Kikwete bora kuliko Lipumba na Mbowe pamoja-UTAFITI

Hawa hawatambulikani isipokuwa na wafuasi wa Sultani CCM ,kwani tunaona kwenye kura za maoni katika Marekani kupitia tovuti mbalimbali ikiwemo live show au masuali ya papo kwa papo kwa wapita njia au kwenye migahawa ,hawa tulionao sisi ni wapiga debe wamafisadi ,yaani unasikia wamekurupuka tu ,wanahojiana wenyewe kwa wenyewe na kutoa data zinazowafurahisha ,hebu badilisheni Katiba halafu ndio mje na mauzauza ,hakuna mtakalolifanya kuisifu serikali au mfuasi yeyote yule wa Sultani CCM kama baadhi ya mambo hayajawekwa sawa,Katiba ya Nchi ,Mahakama za Nchi Tume ya Uchaguzi usawa katika kutumika kwa vyombo vya habari na jeshi la polisi.

Kama mnaamini Kikwete anapendwa kwa asilimia 62 (Kuwarahisishia walilonalo rohoni ,Serikali ya Sultani CCM inapendwa) wekeni uchaguzi huru na wa haki na wananchi na vyama vyote viridhike kuwa kuanzia uandikishaji mpaka uwasilishaji wa vifaa vya kupigia kura vinakuwa na kufika kwa wakati na vituo kufunguliwa kwa wakati na wananchi wanapiga kura bila ya masumbuko kutoka kwa polisi na wanamgambo.
Ni juzi tu masandanduku na makaratasi yameonekana yakitokea vichochoroni na wengine kukamatwa nayo ,halafu iwe vitendo hivyo vyote mnavyofifanya vya uchafuzi iwe ndio mna asilimia kubwa ,wacheni uwongo na kutumia vyombo vya habari kuwalaghai WaTanzania na kamati zenu uchwara ,wanaopendwa hawafichi wala hawafanyi uhalifu katika harakati za uchaguzi ,tume hatukuisikia kukoromea yaliotokea Mbeya ,hivi ndio kupendwa kwa Kikwete huko.
 
04_09_4heph6.jpg


Kampeni za 2010 hizo!
 
Steadman Group wako Kenya, Tanzania na Uganda na biashara kubwa wanayofanya ni kuandaaa ripoti kuhusu utazamaji wa televisheni yaani TV viewership. Pia huwa wanalipwa kufanya research kwa ajili ya kampuni kuhusu bidhaa zao etc. Ni kweli kwamba watu wengi wamekuwa wakiilalamikia Steadman na hata watu wa marketing wanaotumia data za Steadman wameona ya kuwa kuna walakini mkubwa. Kwa mfano kwa miaka mingi walikuwa wanaonyesha kuwa ITV ndiyo namba 1 kwa utazamaji nchini kati ya televisheni zote, lakini sasa TBC ndo inaongoza na kutazamwa zaidi ya ITV, na hakuna rationale behind, sampling zao huwa ni ndogo na haieleweki ni methodology gani wanatumia.
Pia some of their conclusions are based on appearances and not reality. Hata hii polling ya kisiasa watakuwa wako commissioned maana hawawezi kuwauzia upinzani hivihivi unlike TV viewership ambapo marketing departments zitanunua data zote kujua watumie vipi pesa zao. Na hawa Steadman mara nyingi hawafanyi kazi bila commission. Ni wazi kazi hii walipewa na CCM. kama siyo hawana budi kusema walifanya kwa malengo gani.
 
Nikiangalia hii sampling ndogo ya 2000 respondents na mkanganyiko wa parameters walokuwa wakizitafuta, I suppose we can safely label the whole thing as simply senseless, bogus and unscholarstic.

Mtindiowaubungo,

Kwenye statistics hiyo sample ni tosha kabisa. Kinachoangaliwa sio quantity bali quality ya sample husika. Muhimu hapo ni kwamba hiyo sample iwe ina represent makundi yote ya jamii ya Tanzania kwa uwiano ule kwa mfano ambao ulipatikana kwenye uchaguzi wa 2005.

