Kufunga minyororo magari yanayodaiwa ushuru wa maegesho mijini ni utaratibu wa ovyo kabisa

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,284
21,403
Siamini kabisa kwamba kuna wasomi walikaa sehemu wakajadili na kulipana posho za kikao kwamba:

Magari yanayodaiwa ushuru wa maegesho (parking) Yaanze kufungwa minyororo ili kushinikiza wamiliki kulipia tozo hizo.

Huu ni utaratibu wa hovyo sana

1. Huu utaratibu ni Hovyo kwasababu unatupunguzia wateja sisi wafanyabiashara Kariakoo, Ilala! Sisi wafanyabiashara tunalipia leseni manispaa, tunalipia zimamoto, tunalipia pesa za usafi, tunalipa kodi nyingi tu ili tufanye biashara, Mnapowafungia wateja wetu magari yao mnawatisha kwamba wasije ilala kwamba watakamatwa hili peke yake linatuondolea wateja katika biashara zetu.

2. Jambo jingine la kushangaza hivi nyie wachukua maokoto ya ushuru mmechangia nini kwenye kuwekeza maegesho hadi mchukue ushuru wa maegesho? Magari mengi yanaibiwa kwenye maegesho na ushuru wanalipa, agari yanaibiwa vipuri au taa yakiwa kwenye maegesho huo ushuru mnaolipwa je unafaida gani kwa mwenye chombo kama hamyalindi magari yao wala hamlipi fidia linapotokea janga au uharibifu?

3. Wizara na serikali kwa ujumla mlipopitisha huu utaratibu wa ushuru wa maegesho mlitegemea kwamba hawa wenye magari waendeshe halafu wakapark wapi!?

Gari ileile moja mnaitoza ushuru kibao hamuoni hiyo ni kero jaman
  • gari ileile mnaitoza ushuru wa kuingiza nchini (TRA)
  • Mnaitoza Ushuru wa kutumia barabara (road licence) kwenye kila lita moja ya mafuta mnafyeka sasa mnategemea huyu mtu akapaki porini?
  • Mnamchukua nenda kwa usalama
  • kwenye bima cha kwenu pia kipo na mengine mengi.
Mnataka hawa wenye magari waendeshe magari then wakapark wapi?

Huu utaratibu wa kutoza ushuru maegesho haupaswi kabisa kuwepo, ni utaratibu wa hovyo kabisa.

Mwenye gari katoka zake nyumbani kisitaarabu kufuata huduma kwa mfanya biashara halafu nyie kama serikali mnavalisha watu vibrauzi vya njano kwa kazi ya kufungia wateja wetu magari yao mnataka wateja tupate wapi wakiogopa kuja mijini?

Kwanini mnapenda kuifanya nchi yetu sote iwe kero kwa wengine jamani.
 
Nchi ya hovyo sana hii inashangaza huo upuuzi unaota mizizi ukiwaambia hizi ni mambo za kijinga wanakwambia tunakusanya Mapato na hivi vitu vya kijinga jinga sijui tunaiga wapi wao badala ya badala ya kuiga vitu vizuri wanakuja na kikosi kazi kitembee na Machuma mjini inaonekana kabisa uwezo wetu wa kufikiri ni mdogo sana.
 
Nchi ya hovyo sana hii inashangaza huo upuuzi unaota mizizi ukiwaambia hizi ni mambo za kijinga wanakwambia tunakusanya Mapato na hivi vitu vya kijinga jinga sijui tunaiga wapi wao badala ya badala ya kuiga vitu vizuri wanakuja na kikosi kazi kitembee na Machuma mjini inaonekana kabisa uwezo wetu wa kufikiri ni mdogo sana...
yaani kuna mambo ya hovyo sijui hadi siku mtu atiwe ndosi ya ubongo ndipo wafute! Kuwaongezea stress watu pasipo sababu kabisa
 
yaani kuna mambo ya hovyo sijui hadi siku mtu atiwe ndosi ya ubongo ndipo wafute! Kuwaongezea stress watu pasipo sababu kabisa
2023 wajinga wanatembea na minyororo kukamata magari yanayolipa kodi kwenye mafuta karibu 26% yenyewe kuingia hiyo kodi yake Mlima Kilimanjaro harafu unakutana na muhuni ana chuma cha mnyororo Mjini unashangaa kabisa hawa vima si waende maporini huko watafutieni maeneo walime kuliko kupoteza nguvu kazi bure hiyo Parking waachiwe Trafiki tu wakipita wakiona Parking ya hovyo mtu apewe faini na maeneo ya biashara waachwe wanunuzi wakanunue na magari yao bila usumbufu wa Minyororo ya Wakoloni...
 
