Kinana awa Katibu Mkuu mpya wa CCM! Meghji na Migiro waula...

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,048
144,454
New CCM Secretariat:

Secretary General:
Kinana;
Deputy
Secretary General: Mwigulu;
Deputy
Secretary General: Ali Vuai;
Foreign:
Migiro;
Finance:
Meghji;
Organisation:
M.S.Khatib;
Publicity:
Nape



Previously:
  • Mukama kung'olewa, nyota ya Nape yang'ara

WAKATI mjadala wa nani anatoka katika uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na nani anaingia, hususan katika sekretariati mpya ya chama hicho ukiwa umeshika kasi, jina la Abdulhaman Kinana limetajwa kuwa huenda akateuliwa kushika nafasi hiyo.

Kitendawili cha mjadala huo ulio gumzo ndani na nje ya CCM, kinatarajiwa kinateguliwa leo na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Rais Jakaya Kikwete.

Tayari Rais Kikwete ameshamteua Katibu Mkuu wa zamani, Philip Mangula, kuwa Makamu Mwenyekiti, akirithi mikoba ya Pius Msekwa, mwanasiasa mkongwe na mzoefu akiwa na rekodi ya kuwahi kuwa Katibu Mtendaji Mkuu wa kwanza wa CCM.

Hii ni mara ya pili kwa jina la Kinana kuchomoza kuwa mtu anayefaa kushika nafasi hiyo kwani miaka miwili iliyopita wakati Rais Kikwete alipovunja Kamati Kuu (CC) na sekretarieti na kuziunda upya, Kinana alitajwa kuwa angeteuliwa kushika wadhifa huo.

Hata hivyo, Rais Kikwete alimteua Willson Mukama, akirithi mikoba ya Mzee Yusuf Makamba.

Duru za siasa kutoka ndani ya CCM, zinasema kuwa kwa sasa Mukama anaonekana kushindwa kumudu uendeshaji wa siasa za sasa, ikiwa ni dhahiri ameshindwa kumudu siasa za jukwaani.

Habari za ndani ya CCM ambazo gazeti hili imezipata, zilisema kuwa jina la Kinana ni moja ya majina yaliyopendekezwa na Makamu Mwenyekiti mpya, Mangula, ambaye anaelezwa kumpa masharti Rais Kikwete ya kufanya kazi na Katibu Mkuu atakayesimamia maamuzi yake.

"Jina la Kinana limetokana na masharti ya Mangula ambaye alimwambia Jakaya kwamba anataka kufanya kazi na katibu atakayeweza kusimamia maamuzi yake hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwaka 2015," kilisema chanzo chetu cha habari.

Sifa moja kubwa anayotajwa kuwa nayo Kinana ni msimamo mkali dhidi ya masuala ya ufisadi na kubwa zaidi anatajwa kuwa bingwa wa mikakati ya kisiasa ndani ya chama hicho.

Itakumbukwa kuwa Kinana ndiye aliyeongoza kampeni za Benjamin Mkapa mwaka 1995, dhidi ya Augustine Mrema, aliyekuwa mwanasiasa maarufu na aliyekubalika kwa wakati huo.

Tangu wakati huo, Kinana amekuwa akiongoza kampeni za urais. Ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM anayetajwa kusimamia mawazo anayoamini ni sahihi, lakini akiwa tayari kuunga mkono hoja zenye lengo la kukijenga chama hicho.

Hata hivyo, Kinana alipata kukaririwa kwamba anang'atuka siasa baada ya kuwa mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) kwa miaka 25 mfululizo.

Mbali ya Kinana, jina lingine linalotajwa kushika nafasi hiyo ni la Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.

Nyota ya Nape Nnauye ndiyo inayong'ara zaidi akitajwa kuchangamsha siasa za jukwaani na za kiutendaji za chama hicho.

Nape anapewa nafasi kubwa kutokana na uwezo wake kisiasa, lakini pia ni kutokana na kuungwa mkono na vijana wengi hata nje ya chama hicho, ambao kimsingi, ndio wanaobeba jahazi la kisiasa nchini.

Mabadiliko mengine yanatajwa katika nafasi ya Katibu ya Uchumi na Fedha ambayo kwa sasa inashikiliwa na Mwigulu Nchemba.

Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa, naye anatajwa kuweza kumng'oa Mwigulu.

