Penye tija huyu bwana haoni, na kule pa kufuja kodi zetu wala hasahau.
Wakati mwingine namkumbuka sana Prof Chinua Achebe na mhusika wake Mkuu mojawapo, Mzee Unoka (Baba yake Jemadari Okonkwo) mfumo wa maisha yake, kupenda kwake kupiga Ugene na gambuzi kila siku katika mwaka na kutamani kila siku ipitayo iwe ni kama Krismasi kwa Wakristo au Idd El Hajj kwetu sie Waislamu.
Jamani huenda Prof Achebe alikua analipiga vijembe taifa letu kwenye kitabu chake cha 'Things Fall Apart' kwa kumchora Mzee Unoka na Mjukuu wake Nwoye jinsi alivyowachora na kumzidishia wino zaidi Jasiri Okonkwo na Obierika Mzee wa Busara?????????????
Simuelewi JK hata kidogo mwezi uliopita tu ametoka SA jamani anafuata nini mara hii tu?au ndio anasema yeye bingwa wa kuhemea??au ana fanya timing za UK PM?akaombe chenji??nimesikitika hadi sasa bado anaenda kutembea Robin Island kuna jipya gani hukoo??miaka yote asiende anaenda kipindi hiki nchi iko gizani yeye anaenda historical sites
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.