Desteo
JF-Expert Member
- Jul 27, 2011
- 494
- 123
Najua ewe rais wetu unashindwa kufanya maamuzi magumu kutokana na utata wa chaka lenyewe. Tunajua umeshika kiberiti ukitaka kulipua hilo chaka lililolowa wese kumbe na wewe umelowa wese. Ni rahisi. Kaa mbali kabisa kisha mpe mtoto wa mkulima hicho kiberiti. Hakika ukifanya hivyo na tukajua, hatia juu yako itapungua.
Watz ni wepesi wa kusamehe pindi wakifanyiwa wema. Hilo chaka lina epa, richmond, meremeta, uda, rada, shimbo (huyu ni taasisi kabisa), n.k. Unajua fika hili chaka linatugharimu kwa uwepo wake. Pinda yu tayari kufanya utakalomwagiza. Nadhani ulipata hansard ya lile tukio la jairo. Ulimsikia kwa maneno yake. Kikwazo kikubwa kilikuwa wewe.
Watz tumechoshwa na haya. Usione tuko kimya juu ya hii hali mbaya ya maisha. Nikwambie tu, watz wanakuchukia mpaka basi. Ila watakupenda mpaka basi ukiwapatia 'kichwa cha Yohana' Ni ngumu kweli ila ufanyeje? Fanya kujaribu tu.
Hutaamini. Chukua hela za hiyo 'taasisi' ukatujengee stiegler's gorge-ahadi ya enzi na enzi. Unayo miaka minne ya kujipoteza ama kujisimika mioyoni mwa watz. Ila pia ukumbuke na ahadi ya babu. Hatakufa hadi kieleweke.
You can prove him wrong by doing it right.
Watz ni wepesi wa kusamehe pindi wakifanyiwa wema. Hilo chaka lina epa, richmond, meremeta, uda, rada, shimbo (huyu ni taasisi kabisa), n.k. Unajua fika hili chaka linatugharimu kwa uwepo wake. Pinda yu tayari kufanya utakalomwagiza. Nadhani ulipata hansard ya lile tukio la jairo. Ulimsikia kwa maneno yake. Kikwazo kikubwa kilikuwa wewe.
Watz tumechoshwa na haya. Usione tuko kimya juu ya hii hali mbaya ya maisha. Nikwambie tu, watz wanakuchukia mpaka basi. Ila watakupenda mpaka basi ukiwapatia 'kichwa cha Yohana' Ni ngumu kweli ila ufanyeje? Fanya kujaribu tu.
Hutaamini. Chukua hela za hiyo 'taasisi' ukatujengee stiegler's gorge-ahadi ya enzi na enzi. Unayo miaka minne ya kujipoteza ama kujisimika mioyoni mwa watz. Ila pia ukumbuke na ahadi ya babu. Hatakufa hadi kieleweke.
You can prove him wrong by doing it right.