Oxlade-Chamberlain
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 8,635
- 2,198
Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, amesema hoja yake ya kulitaka Bunge liunde kamati teule ya kuchunguza wizi wa nyara za serikali anaivutia pumzi akisubiri majibu ya uchunguzi unaofanywa na polisi wa kimataifa Interpol.
Hata hivyo, alisema amefurahishwa na majibu yaliyotolewa Jumamosi iliyopita bungeni na Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga, juu ya ukweli wa sakata la wizi na utoroshaji nje wa nyara za serikali.
Waziri alivyokiri juzi kwenye majibu yake amenisaidia sana. Mimi kufuatilia Interpol inatoa majibu gani Kila mara sisi wabunge tutakuwa tunafuatilia, alisema Kilango.
Kilango alisema hayo katika mahojiano maalum na gazeti hili nyumbani kwake mjini hapa jana akiwa kwenye mapumziko ya muda mfupi baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo mwishoni mwa wiki katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Kilango ambaye juzi alifanyiwa upasuaji mdogo hospitalini hapo na kuruhusiwa jana asubuhi, alisema baada ya kutoa mchango wake na nia yake ya kuwasilisha hoja binafsi, alichotaka kusikia ni majibu ya Waziri Mwangunga kwa kuwa suala hilo alilifanyia utafiti na alikuwa na majibu yote.
Nilikuwa nataka aseme ukweli na kweli alijibu vile nilivyotaka Ndio maana baada ya majibu yale mimi nilitoka kwa kuwa nilikuwa na 'appointment (ahadi ) hospitali ya kufanyiwa upasuaji, alisema.
Kilango alisema hakuwa na nia ya kuwasilisha hoja hiyo, lakini alichotaka kusikia kwenye hotuba ya wiziri ni juu ya wizi wa nyara hizo.
Alisema suala hilo ni kubwa na wabunge wataendelea kulifanyia kazi kwa kuwa majibu yake yamesaidia wao kufuatilia suala hilo na kupata ukweli.
Nilitaka aseme kwenye wizara yake tunaibiwa kiasi gani, lakini yeye hakuzungumzia suala hilo, alisisitiza mbunge huyo machachari, ambaye amekuwa akitoa mchango mkubwa wakati wa kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu ufisadi.
Alisema wabunge wanachopigania ni rasilimali za taifa zisiende mikononi mwa watu wachache. Hatukwenda bungeni kuvaa magauni, tumekwenda kutetea wananchi wetu, alisema wakati wa mahojiano hayo.
Kilango alisema wabunge ndio wanaopaswa kumsaidia rais ili nchi iweze kuwa na utawala bora.
Kitu kinachonikera ni kwamba hata Rais Barrack Obama (wa Marekani) juzi, alisema nyinyi Waafrika umaskini mnajitakia wenyewe kwani mna rasilimali za kutosha, alisema Kilango.
Hata hivyo, Kilango alitoa tahadhari kuwa wabunge wanapohoji juu ya hoja mbalimbali bungeni, hawamhoji mtu (akimaanisha waziri ) bali wanahoji taasisi ya waziri. Alisema kuna kauli zinazotolewa na baadhi ya wabunge kuwa ni mbaya zinazoweza kuhatarisha amani.
Kilango alisema katika baadhi ya kauli hizo ni pale baadhi ya wabunge wanaposema mawaziri Waislamu wanabanwa na wabunge Wakristo.
Kauli hii isisikike tena, kama kuna watu wenye kauli hiyo waache mara moja, alisema mbunge huyo, ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akijiadili hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii bungeni wiki iliyopita, Kilango, alitaja makontena ya nyara za serikali yaliyokamatwa nchini Vietnam na Ufilipino, na kumtaka Waziri aseme yalipitaje bandari ya Dar es Salaam na nani walihusika.
Waziri Mwangunga alithibitisha kukamatwa kwa makontena hayo na watu wanaoshikiliwa kwa utoroshaji huo wa nyara kupitia bandari ya Dar es Salaam.
Hii ni mara ya pili katika kipindi cha mwaka huu Waziri Mwangunga kuwa katika kikaango baada ya kubanikwa tena Aprili mwaka huu juu ya ada za vitalu vya uwindaji wa kitalii, ambavyo vilipandishwa kwa azimio la Bunge, lakini wizara yake ikalipuunza Bunge na kuvishusha.
Kikaango hicho kilitokana na hoja binafsi ya Mbunge wa Kwela (CCM), Chrisant Mzindakaya, aliyetaka kujua sababu za waziri huyo kupuuza azimio la Bunge na kutaka akemewe. Hata hivyo, baada ya maombi ya Mwangunga na kujieleza kwa kirefu, Mzindakaya aliiondoa hoja yake na kusisitiza kwamba watendaji serikalini wasaidie mawaziri si kuwakomoa.
