Kuahirishwa BMK maana yake ipo wapi ??

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Sijui kilichosemwa mpaka ikafikia kuwa mchakato huo wa Katiba mpya usitishwe hadi baada ya uchaguzi mkuu ,suali ni jee utafutaji huo wa Katiba mpya utaanza ulipofikia au utaanza upya ?

Wananchi tunataka ukweli juu ya maoni tuliyoyatoa na kumkabidhi jaji Warioba na kundi lake ,Je ni maoni hayo ndio yatakayojadiliwa au ni makaburasha walioingia nayo Miccm ?

Tunahitaji kujua walichokubaliana ni kipi ? Hii katiba inayotafutwa si ya watu kujifungia na kutoka na heading ya maafikiano bila ya kujua kilichopelekea hata kufikia kutoa heading ni kitu gani ,Je inawezekana kuwa mchakato wa Katiba hauwezi kuanza tena upya hivi sasa kwa kuwa muda hautoruhusu au hicho kilichobakia hakiwezi kuhitimishwa japo hicho sicho kwani ahadi ya Sita ni kumkabidhi Mheshimiwa Kikwete Katiba mpya mwezi wa kumi mwaka huu.

Miccm imemaliza kasiki la Taifa na sasa wanamtwisha mzigo raisi mpya atakaekuja ,tutawafungulia mashtaka msifanye mchezo na hela ya taifa kana kwamba mnagawa visheti. Mlijua tokea mwanzo baada ya UKAWA kuchemka kuwa KATIBA haitopatikana ,ila mkaendelea kugawana hela za Taifa mkiita posho ,posho lakitatu kwa siku hata hizo nchi tajiri hazifanyi kufuru hiyo.

Wananchi tunahitaji kujua kilicho au kitakachoahirishwa na kuja tena ni kitu gani ???
 
Sijui kilichosemwa mpaka ikafikia kuwa mchakato huo wa Katiba mpya usitishwe hadi baada ya uchaguzi mkuu ,suali ni jee utafutaji huo wa Katiba mpya utaanza ulipofikia au utaanza upya ?

Wananchi tunataka ukweli juu ya maoni tuliyoyatoa na kumkabidhi jaji Warioba na kundi lake ,Je ni maoni hayo ndio yatakayojadiliwa au ni makaburasha walioingia nayo Miccm ?

Tunahitaji kujua walichokubaliana ni kipi ? Hii katiba inayotafutwa si ya watu kujifungia na kutoka na heading ya maafikiano bila ya kujua kilichopelekea hata kufikia kutoa heading ni kitu gani ,Je inawezekana kuwa mchakato wa Katiba hauwezi kuanza tena upya hivi sasa kwa kuwa muda hautoruhusu au hicho kilichobakia hakiwezi kuhitimishwa japo hicho sicho kwani ahadi ya Sita ni kumkabidhi Mheshimiwa Kikwete Katiba mpya mwezi wa kumi mwaka huu.

Miccm imemaliza kasiki la Taifa na sasa wanamtwisha mzigo raisi mpya atakaekuja ,tutawafungulia mashtaka msifanye mchezo na hela ya taifa kana kwamba mnagawa visheti. Mlijua tokea mwanzo baada ya UKAWA kuchemka kuwa KATIBA haitopatikana ,ila mkaendelea kugawana hela za Taifa mkiita posho ,posho lakitatu kwa siku hata hizo nchi tajiri hazifanyi kufuru hiyo.

Wananchi tunahitaji kujua kilicho au kitakachoahirishwa na kuja tena ni kitu gani ???

Hapo ndokila mtanzania mwenye kupenda taifa hili anajiuliza, wakirudi mchakato utaanzia wapi, kwenye haya matapishi au itabidi uanze upya?
 
WaTanzania hawana udhubutu viongozi hawa wanawajua fika wakuu lipo wazi wataendelea walipoishia.
 
WaTanzania hawana udhubutu viongozi hawa wanawajua fika wakuu lipo wazi wataendelea walipoishia.

Nionavyo watataka lianze upya ,unajua kwanini ? Ni posho tu ,labda ukawa wadai bunge zima lifumuliwe na wajumbe wasajiliwe upya na wachaguliwe kiufundi ,ikimaanisha wawe wasomi wasiofungamana na upande wowote kama inawezekana !
 
Nafikiri watajitahidi waikabidhi hivyo hivyo tu hata kama itakuwa haijakaa vizuri. La sivyo, baada ya uchaguzi wabunge wengi hawatakuwepo na kutakuwa na wabunge wengine wengi wapya. Na tukumbuke hawa wabunge ndio wajumbe wengi katika BMK. Sijui itakuwaje tu!
 
Back
Top Bottom