mi namshangaa hapendi ndoa kama nini huyu jamaa<br />
<br />
Kwahiyo wewe huoi/huolewi? Acha zako bana
Mwenzangu inabidi na sie tujifunze maana kila nikitaka kutoka nakwamia njiani na cancelSafi sana mashairi yametulia. Hongereni wote.
Uko fiti aiseemajuti ni mjukuu, babu yangu aliniasa
nenda wangu mjukuu, uachane na anasa
ukaweke lango kuu, ukafunge na vitasa
kama imekuwa fasheni, nani wa kulaumiwa?
vionjo unavitaka, ndoa unaitaka
wafanana na maji taka, yangu ndio mashaka
hata utoe zaka, milele una mashaka
kama hukuwa tayari, uliharakia nini?
Mwenzangu inabidi na sie tujifunze maana kila nikitaka kutoka nakwamia njiani na cancel
<br />mi namshangaa hapendi ndoa kama nini huyu jamaa
Jamani Dena u mzima, si unafahamu wewe ndio celebrity wa MMU, sisi tuliagana labda kukumbushia tu sasa lol!<br />
<br />
Hapo chacha ana matatizo huyu km ni mwanaume ni mbinafsi sana
<br />Jamani Dena u mzima, si unafahamu wewe ndio celebrity wa MMU, sisi tuliagana labda kukumbushia tu sasa lol!
Baada ya kuongea na rafiki zangu kadhaa, nimegundua kwamba ''Kuagana" imekuwa fasheni siku hizi.....Labda nawahukumu bure....
Ndoa ni kitu tukufu, misahafu ni shahidi,
Yataka moyo mkunjufu, hakuna mlio wa bundi,
Zawadi kama mikufu, tuzo njema kwa ushindi,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Zamani likuwa sifa, heshima liwekwa mbele,
Binti alifundwa vyema, katu sipige kelele,
Uwanja safi daima, watoto sipate upele,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Ndoa meingia doa, leo kuna kuagana,
Siku muhimu ya ndoa, wa zamani anapewa,
Penzi kama kukohoa, ni tabu kwa waungwana,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Kama wa zamani mzuri, kwanini hakukuoa,
Ka anukia uturi, nenda kapeleke posa,
Kwao huyu umekiri, kwa yule nataka poza,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Fungate haina mvuto, viungo vimelegea,
Ndoa sasa ni kipato, na bado utamegewa,
Ni moto pia fukuto, la upate ngekewa,
Kuagana na wa zamani, siku hizi imeshakuwa fasheni?
Mwenzangu inabidi na sie tujifunze maana kila nikitaka kutoka nakwamia njiani na cancel
siku hizi watu hawana condidence kabisaa na ndoa,kila mtu amekaa kimachale machale/anaibiwa....msifunge ndoa kama mko uncertain:majani7:
Big up Ngondya,hata mimi sijasomea chochote kwenye ushairi zaidi somo la kiswahili la primary school and "O" level.
Msiogope kujaribu,tena utaona misamiati na maneno yanaflow tu,ndicho kinachonitokea mimi.:smiling:
Ni kweli kabisa, mfano mzuri ni Mjomba Mpoto, anavyoongea ni kama amekaa darasani sana kuisomea lugha hii, lakini ukweli ni kwamba amejifunza mengi kwa kujisomea mwenyewe nyumbani. Ukijifunza kuandika, unakuwa unafurahia-inakuwa kama hobby.
Mmmh, kuna ukweli ndani yake. Kabla ya send off anaagwa nusu, kabla ya harusi anaagwa full, baada ya ndoa anakaribishwa kwenye ulimwengu wa wizi na risk ya kufumaniwa.