Hata hivyo, alisema amefurahishwa na majibu yaliyotolewa Jumamosi iliyopita bungeni na Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga, juu ya ukweli wa sakata la wizi na utoroshaji nje wa nyara za serikali.
Waziri alivyokiri juzi kwenye majibu yake amenisaidia sana. Mimi kufuatilia Interpol inatoa majibu gani Kila mara sisi wabunge tutakuwa tunafuatilia, alisema Kilango.
Kilango alisema hayo katika mahojiano maalum na gazeti hili nyumbani kwake mjini hapa jana akiwa kwenye mapumziko ya muda mfupi baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo mwishoni mwa wiki katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Kilango ambaye juzi alifanyiwa upasuaji mdogo hospitalini hapo na kuruhusiwa jana asubuhi, alisema baada ya kutoa mchango wake na nia yake ya kuwasilisha hoja binafsi, alichotaka kusikia ni majibu ya Waziri Mwangunga kwa kuwa suala hilo alilifanyia utafiti na alikuwa na majibu yote.
Nilikuwa nataka aseme ukweli na kweli alijibu vile nilivyotaka Ndio maana baada ya majibu yale mimi nilitoka kwa kuwa nilikuwa na 'appointment (ahadi ) hospitali ya kufanyiwa upasuaji, alisema.
Kilango alisema hakuwa na nia ya kuwasilisha hoja hiyo, lakini alichotaka kusikia kwenye hotuba ya wiziri ni juu ya wizi wa nyara hizo.
Alisema suala hilo ni kubwa na wabunge wataendelea kulifanyia kazi kwa kuwa majibu yake yamesaidia wao kufuatilia suala hilo na kupata ukweli.
Nilitaka aseme kwenye wizara yake tunaibiwa kiasi gani, lakini yeye hakuzungumzia suala hilo, alisisitiza mbunge huyo machachari, ambaye amekuwa akitoa mchango mkubwa wakati wa kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu ufisadi.
Alisema wabunge wanachopigania ni rasilimali za taifa zisiende mikononi mwa watu wachache. Hatukwenda bungeni kuvaa magauni, tumekwenda kutetea wananchi wetu, alisema wakati wa mahojiano hayo.
Kilango alisema wabunge ndio wanaopaswa kumsaidia rais ili nchi iweze kuwa na utawala bora.
Kitu kinachonikera ni kwamba hata Rais Barrack Obama (wa Marekani) juzi, alisema nyinyi Waafrika umaskini mnajitakia wenyewe kwani mna rasilimali za kutosha, alisema Kilango.
Hata hivyo, Kilango alitoa tahadhari kuwa wabunge wanapohoji juu ya hoja mbalimbali bungeni, hawamhoji mtu (akimaanisha waziri ) bali wanahoji taasisi ya waziri. Alisema kuna kauli zinazotolewa na baadhi ya wabunge kuwa ni mbaya zinazoweza kuhatarisha amani.
Kilango alisema katika baadhi ya kauli hizo ni pale baadhi ya wabunge wanaposema mawaziri Waislamu wanabanwa na wabunge Wakristo.
Kauli hii isisikike tena, kama kuna watu wenye kauli hiyo waache mara moja, alisema mbunge huyo, ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akijiadili hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii bungeni wiki iliyopita, Kilango, alitaja makontena ya nyara za serikali yaliyokamatwa nchini Vietnam na Ufilipino, na kumtaka Waziri aseme yalipitaje bandari ya Dar es Salaam na nani walihusika.
Waziri Mwangunga alithibitisha kukamatwa kwa makontena hayo na watu wanaoshikiliwa kwa utoroshaji huo wa nyara kupitia bandari ya Dar es Salaam.
Hii ni mara ya pili katika kipindi cha mwaka huu Waziri Mwangunga kuwa katika kikaango baada ya kubanikwa tena Aprili mwaka huu juu ya ada za vitalu vya uwindaji wa kitalii, ambavyo vilipandishwa kwa azimio la Bunge, lakini wizara yake ikalipuunza Bunge na kuvishusha.
Kikaango hicho kilitokana na hoja binafsi ya Mbunge wa Kwela (CCM), Chrisant Mzindakaya, aliyetaka kujua sababu za waziri huyo kupuuza azimio la Bunge na kutaka akemewe. Hata hivyo, baada ya maombi ya Mwangunga na kujieleza kwa kirefu, Mzindakaya aliiondoa hoja yake na kusisitiza kwamba watendaji serikalini wasaidie mawaziri si kuwakomoa.