Kipindupindu chatikisa Rukwa; Mmoja afariki, 20 walazwa

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,252
Rukwa.jpg

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine ishirini wamelazwa kwenye zahanati ya kijiji cha Samazi,katika wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa,kufuatia kuibuka kwa ugonjwa wa kipindupindu kwenye kijiji hicho,kilichoko kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika.

Mganga mkuu wa mkoa wa Rukwa Dakta Boniface Kasululu,akiwa ameongozana na mkuu wa mkoa huo Bw Zelote Steven akizungumza kijijini Samazi,amethibitisha kuwa mlipuko huo wa kuhara na kutapika ni ugonjwa wa kipindupindu, na kwamba tayari wametenga mahali pa kuwalaza wagonjwa waliokumbwa na ugonjwa huo kwa ajili ya tiba,huku mkuu wa mkoa huyo akipiga marufuku tiba za kienyeji,na wengine kwa imani zao wakiwaombea wagonjwa na kuwachelewesha kwenda kupata tiba.

Baadhi ya wananchi wakiongea kijijini hapo Samazi,wamesema wanakabiliwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa maji safi na salama,na hivyo kulazimika kuyatumia maji ya ziwa tanganyika kwa shughuli zao zote,ambayo sio salama kabisa kwa vile yanachafuliwa mno kwa watu wengi kuligeuza ziwa hilo kuwa choo.

Chanzo: ITV
 
Mtu mmoja amefariki dunia na wengine ishirini wamelazwa kwenye zahanati ya kijiji cha Samazi,katika wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa,kufuatia kuibuka kwa ugonjwa wa kipindupindu kwenye kijiji hicho,kilichoko kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika.

Mganga mkuu wa mkoa wa Rukwa Dakta Boniface Kasululu,akiwa ameongozana na mkuu wa mkoa huo Bw Zelote Steven akizungumza kijijini Samazi,amethibitisha kuwa mlipuko huo wa kuhara na kutapika ni ugonjwa wa kipindupindu, na kwamba tayari wametenga mahali pa kuwalaza wagonjwa waliokumbwa na ugonjwa huo kwa ajili ya tiba,huku mkuu wa mkoa huyo akipiga marufuku tiba za kienyeji,na wengine kwa imani zao wakiwaombea wagonjwa na kuwachelewesha kwenda kupata tiba.

Baadhi ya wananchi wakiongea kijijini hapo Samazi,wamesema wanakabiliwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa maji safi na salama,na hivyo kulazimika kuyatumia maji ya ziwa tanganyika kwa shughuli zao zote,ambayo sio salama kabisa kwa vile yanachafuliwa mno kwa watu wengi kuligeuza ziwa hilo kuwa choo.

Chanzo: ITV

hii habari sio nzuri kabisa, wananchi inabidi waelimishwe kuhusu usafi
 
Back
Top Bottom