Labda useme hukubaliani na quality ya sample yao maana garbage in garbage out. Kama wameenda kuwahoji wana CCM tu, ni wazi matokeo nayo yatakuwa fake.

Kwa mfano kwenye li nchi likubwa kama USA, ukiangalia opinion polls zao utakuta ni kati ya watu 1000 na 5000.

Mimi naona kama hiyo asilimia 62 kwa JK ni kitu cha kukitegemea kabisa kwa TZ. Kwa kuangalia hizi findings zao, ningelikuwa mpinzani ningelikuwa positive sana maana kushuka kwa umaarufu wa JK kunaongozana na kushuka kwa umaarufu wa CCM. Sasa kama CCM sio maarufu na JK sio maarufu hapo ni double whammy. Huenda hawa jamaa wangechunguza na umaarufu wa vyama basi CCM ingelikuwa chini ya asilimia 50.

Upinzani unganeni na mna nafasi kubwa ya kuishinda au kuikaribia sana CCM kwenye ubunge. Nafasi kwenye urais naona ni ndogo labda mambo yabadilike kati ya sasa na mwaka kesho.
 
Zitatafutwa justification ilimradi tu asionekane kashida kwa zengwe 2010. Anatuyeyusha tu akae pembeni watu warekebishe nchi yeye hii sio fani
 
inategemea watu hao wanamjudge JK kwa kutumia kigezo gani. Kama wanatumia kigezo cha uongozi ni wazi kuwa matokeo yao ni ya uongo. Hakuna asiyejua kuwa JK ameshindwa kuongoza Chama na ameshindwa kuprovide leadership kwenye serikali. Kama kinachozungumziwa ni u-handsome nadhani JK ni most handsome of them all, kama ni competence nadhani ni vice versa.
Mjumbe mmoja ameuliza swali zuri kabisa, ni nani waliwalipa watafiti na walifanya utafiti kwa lengo gani. Au ndio vision 2010??
 
Ubora wa mtu hauji kwa sababu yeye ni zaidi ya wengine, ila tu kwa sababu amefanya zaidi ya mategemeo yake na jamii inayomzunguka.
hivyo nahisi JK atleast amefanya zaidi ya uwezo wake waki Lipumba na Mbowe wameendelea kubaki na kufanya yale tu tuliyoyategemea. hawajafanya ile 'extra'
Na tukumbuke extra ya JK inaweza ikawa sio extra kwa mtu mwingine, lakini kwa kuwa JK amweifikia hiyo extra basi si jambo la kushangaza kutangazwa bora zaidi ya wengine.
 
Hawa mafisadi wameanza tena vijikampeni mshenzi kama yule Mkandala alivyofanya 2005 na REDET yake kumbe alikuwa anajitafutia ujiko tu.
Hakuna umaarufu wowote. Watanzania wengi wako hoi na hawamuhitaji tena huyu kibaka wa kisiasa.
 
Jamani eeeh... kama alivyosema Mtanzania, tushukuru hizo polls zimeshuka kwa kiwango hicho...Siku zote tujiandae kwa habari mbaya kuliko njema na polls kama hizi ziwe kiamsho kwa wananchi kwamba vita yetu bado kabisa haijafikia ushindi..
Binafsi sipendi kabisa CCM irudi jukwaani lakini nafahamu fika Kikwete bado ana mvuto mkubwa sana kwa baadhi ya watu tofauti na wengi tunavyofikiria...Hiyo asilimia 62 imenipa moyo sana kwa sababu naamini kabisa kuwa wabunge wengi wa CCM walipita kutokana na nguvu ya Kikwete akiwa ndani ya Mtandao..NBa polls siku zote hupigwa toka mitaani na kwa idadi ndogo sana na watu.. Still, kati ya kila watu 10 haiwezekani wote mkafikiria sawa..
Sasa kama wananchi wameanza kuunganisha vitu hivi viwili tena wakati huu mbaya wa uchumi duniani nina hakika by 2010 rating ya Kikwete itakuwa chini zaidi..
Nina hakika wananchi hawataafiki sababu zozote zinazohusiana na hali ya Uchumi duniani kuwa ndio sababu bali Kikwete mwenyewe..Na laukama wapinzani wakijipanga na list ndogo tu ya Mbowe, Dr. Slaa, Lipumba na Mtu mwingine maarufu toka Zanzibar..Basi ushindi umepatikana..Kikwete can't stand alone kitaifa anaweza kushinda ndani ya CCM lakini Kitaifa itategemea na wapinzani wamejipanga vipi..
It's gonna be the Only time ya kula Turkey! -Thanksgiving day..
 
