Ni Asubuhi tulivu ya siku ya Alhamisi.
Kiongozi mkuu wa Upinzani Freeman Mbowe anatarajiwa kuletwa mahakamani Kisutu Leo katika Kesi ya Ugaidi.
Kesi hii inavuta kila mpenda haki na mwanademokrasia kutokana na ukweli Mbowe amebambikizwa kesi hii ili kumnyamazisha kutokana na Kampeni aliyoasisi ya Kudai Katiba Mpya
Mahakama hii inatarajiwa kufurika umati mkubwa wa watu kulaani unyama na uonevu wa vyombo vya dola.Ikumbukwe ni juzi tu bila Aibu alijitokeza IGP Simon Sirro na kuingilia mhimili wa Mahakama kwa kumhukumu Mbowe huku akijua kesi iko mahakamani.
Watu wengine wanaotarajiwa kufurika Kisutu ni Wawakilishi kutoka Jumuiya ya Ulaya, Marekani na balozi kadhaa nchini huku vyombo vikubwa vya Habari Duniani BBC, VOA, DW na Aljazeera vikitarajiwa kuwa live mahakamani.
Molemo media tayari iko kwenye viwanja vya Mahakama hii kuwaletea kila kinachojiri.
Updates
Imethibitishwa kwamba Freeman Mbowe hataletwa mahakamani na badala yake kesi inaendeshwa kwa njia ya Mtandao (Video Conference)
Taarifa za Uhakika ni kwamba dola Wana hofu kubwa kumleta Mbowe Mahakamani kutokana na Hasira ya wananchi.
Pamoja na vitisho vya IGP Simon Sirro alivyotoa juzi dhidi ya watakaohudhuria mahakamani Kisutu na kuongea uongo mwingi dhidi ya Mbowe lakini Leo idadi kubwa ya watu imehudhuria mahakamani na wengine wakiendelea kumiminika kabla ya kuanza kuondoka baada ya Taarifa kwamba kesi itaendeshwa kimtandao.
Kamanda wa Polisi DSM Muliro Jumanne alifika mapema Kisutu kuona Hali ya mambo huku kukiwa na Askari zaidi ya 100 wenye silaha na wengine waliovalia kiraia.
Pamoja na Serikali kuogopa kumleta Mbowe Mahakamani lakini ni wazi Kelele za umma unaotaka haki zimewatisha na kuwaogofya
Kesi Yaahirishwa
Ilipotimu saa 4 na dakika 20 kesi Imeahirishwa hadi kesho Ijumaa tarehe 6 August saa 3 Asubuhi kutokana na kile kilichoelezwa ni matatizo ya kimtandao
=====
KISUTU, DAR: Kesi ya Freeman Mbowe (CHADEMA) imeahirishwa hadi Kesho kutokana na muonekano hafifu wa Video Conference kati ya Mahakama ya Kisutu na gereza la Ukonga
Watuhumiwa wataletwa kesho saa 3 asubuhi mahakamani (Physically) na taratibu nyingine za kisheria zitafata.
Kiongozi mkuu wa Upinzani Freeman Mbowe anatarajiwa kuletwa mahakamani Kisutu Leo katika Kesi ya Ugaidi.
Kesi hii inavuta kila mpenda haki na mwanademokrasia kutokana na ukweli Mbowe amebambikizwa kesi hii ili kumnyamazisha kutokana na Kampeni aliyoasisi ya Kudai Katiba Mpya
Mahakama hii inatarajiwa kufurika umati mkubwa wa watu kulaani unyama na uonevu wa vyombo vya dola.Ikumbukwe ni juzi tu bila Aibu alijitokeza IGP Simon Sirro na kuingilia mhimili wa Mahakama kwa kumhukumu Mbowe huku akijua kesi iko mahakamani.
Watu wengine wanaotarajiwa kufurika Kisutu ni Wawakilishi kutoka Jumuiya ya Ulaya, Marekani na balozi kadhaa nchini huku vyombo vikubwa vya Habari Duniani BBC, VOA, DW na Aljazeera vikitarajiwa kuwa live mahakamani.
Molemo media tayari iko kwenye viwanja vya Mahakama hii kuwaletea kila kinachojiri.
Updates
Imethibitishwa kwamba Freeman Mbowe hataletwa mahakamani na badala yake kesi inaendeshwa kwa njia ya Mtandao (Video Conference)
Taarifa za Uhakika ni kwamba dola Wana hofu kubwa kumleta Mbowe Mahakamani kutokana na Hasira ya wananchi.
Pamoja na vitisho vya IGP Simon Sirro alivyotoa juzi dhidi ya watakaohudhuria mahakamani Kisutu na kuongea uongo mwingi dhidi ya Mbowe lakini Leo idadi kubwa ya watu imehudhuria mahakamani na wengine wakiendelea kumiminika kabla ya kuanza kuondoka baada ya Taarifa kwamba kesi itaendeshwa kimtandao.
Kamanda wa Polisi DSM Muliro Jumanne alifika mapema Kisutu kuona Hali ya mambo huku kukiwa na Askari zaidi ya 100 wenye silaha na wengine waliovalia kiraia.
Pamoja na Serikali kuogopa kumleta Mbowe Mahakamani lakini ni wazi Kelele za umma unaotaka haki zimewatisha na kuwaogofya
Kesi Yaahirishwa
Ilipotimu saa 4 na dakika 20 kesi Imeahirishwa hadi kesho Ijumaa tarehe 6 August saa 3 Asubuhi kutokana na kile kilichoelezwa ni matatizo ya kimtandao
=====
KISUTU, DAR: Kesi ya Freeman Mbowe (CHADEMA) imeahirishwa hadi Kesho kutokana na muonekano hafifu wa Video Conference kati ya Mahakama ya Kisutu na gereza la Ukonga
Watuhumiwa wataletwa kesho saa 3 asubuhi mahakamani (Physically) na taratibu nyingine za kisheria zitafata.