Mwigulu anatajwa kushindwa kukiwezesha chama hicho kuacha kutegemea ruzuku kuendesha shughuli zake.

Tangu ashike wadhifa huo, Mwigulu anatajwa kuendesha shughuli nyingine za kisiasa na kusahau jukumu la msingi la kufufua uchumi wa chama hicho chenye rasilimali nyingi nchini.

Kwenye nafasi ya Itikadi na Uenezi, ambayo jina la Nape nalo linatajwa, linaweza pia kuchukuliwa na William Ngeleja, William Lukuvi na Katibu wa Vijana wa CCM (UVCCM), Martine Shigela.

Katika hatua nyingine, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, amelazima kutumia nguvu ya ziada kuwalainisha wajumbe wa mkutano mkuu waliopanga kupiga kura za hapana kwa Rais Kikwete.

Mzee Makamba akitumia vitabu vya dini alimwelezea Kikwete kama mtu wa watu aliyeletwa na Mungu kuwaongoza wengine.

Hadi jana jioni majira ya saa moja kura za Mwenyekiti (Kikwete) na Makamu wake wawili (Mangula) na Dk. Ali Mohamed Shein, zilikuwa zinahesabiwa.

Chanzo: Tanzania Daima
 
Kurudi kwa Mangula CCM ni faraja kubwa kwa wana CCM. Huyu Mzee ni strategist mzuri. Walimtupa lakini baada ya maji kufika puani wameamua kumkumbuka. Mzee huyui ana hekima

Kinana naye ni mzuri kwa kutenda kimya kimya bila mayowe. Ukatibu Mkuu unamstahili kwa sasa labda tu umri unaweza kuwa unamtupa manake kwa siasa za sasa unahitaji kukaaa masaa mengi ukiwatumikia wanachama.

Nape ni mzuri lakini kwa Ukatibu Mkuu naona kama bado kidogo abaki hapo kwenye wenezi ili apambane na vijana wenzake majukwaani kwa kutoa matamko ya kisiasa. Ukatibu Mkuu hauhitaji kusema sana na kupambana majukwaani unatakiwa upambane kwa ku organize resources ndani ya Chama.
 
[h=5]Kinana Kutangazwa Kuwa Katibu Mkuu CCM Hii Leo...

CCM wamemaliza Mkutano wao Mkuu jana usiku. Kuna kila dalili kuwa Abdulahaman Kinana atatangazwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM kuchukua nafasi ya Wilson Mukama.

Na kutokana na Mkutano wa CCM kuchukua saa nyingi za kazi na uwepo wa sura nyingi mpya za wajumbe wa NEC, yawezekanakabisa , Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete, kinyume na ilivyo kawaida, safari hii akahitaji muda zaidi kabla ya kufanya Uteuzi wa Wajumbe wa Sekreteriati ya CCM. Ikumbukwe, Mkutano Mkuu ujao wa CCM utafanyika mwaka 2015, mwaka wa Uchaguzi.
[/h]


 
Mbona hata Mangula naye alitangaza kustaafu siasa? Huyo sasa karudi kwa kura za woga (kishindo).
 
Mkuu PakaJimmy

Ndiyo maana tunaandaa vitambulisho vya taifa huko nyuma ilikuwa rahisi raia wa nchi nyingine kuishi Tanzania bila shida ya kufuatwa fuatwa.Umesahau uraia wa Kinana niwa makaratasi na hii ilikuwa sababu ya kukimbia ubunge wa Arusha wazawa wa nchi walishamchokonoa akakimbilia kujificha nyuma ya chama.

Mkuu, umesahau kuwa huyu keshashika nafasi nyeti tu, acha za chama, hadi za serikali kabisa!
Hii ni No-Man's-Land!
 
Last edited by a moderator:
Wakimwingiza Kinana ukatibu mkuu, watuhumiwa wa ufisadi watakuwa na hali mbaya sana katika chama. Na kwaujumla wake wanaoitwa wanamtandao watakuwa wamebanwa mbavu sana. Hapa chama kitarudisha hadhi yake na mimi kama mwanaCDM, naona tutakuwa tumebanwa kiaiana.
Na hawa wawili wanafahamiana vizuri sana toka enzi za Nyerere. Watatoka na mgombea ambaye watawalazimisha Lowasa na Membe kumpigia kampeni.
 
Back
Top Bottom