Watanzania tujifunze kukubali kusikia tusiyoyapenda. Kukimbilia kushutumu taarifa yeyote isiyoendana na fikira na mitazamo yetu bila hata kujua undani wa zoezi zima la utafiti lilivyofanyika ni kufilisika kimawazo. Watanzania ni karibia milioni 40 na wanaowakilisha kada yetu tunaotumia mitandao hawafiki milioni moja. Sasa iweje sisi wachache hivyo tukawa tunajua mitizamo ya watanzania wenzetu walio wengi ambao inawezekana kabisa wakawa wanaangalia hayo tunayoyaona ni mapungufu ya JK kwa mtazamo mwengine kabisa. Ukiachilia mbali wengi wetu tanzania tunaijuwa kutoka katika mitandao na magazeti yaliyopoteza dira ya ujenzi na kuchukua mwelekeo wa kubomoa.

Kwangu mimi utafiti huu ni muhimu kwa WAPINZANI kuuchukulia kwa umakini wa hali ya juu. Kimoja ninachokiona ni kuwa UPINZANI una tatizo la uongozi wa kitaifa. Hili ni suala nyeti sana kulishughulikia kabla ya uchaguzi wa 2010 kama kweli tunapenda kuona UPINZANI unaongeza nguvu zake katika vyombo vya maamuzi nchini kama BUNGENI na pengine URAIS.

Kumbukeni wengin tulikimbilia kubeza utafiti wa REDET kabla ya uchaguzi wa 2005 kama ilivyo sasa na kuacha kuufanyia kazi kama changamoto. Matokeo ya uchaguzi mkuu yalipokuja hayakuwa na tofauti na matokea ya utafiti wa REDET kwa uponde wa urais na ubunge pia.
 
Jamani eeeh... kama alivyosema Mtanzania, tushukuru hizo polls zimeshuka kwa kiwango hicho...Siku zote tujiandae kwa habari mbaya kuliko njema na polls kama hizi ziwe kiamsho kwa wananchi kwamba vita yetu bado kabisa haijafikia ushindi..
Binafsi sipendi kabisa CCM irudi jukwaani lakini nafahamu fika Kikwete bado ana mvuto mkubwa sana kwa baadhi ya watu tofauti na wengi tunavyofikiria...Hiyo asilimia 62 imenipa moyo sana kwa sababu naamini kabisa kuwa wabunge wengi wa CCM walipita kutokana na nguvu ya Kikwete akiwa ndani ya Mtandao..NBa polls siku zote hupigwa toka mitaani na kwa idadi ndogo sana na watu.. Still, kati ya kila watu 10 haiwezekani wote mkafikiria sawa..
Sasa kama wananchi wameanza kuunganisha vitu hivi viwili tena wakati huu mbaya wa uchumi duniani nina hakika by 2010 rating ya Kikwete itakuwa chini zaidi..
Nina hakika wananchi hawataafiki sababu zozote zinazohusiana na hali ya Uchumi duniani kuwa ndio sababu bali Kikwete mwenyewe..Na laukama wapinzani wakijipanga na list ndogo tu ya Mbowe, Dr. Slaa, Lipumba na Mtu mwingine maarufu toka Zanzibar..Basi ushindi umepatikana..Kikwete can't stand alone kitaifa anaweza kushinda ndani ya CCM lakini Kitaifa itategemea na wapinzani wamejipanga vipi..
It's gonna be the Only time ya kula Turkey! -Thanksgiving day..[/QUOTEa]

