Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Leo Marietha anatimiza miaka 50 kamili na ana watoto 4 wakubwa wanaojitegemea na ametengana na mume wake kwa mwaka wa 10 sasa. Marietha ni mwanamke msomi na mjasiriamali na pia ni mwanaharakati! Miaka 30 iliyopita kuna tukio lililomtokea Marietha ambalo ndilo hasa nataka kushiriki nanyi kwenye siku yake hii ya kuzaliwa. Awali ya yote "Happy Birthday" Marietha!!
Mwaka 1981 wakati huo Marietha akiwa ni binti wa miaka 19 alikuwa amemaliza masomo ya sekondari Kidato cha Sita na anangojea kujiunga na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria. Wakati huo Marietha alikuwa ana Boy Friend wake waliokuwa wanapendana sana tena sana ambaye naye alikuwa amemaliza kidato cha Sita kama yeye Marietha.
Lakini katikakati ya Mahusiano yao hayo akatokea Bwana mmoja ambaye anamzidi Marietha kwa miaka 6 na kumrubuni Marietha aachane na mpenzi wake kwa ahadi na zawadi mbalimbali. Katikati ya Mahusiano hayo mapya Marietha akashika ujauzito. Lakini bila ya kumjulisha mpenzi wake wa awali kwamba ni mjamzito.
Kabla ya kwenda JKT mpenzi wake wa zamani akagundua kwamba Marietha ni mjamzito, na alipombana amueleze ni ujauzito wa nani Marietha maji yakazidi unga akamtaja jamaa aliyemrubuni ambaye wakati huo alikuwa anasomea Diploma yake ya uhasibu pale IFM. Yule mpenzi wake wa awali akakubali kwamba walee ile mimba mpaka mtoto atakapozaliwa halafu waendelee na uhusiano wao kwa lengo la kujenga familia yao pamoja na mtoto wa yule jamaa.
Hayo yote yakitokea Marietha hakuwahi kumwambia yule aliyempa mimba kama ana uhusiano na mtu mwingine. Siku moja kabla ya kwenda JKT yule mpenzi wake alimtembelea Marietha nyumbani kwao kwa nia ya kumuaga, wakati huo Marietha alikuwa anaishi kwa wazazi wake kwenye Maghorofa ya NHC (zama hizo Msajili wa Majumba) maeno ya Faya.
Baada ya maongezi na kuagana kwingi Marietha alimsindikiza Mpenzi wake huyo hadi kituo cha Basi Faya, na walipoagana jamaa akawa anavuka upande wa Pili wa barabara ili akapande UDA za kwenda Ubungo. Alipokuwa anavuka barabara gari moja likitokea maeneo ya Posta kwa kasi lilimgonga na kufariki papo hapo!!
Kishindo kile cha kugongwa kilimstua Marietha na alipogeuka alimuona Mwanaume aliyempenda amelala chini kwenye dimbwi la damu akiwa hana uhai tena. Ingawa Marietha aliolewa na yule aliyempa Mimba na kufanikiwa kuongeza watoto wengine watatu lakini mpaka leo anasema kila inapofika siku aliyogongwa mpenzi wake yule hufanya kumbukumbu ya kibinafsi. Bahati MBAYA sana kwake siku hiyo ni siku yake pia ya kuzaliwa!! Happy Birthday Marietha!!
Mwaka 1981 wakati huo Marietha akiwa ni binti wa miaka 19 alikuwa amemaliza masomo ya sekondari Kidato cha Sita na anangojea kujiunga na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria. Wakati huo Marietha alikuwa ana Boy Friend wake waliokuwa wanapendana sana tena sana ambaye naye alikuwa amemaliza kidato cha Sita kama yeye Marietha.
Lakini katikakati ya Mahusiano yao hayo akatokea Bwana mmoja ambaye anamzidi Marietha kwa miaka 6 na kumrubuni Marietha aachane na mpenzi wake kwa ahadi na zawadi mbalimbali. Katikati ya Mahusiano hayo mapya Marietha akashika ujauzito. Lakini bila ya kumjulisha mpenzi wake wa awali kwamba ni mjamzito.
Kabla ya kwenda JKT mpenzi wake wa zamani akagundua kwamba Marietha ni mjamzito, na alipombana amueleze ni ujauzito wa nani Marietha maji yakazidi unga akamtaja jamaa aliyemrubuni ambaye wakati huo alikuwa anasomea Diploma yake ya uhasibu pale IFM. Yule mpenzi wake wa awali akakubali kwamba walee ile mimba mpaka mtoto atakapozaliwa halafu waendelee na uhusiano wao kwa lengo la kujenga familia yao pamoja na mtoto wa yule jamaa.
Hayo yote yakitokea Marietha hakuwahi kumwambia yule aliyempa mimba kama ana uhusiano na mtu mwingine. Siku moja kabla ya kwenda JKT yule mpenzi wake alimtembelea Marietha nyumbani kwao kwa nia ya kumuaga, wakati huo Marietha alikuwa anaishi kwa wazazi wake kwenye Maghorofa ya NHC (zama hizo Msajili wa Majumba) maeno ya Faya.
Baada ya maongezi na kuagana kwingi Marietha alimsindikiza Mpenzi wake huyo hadi kituo cha Basi Faya, na walipoagana jamaa akawa anavuka upande wa Pili wa barabara ili akapande UDA za kwenda Ubungo. Alipokuwa anavuka barabara gari moja likitokea maeneo ya Posta kwa kasi lilimgonga na kufariki papo hapo!!
Kishindo kile cha kugongwa kilimstua Marietha na alipogeuka alimuona Mwanaume aliyempenda amelala chini kwenye dimbwi la damu akiwa hana uhai tena. Ingawa Marietha aliolewa na yule aliyempa Mimba na kufanikiwa kuongeza watoto wengine watatu lakini mpaka leo anasema kila inapofika siku aliyogongwa mpenzi wake yule hufanya kumbukumbu ya kibinafsi. Bahati MBAYA sana kwake siku hiyo ni siku yake pia ya kuzaliwa!! Happy Birthday Marietha!!