Mziray, msomi wa fani ya Elimu ya Viungo (PE), aliyewahi kuwa Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alijiunga na Simba hivi karibuni kuimarisha benchi la ufundi la timu hiyo.
Kutokana na kuugua, Mziray alishindwa kushiriki maandalizi ya kuelekea mechi ya watani wa jadi, Simba na Yanga iliyochezwa Oktoba 16 ambayo Simba ilifungwa bao 1-0.
Kocha huyo aliyewahi kuzinoa timu mbalimbali zikiwemo za Simba, Yanga na Sigara, ndiye kocha wa mwisho kuibebesha Bara ubingwa wa Kombe la Chalenji mwaka 1994.
Bara ilitwaa ubingwa mwaka huo ukiwa wa pili katika historia ya michuano hiyo tangu mwaka 1973 ilipoutwaa kwa jina hilo kutoka Gossage Cup. Mara ya kwanza ilikuwa mwaka 1974. Utakumbukwa kwa mengi hasa la la kuiwezesha taifa stars kushinda kombe la challenge, Once again R.I.P Super Coach
Kwa habari za haraka haraka tu, Kocha na mhadhiri wa michezo UDSM ndo kasharudisha namba kwa mhukumu wa haki! Bwana ametoa na sasa ametwaa, jina lake libarikiwe! Tujiulize sie tulIobaki, WHO IS NEXT???????
Inallilah wainailahi rajiuun hakika sisi ni wa MwenyeziMungu na kwake tutarejea.... nawatakia subra ndugu jamaa na marafiki na watanzania wote kwa ujumla.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.