hakuna kiwanja cha ukubwa huo kilichopimwa maana huo ni sawa na ukubwa wa sebule ya maana.hiyo lazima iwe ni mita.kuwa makini.je umepima mwenyewe au eneo lote limepimwa nikimaanisha na majirani zako
Hizo ni mita kwa kutumia hatua za miguu na ndio vipimo vinavyotumika vijijini kuuziana mashamba ila ukiwa na mpimaji mwenye miguu mirefu unafanikiwa kupata kiwanja kikubwa zaidi. Kiwanja chenye hati kinapimwa kwa vipimo vya kisasa kwa kutumia kamba maalumu ya kupimia (tape measure).
Unajua nimecheka mpaka basi: mmemuuliza kimepimwa akasema ndiyo urefu 25 upana 30 tena kwa kushirikiana na majirani zake. Mimi pia nimepima cha kwangu 50 kwa 50 kwa kuwashirikisha majirani (ila sikiuzi). Au labda wauliza swali waweke wazi nani kapima? Ardhi au mwenye kiwanja?
atakuwa kapima mwenye kiwanja, sio mamlaka ya arthi. na hizo hati zitakuwa si za serekali. anyway kwa iyo bei, si mbaya kama utanunua alafu ukapime mwenyewe. what matters ni uhakika kwenye uuzwaji usije ukaingia cha kike, maana skuizi hadi wazee wa miaka 60 matapeli.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.