Nilipita ktk bank moja mjini Dar na nimemwona graduate wa SUA akitoa huduma kinyume na masomo yake ya kilimo. Mheshimiwa Rais naomba kwa huruma yako uniuzie mimi lile shamba la mifugo la Kitulo Makete ili niweze kuutumia ujuzi wangu wa mifugo pale. Ukinipa shamba lile, naamini mimi na vijana wenzangu tutafanya yafuatayo. Moja, ni lazima tutajenga kiwanda cha kusindika maziwa pale, vijana wa SUA watapata ajira palem vijana wa food science watapata cha kufanya pale kiwandani kwetu. Shamba lile lina umeme wa grid na ng`ombe wachache wapo.
Mheshimiwa Rais, ukitupa sisi vijana wako dhamana hii hatutakuangusha, najua mimi na wenzangu hatuwezi kupambana ktk njia za kisheria ili kulipata shamba hili kwa sababu ya kitu kidogo, lakini sisi ndio watalaamu wako, je unataka twende Botswana, hapana. Nimeona nikuombe badala ya kukaa kijiweni na kulalamika kana kwamba nimeomba nikanyimwa.Naamini kwa huruma yako utatusikiliza.
Mheshimiwa Rais, ukitupa sisi vijana wako dhamana hii hatutakuangusha, najua mimi na wenzangu hatuwezi kupambana ktk njia za kisheria ili kulipata shamba hili kwa sababu ya kitu kidogo, lakini sisi ndio watalaamu wako, je unataka twende Botswana, hapana. Nimeona nikuombe badala ya kukaa kijiweni na kulalamika kana kwamba nimeomba nikanyimwa.Naamini kwa huruma yako utatusikiliza.