Kongamano la Katiba Mpya- Ukumbi wa Kiramuu Mbezi beach

Mh. Halima mdee amemaliza kuongea.
Kwa ufupi amezungumzia mchakato mzima wa upitishwaji wa muswaada kuanzia kwenye kamati ya bunge ambapo spika alikiuka kanuni za bunge na kuongeza wajumbe watano baada ya hoja ya kutaka muswada usomwe kwa mara ya kwanza kuelekea kukubaliwa na wajumbe wa kamati ya sheria na katiba. Pia amezungumzia spika alivyopora madaraka ya kamati na kufanya maamuzi na watu wake wachache ili kuhakikisha muswada unapita.

Pia amefichua siri kwamba baada ya yeye na mh. Lisu kuainisha mapungufu ya sheria ya mchakato wa katiba, wabunge wa ccm walikiri mapungufu hayo lakini wakadai wameelekezwa kuupitisha muswada kama ulivyo.

Ameeleza sababu ya kuweka kipengele cha adhabu kwa mtu mwingine yeyote atakayetoa elimu ya uraia juu ya mchakato wa katiba ni kwa nia ya kuwadhibiti chadema baada ya kugundua kwamba chadema watatumia mapungufu ya sheria hii kuwaelimisha wananchi na huenda katiba ''mpya'' wanayotaka wao isipitishwe.

Amemalizia kwa kusema chadema tuko tayari kwa lolote maadam tunatekeleza wajibu wetu wa kikatiba.
 
Wadau,
Leo tarehe 18/12/2011 katika ukumbi wa Kiramuu uliopo mbezi beach high school, kunafanyika kongamano la katiba mpya, lililoandaliwa na kuendeshwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Wazungumzaji wakuu ni katibu mkuu wa chama Dr. Slaa, Mbunge wa Ubungo Mh. Mnyika na mjumbe wa kamati kuu Wakili Mabere Marando.

Kongamano hilo limejumuisha wanachama wa chadema mikoa (ya kichama) ya Ilala, Kinondoni na Temeke.

Kwa wale walio karibu na ukumbi ama wanaoweza kufika wanakaribishwa.

Sasahivi zoezi la usajili linaelekea kukamilika na kongamano litaanza muda mfupi ujao.
Nawasilisha.

Mwita Maranya, asante kwa taarifa na update. Japo naishi mtaa wa pili nyuma ya Kiramuu, nyuma ya nyumba Mboya, bado siwezi kuhudhuria Kongamano hili, nadhani ni inside matters kwa members na followes only na sio public forum kwa yeyote ila nafuatilia update zako.

Thanks.
 
Sasa ni muda wa maswali na majibu.
Yameulizwa maswali kuhusu sheria ya mchakato wa katiba, mambo ya muungano, mazungumzo ya chadema na raisi kikwete na mambo ya uimarishaji na utekelezaji wa program za maendeleo ya chama.
 
Mwita Maranya, asante kwa taarifa na update. Japo naishi mtaa wa pili nyuma ya Kiramuu, nyuma ya nyumba Mboya, bado siwezi kuhudhuria Kongamano hili, nadhani ni inside matters kwa members na followes only na sio public forum kwa yeyote ila nafuatilia update zako.

Thanks.

Ahsante Pasco na karibu tena mara nyingine.
Kongamano ni kwa wanachama wa chadema tu ingawa mwanzoni wanahabari waliruhusiwa kuingia na kuchukua habari ambazo bila shaka wataziripoti kwa ufasaha zaidi kwa manufaa ya umma wa watanzania.
 
CHAMA cha NCCR- Mageuzi kimeomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete kwa nia ya kutoa mawazo yake kuhusu mchakato wa kutungwa kwa Katibu mpya ya Tanzania, kama ilivyoahidiwa kwa wananchi na Rais mwenyewe mwishoni mwa mwaka jana.

Aidha, Baraza la Taifa la Taasisi zisizokuwa za Kiserikali (NGOs) limeomba kukutana na kuzungumza na Rais kuhusu mchakato huo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu, Rais Kikwete ameyakubali maombi yote mawili na ameagiza wahusika kupanga mikutano hiyo kati yake na NCCR-Mageuzi na kati yake na Baraza la Taifa la NGOs.

Tayari Rais amekutana na uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHDEMA) na ule wa Chama cha Wananchi (CUF) kuhusu mchakato huo baada ya kuwa ameomba kukutana na viongozi wa vyama hivyo.

Mikutano kati ya Rais na viongozi wa vyama hivyo viwili ilimalizika kwa maridhiano na maelewano juu ya namna bora zaidi ya kusukuma mchakato huo kwa namna inavyofaa kwa mustakabali wa nchi.
 
hii ni kuhakikisha polisi magamba hawapati taarifa za kiinteleginsia lol!!!
Hii intelijensia ya magamba itatumaliza... mimi nipo dk tatu kutoka kwenye huu ukumbi lakini mpaka leo ndiyo najua hii habari...nashangaa hata hapa ilinipitia pembeni! Kwa kweli inabidi kutoa matangazo mapema.
 
Back
Top Bottom