Kuna Tanroad wakishirikiana na Polisi njia ya Nelson Mandela, mitaa ya kuanzia Tabata Gereji mpaka TIOT. Dereva akipaki pembeni kwenye service road wanakamata gari na saa nyingine wanaivuta na Breakdown kisha utalipa gharama zote.

Polisi wanakuja full na risasi kisa gari lipo service road, sometimes wanakamata gari za transit za wageni na kuwafanyia harassment, tunaonekana watanzania sio watu wa kufikiri
 
Kuna Tanroad wakishirikiana na Polisi njia ya Nelson Mandela, mitaa ya kuanzia Tabata Gereji mpaka TIOT. Dereva akipaki pembeni kwenye service road wanakamata gari na saa nyingine wanaivuta na Breakdown kisha utalipa gharama zote.

Polisi wanakuja full na risasi kisa gari lipo service road, sometimes wanakamata gari za transit za wageni na kuwafanyia harassment, tunaonekana watanzania sio watu wa kufikiri
mbuzi wa bwana kheri shamba la bibi kheri ! tena wakiwa wanakamata utazani wamedaka jambazi sugu! Bongo nyoso
 
Siamini kabisa kwamba kuna wasomi walikaa sehemu wakajadili na kulipana posho za kikao kwamba:

Magari yanayodaiwa ushuru wa maegesho (parking) Yaanze kufungwa minyororo ili kushinikiza wamiliki kulipia tozo hizo.

Huu ni utaratibu wa hovyo sana

1. Huu utaratibu ni Hovyo kwasababu unatupunguzia wateja sisi wafanyabiashara Kariakoo, Ilala! Sisi wafanyabiashara tunalipia leseni manispaa, tunalipia zimamoto, tunalipia pesa za usafi, tunalipa kodi nyingi tu ili tufanye biashara, Mnapowafungia wateja wetu magari yao mnawatisha kwamba wasije ilala kwamba watakamatwa hili peke yake linatuondolea wateja katika biashara zetu.

2. Jambo jingine la kushangaza hivi nyie wachukua maokoto ya ushuru mmechangia nini kwenye kuwekeza maegesho hadi mchukue ushuru wa maegesho? Magari mengi yanaibiwa kwenye maegesho na ushuru wanalipa, agari yanaibiwa vipuri au taa yakiwa kwenye maegesho huo ushuru mnaolipwa je unafaida gani kwa mwenye chombo kama hamyalindi magari yao wala hamlipi fidia linapotokea janga au uharibifu?

3. Wizara na serikali kwa ujumla mlipopitisha huu utaratibu wa ushuru wa maegesho mlitegemea kwamba hawa wenye magari waendeshe halafu wakapark wapi!?

Gari ileile moja mnaitoza ushuru kibao hamuoni hiyo ni kero jaman
  • gari ileile mnaitoza ushuru wa kuingiza nchini (TRA)
  • Mnaitoza Ushuru wa kutumia barabara (road licence) kwenye kila lita moja ya mafuta mnafyeka sasa mnategemea huyu mtu akapaki porini?
  • Mnamchukua nenda kwa usalama
  • kwenye bima cha kwenu pia kipo na mengine mengi.
Mnataka hawa wenye magari waendeshe magari then wakapark wapi?

Huu utaratibu wa kutoza ushuru maegesho haupaswi kabisa kuwepo, ni utaratibu wa hovyo kabisa.

Mwenye gari katoka zake nyumbani kisitaarabu kufuata huduma kwa mfanya biashara halafu nyie kama serikali mnavalisha watu vibrauzi vya njano kwa kazi ya kufungia wateja wetu magari yao mnataka wateja tupate wapi wakiogopa kuja mijini?

Kwanini mnapenda kuifanya nchi yetu sote iwe kero kwa wengine jamani.
Ni kero kwakweli
 
Back
Top Bottom