Kisa cha Double Agent Juma Zangira na afande wa polisi, Abdallah Mssika

TAJIRI MKUU WA MATAJIRI

JF-Expert Member
Dec 1, 2010
5,720
10,218
Mwite Juma Thomas Zangira, Komando mpelelezi wa kwanza Tanzania aliyekamatwa baada ya kuwa anavujisha siri za nchi. Alikamatwa mwaka 1977 akiwa ndio amekwenda Posta kupokea barua yake ya mwisho ambayo ilikuwa imebeba maelekezo mengi na mipango ya kijasusi.

1685706402051.jpg

Aliyemkamata ni Afisa wa Polisi, Bwana Abdallah Mssika. Kabla ya kumkamata Jasusi huyu pia alipewa mafunzo ya namna gani ya kujihami kwa lolote lile ambalo lingetokea mbele yake,katika interview yake Mssika anaeleza alipewa somo la kumsoma kwanza yeye alivyo,namna gani anaweza kutumia miguu yake au mikono yake kwa kujihami. Hasa akaaelezwa anatumia sana mkono wa kushoto, hivyo akafunzwa kwanza namna ya mkao atakapokuwa nyuma yake,awe mwepesi kujihami. Mzee Mssika hata kuhusu mlo wa chakula chake ulibadilishwa ili tu kumjenga kufocus kwenye mission hiyo ya kumkamata Komando Zangira.

Kazi ya kumfuatilia ilichukua muda mrefu takribani miaka 6, Bwana Zangira hakuwa anajua kama anafuatiliwa. Kila barua aliyokwenda kupokea ilikuwa tayari wameshaipata kisha kuitoa copy,hata fedha alizokuwa anatumiwa walizibaini ni kiasi gani. Barua zote alizokuwa akitumiwa zilitoka South Africa, ila hapo kabla walijua zinatoka London. Kumbe London zilipitia tu ili isijulikane ni wapi zinatoka,ilikuja kufahamika baada ya kukamatwa Bwana Zangira.

Baada ya Serikali kujiridhisha kuwa ni kweli Jasusi Zangira anafanya usaliti, basi oda ikatolewa akamatwe! Ndipo Afisa huyo wa Polisi,Bwana Abdallah Mssika alipoenda yeye na wenzake wakiwa wanamfuata nyuma. Komando Zangira alipofika Posta akafungua sanduku la barua,alipoitoa tu tayari aliamuliwa anyoshe mikono juu,haraka sana magari yaliyokuwa yameandaliwa kwaajili ya ulinzi yalifika.

Komando Zangira alinyang'anywa ile barua na haraka sana akaweka ndani ya gari. Kabla ya kupandishwa ndani ya gari walifanyiwa searching na hukutwa na silaha,pia alifanyiwa searching kwenye mdomo maana Jasusi akiwa kwenye mission za kusaliti mara nyingi huwa anachukua tahadhari hata atakapokamatwa aweze kujihami au hata kujidhuru. Anaweza kuwa na kitu chochote mdomoni, akifanikisha kunga'ata tu au kukikandamiza basi habari inakuwa imekwisha hapo hapo.

Hivyo basi Jasusi Zangira alikamatwa akiwa salama na kufikishwa sehemu husika,baadae alihukumiwa kifungo cha maisha jela.
 
Mwite Juma Thomas Zangira, Komando mpelelezi wa kwanza Tanzania aliyekamatwa baada ya kuwa anavujisha siri za nchi. Alikamatwa mwaka 1977 akiwa ndio amekwenda Posta kupokea barua yake ya mwisho ambayo ilikuwa imebeba maelekezo mengi na mipango ya kijasusi.

View attachment 2643507
Aliyemkamata ni Afisa wa Polisi, Bwana Abdallah Mssika. Kabla ya kumkamata Jasusi huyu pia alipewa mafunzo ya namna gani ya kujihami kwa lolote lile ambalo lingetokea mbele yake,katika interview yake Mssika anaeleza alipewa somo la kumsoma kwanza yeye alivyo,namna gani anaweza kutumia miguu yake au mikono yake kwa kujihami. Hasa akaaelezwa anatumia sana mkono wa kushoto, hivyo akafunzwa kwanza namna ya mkao atakapokuwa nyuma yake,awe mwepesi kujihami. Mzee Mssika hata kuhusu mlo wa chakula chake ulibadilishwa ili tu kumjenga kufocus kwenye mission hiyo ya kumkamata Komando Zangira.

