Tuna nchi nzuri yenye fursa nyingi iliyogeuzwa kuwa mali binafsi ya wachache wenye kufahanika kwa kutokushiba kwao.
Maisha yamekuwa magumu. Mzigo wa kodi na tozo umekuwa usiomithilika. Wakati serikali yenyewe ikiwa imelenga makusanyo tu, bila kujali kuvuja kwa mifuko yake wala kama wananchi wake wanamudu hata zile gharama msingi tu za maisha. Ni gharama za vyakula, elimu, afya nk? Ni umaskini? Hayo siyo kipaumbele cha serikali tena.
Fika kwenye mahospitali kuona pesa za NHIF zinavyopigwa. Gharama za tiba zilivyowekwa kuwa za juu pasipo kuwa na uhalisia wowote.
Ona wizi wa dawa unavyoendelea. Tambua kumbe maduka karibu yote ya ndani au kuzizunguka hospitali hizi ni mali binafsi za vigogo hawa hawa. Ona wananchi wa kawaida kupata huduma ilivyogeuka kuwa ni kwa kudra za mwenyezi Mungu. Ona rushwa ilivyotamalaki, kujuana, kubambikiziana gharama za tiba nk kulivyoota mizizi.
Kwani hata ni sekta ipi basi imenusurika kutoka kwenye mlolongo huu wa kero za rushwa kubambikiziana mambo malengo yakiwa kukusanya mapato haramu au halali kupitia faini au taratibu na sheria za kijanja janja zinazozaliwa kila siku? Ni polisi, takukuru, uhamiaji, TRA, LATRA, Tanroads, Tanesco, mahakamani nk.
Kumbe kwa watendaji wa serikali, wananchi hawana chao. Rasmi na bila aibu watendaji wamewageuza mradi wao. Kodi wanazokamuliwa zinakwenda kuwaneemesha wachache. Haya yakiendelea wao wakitucheza shere kuwa hazina iko mikono salama.
Kwamba hapa chini ni pesa anazoona CAG kuwa tumepigwa?
1. Wizara ya Afya - Tsh. Bilioni 91
2. Wizara ya Elimu - Tsh. ilioni 33.5
3. Wizara ya Maji - Tsh. Bilioni 82.8
4. Wizara ya Maliasili na Utalii - Tsh. Bilioni 1.2
5. Hifadhi ya Jamii (TASAF) - Tsh. Bilioni 1.5
6. Wizara ya Maendeleo ya Jamii - Tsh. Milioni 141.
7. Bado bungeni kuliko na wabunge hewa.
8. Bado TAMISEMI kwenye halmashauri huko.
9. Bado madhirika ya umma.
10. Nk.
Hii haikubaliki.
Kuwaita wezi hawa stupid au kuwataka wote waliohusika kuachia ngazi wenyewe tu, haitoshi. Hawa ni wa kufurusha unceremoniously watake wasitake. Hawa ni WA kutiwa adabu na kulazimishwa kurejesha pesa zote walizofuja. Hawa makazi yao ya kudumu yanapaswa kuwa magereza siyo katika ofisi za umma kazi wizi wao ukiendelea.
Kwamba watupishe? Hawa wasiokiwa na mishipa ya aibu? Nani kasema? Ni wazi kuwa hawataondoka wenyewe eti kwa kutuonea huruma tu.
Serikali siyo mali ya mtu binafsi. Ni vyema mkuu wake akajitenga na wabadhirifu hawa wanaofahamika kwa majina. Akawachukulia hatua stahiki zenye kuonekana na bila ya kuwaangaliana usoni. Wenye nchi tunaangalia na hatutakaa kimya na hasa kama hatua za kuridhisha hazitachukuliwa kama ilivyozoeleka.
Waisijaribu kutu beep. Wanatoka wezi hawa sasa. La sivyo matumizi yetu ya nguvu ya umma yatakuwa ni haki yetu na kwa namna tutakavyoona inafaa.
