? Mafanikio yao ni nini sasa hivi? Eti ni wasafi!! Kwani JK kabla ya 2000 alikuwa na uchafu gani tunaoujua? Si aliitwa chaguo la Mungu?

Saa nyingine tunacheka tamko la waislamu lakini na matendo yetu humu ndani hayapishani sana. Hatuweki vigezo vya kumpata Raisi bora atakayetutoa kwenye dhiki. Tunabaki kujadili watu ambao hatuoni msimamo wao kwenye matatizo yetu ya msingi! Wengine watasingizia collective responsibility, hii haikuzuii kufikiri. Haikuzuii kusimama kidete na kutetea maslahi ya watanzania. Kama waziri au kiongozi unaona unabanwa kutetea achia nafasi na tutakuamini.

Hakuna sababu ya kupoteza muda kuwajadili watu wasio na msaada kwetu. Nakereka sana viongozi wote wako kimya kuhusu dhuluma inayoendelea. Sio wa upinzani sio wa CCM. Hakuna vitendo ni maneno tu. Dowans ni ya fulani, Dowans kampuni ya kitapeli, Mkataba na Richmond feki, huu sasa ni upuuzi! Ni sawa sawa mtu anakukumbusha jina lako!!

Maneno huumba lakini siku wananchi waliochoka na porojo zetu watakapochagua msitu na kutokea huko ndio tutajua 2015 nani Raisi!
 
hili nilisha lielezea hapo nyuma lakini inawezekana kuna watu wa system au kutokuelewa kwa baadhi ya watu basi huleta hizi habari naona kupoza vuguvugu wa masuala ya sasa. lakini ni vizuri kukumbushana watu waache hii tabia.
 
hili nilisha lielezea hapo nyuma lakini inawezekana kuna watu wa system au kutokuelewa kwa baadhi ya watu basi huleta hizi habari naona kupoza vuguvugu wa masuala ya sasa. lakini ni vizuri kukumbushana watu waache hii tabia.

Inakera sana! Nashindwa kuelewa kwamba hao tunaosikia wanatajwa kwamba wanafaa mara hawafai sasa hivi wanafanya nini? Kwa nini wanatuacha tunadhulumiwa? Tunaibiwa? Tunatapeliwa? Kwa nini? Kuna ule msemo 'the silence of our friends hurts more than the noise of our enemy'. Kama wao wanatupenda na wanatufaa ni marafiki zetu, lakini ukimya wao unatuumiza kuliko kelele za mafisadi na wezi wengine! Kuwa kwao safi hakuwapi haki ya kuendelea kukaa kimya
 
Ndio uhuru wa kuongea uo mkubwa! Ama hujui GIGO!!

Najua Mwanamageuko ila 2015 asikudanganye mtu sio karibu. Kwa shida tulizo nazo utafikiri ni mwisho wa karne. Tunaanza kumfikiria mtu mwingine wakati huyu tulie nae hatujamalizana nae! Na hao tunaowasema wako nae, tena karibu kuliko sisi. Ndio washauri wake. Anayoyafanya huyu wa sasa wanayaona pia naamini wanashiriki! Kama wanamshauri hawasikilizi mbona bado wako nae? Au ni maslahi?

Kwa wenzetu mtu kabla ya kuwa mgombea unakuta msimamo wake kwnye mambo kama ushoga, abortion, kodi, mazingira etc unajulikana. Huku hamna hilo! Tunatumia usafi kama kigezo kikuu! Yeye anaweza kuwa 'msafi' marafiki zake mijizi! Halafu anawaendekeza! Uhuru wa kuongea tuutumie kuongea yanayoijenga nchi yetu! Tusiutumie kupiga story!
 

Maneno huumba lakini siku wananchi waliochoka na porojo zetu watakapochagua msitu na kutokea huko ndio tutajua 2015 nani Raisi![/
QUOTE]

Hapo sasa umenena
 
UJUE WATU WENGINE SIJUI WANA AKILI MGANDO, WAKATI HAYA MANGURUWE( meaning CCM by HAMAD RASHID) YAMESHINDWA KUTULETEA MAENDELEO WAO BADO WANAWAKUMBATIA,
 
kaaaaaaaaazi kweli kweli,lakini nadhani ni bora wanaoutaka urais wangetangaza nia mapema ili tupate muda wa kuwajadili kuliko sasahivi watu wanavyojadili uvumi
 
Back
Top Bottom