Kazi ya kumfuatilia ilichukua muda mrefu takribani miaka 6, Bwana Zangira hakuwa anajua kama anafuatiliwa. Kila barua aliyokwenda kupokea ilikuwa tayari wameshaipata kisha kuitoa copy,hata fedha alizokuwa anatumiwa walizibaini ni kiasi gani. Barua zote alizokuwa akitumiwa zilitoka South Africa, ila hapo kabla walijua zinatoka London. Kumbe London zilipitia tu ili isijulikane ni wapi zinatoka,ilikuja kufahamika baada ya kukamatwa Bwana Zangira.

Baada ya Serikali kujiridhisha kuwa ni kweli Jasusi Zangira anafanya usaliti, basi oda ikatolewa akamatwe! Ndipo Afisa huyo wa Polisi,Bwana Abdallah Mssika alipoenda yeye na wenzake wakiwa wanamfuata nyuma. Komando Zangira alipofika Posta akafungua sanduku la barua,alipoitoa tu tayari aliamuliwa anyoshe mikono juu,haraka sana magari yaliyokuwa yameandaliwa kwaajili ya ulinzi yalifika.

Komando Zangira alinyang'anywa ile barua na haraka sana akaweka ndani ya gari. Kabla ya kupandishwa ndani ya gari walifanyiwa searching na hukutwa na silaha,pia alifanyiwa searching kwenye mdomo maana Jasusi akiwa kwenye mission za kusaliti mara nyingi huwa anachukua tahadhari hata atakapokamatwa aweze kujihami au hata kujidhuru. Anaweza kuwa na kitu chochote mdomoni, akifanikisha kunga'ata tu au kukikandamiza basi habari inakuwa imekwisha hapo hapo.

Hivyo basi Jasusi Zangira alikamatwa akiwa salama na kufikishwa sehemu husika,baadae alihukumiwa kifungo cha maisha jela.
Enzi hizo TISS ya Emilio Mzena inafanya kazi kama kikosi cha ulinzi wa Rais Ikulu
 
Kwamba hua wana vitu mdomoni au wanajing'ata ulimi wafe ni stori zisizo na uthibitisho
Atakuwa anamaanisha vidonge vya sumu, ukikirusha mdomoni na kukitafuta ni sekunde tuu mtu anavuta...
 
Mimi nimejiuliza alikuwa anavujisha siri gani za maana za nchi masikini kama tz?au alitaka kuvujisha ile siri ya mwl nyerere kuuza sehemu ya tanzania bara kwa z'bar ambayo kwa sasa imewapiga marufuku wa tanzania bara kufanya shughuki yeyote
 
Kipindi kile Nyerere anawafadhili wapiganaji wa ukombozi kusini mwa bara la africa especially africa kusini kwa kaburu

Kaburu alitaka atumie shortcut kuwamaliza pmj na kutangaza base yao

Kumbuka kwenye medani za vita adui anaweza akaingilia hata mfumo wa chanzo cha maji mnachotumia akatumbukiza sumu mteketee wote
Mimi nimejiuliza alikuwa anavujisha siri gani za maana za nchi masikini kama tz?au alitaka kuvujisha ile siri ya mwl nyerere kuuza sehemu ya tanzania bara kwa z'bar ambayo kwa sasa imewapiga marufuku wa tanzania bara kufanya shughuki yeyote
 
Kuna sumu inaitwa cyanide majasusi wanatumiaga kinakuwa ni kidonge kidogo sana kinaweza kukaa mdomoni na mtu asijue.Ikiwa akikamatwa akakingata anakufa hapohapo ,cyanide ni moja ya sumu mbaya sana duniani.Wakati wa Hilter makamanda,wanajeshi,majasusi wake nk walikuwa wanatumia hii sumu ili kuepuka kufa kwa mateso na kutoa siri ikiwa watakamatwa na maadui
 
Mimi nimejiuliza alikuwa anavujisha siri gani za maana za nchi masikini kama tz?au alitaka kuvujisha ile siri ya mwl nyerere kuuza sehemu ya tanzania bara kwa z'bar ambayo kwa sasa imewapiga marufuku wa tanzania bara kufanya shughuki yeyote
Uliza ujibiwe mkuu
 
Back
Top Bottom