WanaJF tumesikia habari mbalimbali ambazo zilionesha njama za kifisadi za CCM dhidi ya mali za umma au/na dhidi ya vyama vya upinzani, mfano wa Salma na Ridhiwani-matumizi mabaya ya fedha ya umma-ndege ya serikali.
Mara nyingi tuhuma hizi alipoambiwa meneja wa kampeni ya CCM Abdulrahaman Kinana aling'aka na hata kulazimika kufoji risiti-jambo ambalo litamgharimu siku si nyingi uchunguzi ukikamilika.
Nashawishika kusema kuwa Kinana anakiri kwamba tuhuma zote dhidi ya CCM sio 'good news' kwa watanzania.
Kwa hakika ufasadi wa mali za umma kama wa familia ya JK, mafisadi wengine wa CCM hauwezi kuwa 'good news' kwa watanzania. Pia Mhariri wa gazeti la 'ccm' kuitangazia nchi rais wa awamu ya tano kabla wananchi hawajapiga kura sio 'good news' kwa watanzania. Kwa Ujumla hizo ni mbinu za mafisadi ambao kiongozi wao kwa sasa ni Kinana anayehakikisha mbinu zao hizo zinafanikiwa.
Soma sehemu ya habari hii toka gazeti la mwananchi, 24/09/2010.
Meneja kampeni wa CCM, Abdulrahman Kinana jana alikataa kuzungumnzia tuhuma zilizoelekezwa kwa chama hicho akieleza kuwa gazeti hili, halitendi haki kwa CCM.
"Lakini ninyi (Mwananchi) you never have good news for CCM (hamna habari njema kwa CCM) kila siku mkipiga simu ni habari mbaya, mnaandika habari mbaya tu za CCM, nzuri hamzioni," alihoji.
"Mara Mama Salma kafanya hivi, mara Ridhwani kafanya vile, why can't you be carrier of good news? Always you carry bad news? (wakati wote ni mabaya tu, hamwezi kuandika mema ya CCM?
"Tafadhali waulizeni Daily News suala hilo."
Mara nyingi tuhuma hizi alipoambiwa meneja wa kampeni ya CCM Abdulrahaman Kinana aling'aka na hata kulazimika kufoji risiti-jambo ambalo litamgharimu siku si nyingi uchunguzi ukikamilika.
Nashawishika kusema kuwa Kinana anakiri kwamba tuhuma zote dhidi ya CCM sio 'good news' kwa watanzania.
Kwa hakika ufasadi wa mali za umma kama wa familia ya JK, mafisadi wengine wa CCM hauwezi kuwa 'good news' kwa watanzania. Pia Mhariri wa gazeti la 'ccm' kuitangazia nchi rais wa awamu ya tano kabla wananchi hawajapiga kura sio 'good news' kwa watanzania. Kwa Ujumla hizo ni mbinu za mafisadi ambao kiongozi wao kwa sasa ni Kinana anayehakikisha mbinu zao hizo zinafanikiwa.
Soma sehemu ya habari hii toka gazeti la mwananchi, 24/09/2010.
Meneja kampeni wa CCM, Abdulrahman Kinana jana alikataa kuzungumnzia tuhuma zilizoelekezwa kwa chama hicho akieleza kuwa gazeti hili, halitendi haki kwa CCM.
"Lakini ninyi (Mwananchi) you never have good news for CCM (hamna habari njema kwa CCM) kila siku mkipiga simu ni habari mbaya, mnaandika habari mbaya tu za CCM, nzuri hamzioni," alihoji.
"Mara Mama Salma kafanya hivi, mara Ridhwani kafanya vile, why can't you be carrier of good news? Always you carry bad news? (wakati wote ni mabaya tu, hamwezi kuandika mema ya CCM?
"Tafadhali waulizeni Daily News suala hilo."