Hili halina vyama, ni la wananchi na haliwezi kuwa na mswalia mtume.
Maisha yamekuwa magumu. Mzigo wa kodi na tozo umekuwa usiomithilika. Wakati serikali yenyewe ikiwa imelenga makusanyo tu, bila kujali kuvuja kwa mifuko yake wala kama wananchi wake wanamudu hata zile gharama msingi tu za maisha. Ni gharama za vyakula, elimu, afya nk? Ni umaskini? Hayo siyo kipaumbele cha serikali tena.
Fika kwenye mahospitali kuona pesa za NHIF zinavyopigwa. Gharama za tiba zilivyowekwa kuwa za juu pasipo kuwa na uhalisia wowote.
Ona wizi wa dawa unavyoendelea. Tambua kumbe maduka karibu yote ya ndani au kuzizunguka hospitali hizi ni mali binafsi za vigogo hawa hawa. Ona wananchi wa kawaida kupata huduma ilivyogeuka kuwa ni kwa kudra za mwenyezi Mungu. Ona rushwa ilivyotamalaki, kujuana, kubambikiziana gharama za tiba nk kulivyoota mizizi.
Kwani hata ni sekta ipi basi imenusurika kutoka kwenye mlolongo huu wa kero za rushwa kubambikiziana mambo malengo yakiwa kukusanya mapato haramu au halali kupitia faini au taratibu na sheria za kijanja janja zinazozaliwa kila siku? Ni polisi, takukuru, uhamiaji, TRA, LATRA, Tanroads, Tanesco, mahakamani nk.
Kumbe kwa watendaji wa serikali, wananchi hawana chao. Rasmi na bila aibu watendaji wamewageuza mradi wao. Kodi wanazokamuliwa zinakwenda kuwaneemesha wachache. Haya yakiendelea wao wakitucheza shere kuwa hazina iko mikono salama.
Kwamba hapa chini ni pesa anazoona CAG kuwa tumepigwa?
1. Wizara ya Afya - Tsh. Bilioni 91
2. Wizara ya Elimu - Tsh. ilioni 33.5
3. Wizara ya Maji - Tsh. Bilioni 82.8
4. Wizara ya Maliasili na Utalii - Tsh. Bilioni 1.2
5. Hifadhi ya Jamii (TASAF) - Tsh. Bilioni 1.5
6. Wizara ya Maendeleo ya Jamii - Tsh. Milioni 141.
7. Bado bungeni kuliko na wabunge hewa.
8. Bado TAMISEMI kwenye halmashauri huko.
9. Bado madhirika ya umma.
10. Nk.
Hii haikubaliki.
Kuwaita wezi hawa stupid au kuwataka wote waliohusika kuachia ngazi wenyewe tu, haitoshi. Hawa ni wa kufurusha unceremoniously watake wasitake. Hawa ni WA kutiwa adabu na kulazimishwa kurejesha pesa zote walizofuja. Hawa makazi yao ya kudumu yanapaswa kuwa magereza siyo katika ofisi za umma kazi wizi wao ukiendelea.
Kwamba watupishe? Hawa wasiokiwa na mishipa ya aibu? Nani kasema? Ni wazi kuwa hawataondoka wenyewe eti kwa kutuonea huruma tu.
Serikali siyo mali ya mtu binafsi. Ni vyema mkuu wake akajitenga na wabadhirifu hawa wanaofahamika kwa majina. Akawachukulia hatua stahiki zenye kuonekana na bila ya kuwaangaliana usoni. Wenye nchi tunaangalia na hatutakaa kimya na hasa kama hatua za kuridhisha hazitachukuliwa kama ilivyozoeleka.
Waisijaribu kutu beep. Wanatoka wezi hawa sasa. La sivyo matumizi yetu ya nguvu ya umma yatakuwa ni haki yetu na kwa namna tutakavyoona inafaa.
Hili halina vyama, ni la wananchi na haliwezi kuwa na mswalia mtume.