Mkuu,
well said but only if wishes were horses everyone would ride one. Hata wewe leo hii ukiweza kupata pesa ya ufisadi ukawahonga NEC na CC ya sisiwehu utaukwaa urahisi bila hata kutumia sera kwenye kampeni bali ahadi kibao kama vile watu walale tu bila kufanya kazi na watapata maisha bora kwa kila mdanganyika. Uelewa wapiga kura ni karibu na hakuna.
Kuna wakati nilienda kwa babu yangu huko Sengerema nikakuta mzee mmoja pale kijijini ambaye kwa pale anaonekana ndio muelewa yuko kwenye foleni anasubiri mahindi ya mgao(msaada). Kukatokea ubishi wa kisiasa kuhusu rafu alizofanyiwa Masha na William Shija. Yule mzee mjuaji akaanza kuwasifia FFU kwa kumpiga Masha wakati inajulikana wazi kuwa masanduku yaliyokuwa yaamue hatima ya shija yalitoweka na hayakujumuishwa. Kwa baraka za msimamizi (mkurugenzi wa halmshauri) matokeo yakatangazwa Shija kashinda. Na hayo ni masanduku ya hapo Sengerema mjini ambapo shija alikuwa hatakiwi. Kwa ujumla Hata kama wapinzania wote wakiungana haki haiko upande wao. Wakazanie tu wabunge sehemu wanazokubalika.
 
Watanzania tujifunze kukubali kusikia tusiyoyapenda. Kukimbilia kushutumu taarifa yeyote isiyoendana na fikira na mitazamo yetu bila hata kujua undani wa zoezi zima la utafiti lilivyofanyika ni kufilisika kimawazo. Watanzania ni karibia milioni 40 na wanaowakilisha kada yetu tunaotumia mitandao hawafiki milioni moja. Sasa iweje sisi wachache hivyo tukawa tunajua mitizamo ya watanzania wenzetu walio wengi ambao inawezekana kabisa wakawa wanaangalia hayo tunayoyaona ni mapungufu ya JK kwa mtazamo mwengine kabisa.
Hapa inawezekana uko sahihi kwa kiasi fulani. Kumbuka tu kuwa karibu wote wanochangia hoja hii wamefanya huo utafiti ama kama principal researchers au research assistants. Na ukweli nikuwa dodoso hizo hujaziwa kwenye vyumba vya guest house za bei rahisi kama umeshawahi kufanya utelewa nini nasema. Watu huenda kule kupata ile posho na ili kuikoa hujaza dodoso kwa kujihoji wenyewe na kutoa majibu kadri ya mtizamo wao[/QUOTE]Ukiachilia mbali wengi wetu tanzania tunaijuwa kutoka katika mitandao na magazeti yaliyopoteza dira ya ujenzi na kuchukua mwelekeo wa kubomoa.[/QUOTE]
hapa siyo kweli labda ujisemee wewe lakini wengi wetu tunayajua maisha ya mtanzania mlalahoi
Kwangu mimi utafiti huu ni muhimu kwa WAPINZANI kuuchukulia kwa umakini wa hali ya juu. [/QUOTE]Kimoja ninachokiona ni kuwa UPINZANI una tatizo la uongozi wa kitaifa.[/QUOTE] Hii nayo ni propaganda ya kiaina japo ni kweli kuna vyama kama TLP, DP, UDP na NCCR kuvitaja vichache [/QUOTE] Hili ni suala nyeti sana kulishughulikia kabla ya uchaguzi wa 2010 kama kweli tunapenda kuona UPINZANI unaongeza nguvu zake katika vyombo vya maamuzi nchini kama BUNGENI na pengine URAIS.
Hapa tuko pamoja kasoro hiyo sentensi niliyo ihighlight

Kumbukeni wengin tulikimbilia kubeza utafiti wa REDET kabla ya uchaguzi wa 2005 kama ilivyo sasa na kuacha kuufanyia kazi kama changamoto. Matokeo ya uchaguzi mkuu yalipokuja hayakuwa na tofauti na matokea ya utafiti wa REDET kwa uponde wa urais na ubunge pia.
hii nayo haijatulia kwani sababu ni nilizokupa huko juu. Kwamba yalitokea ambayo REDET walisema haimaanishi tumekubali utafiti wao ulikuwa wa kisayansi. Ni kama sheikh Yahya kutabiri halafu ikawa hivyo huwezi kutuambia alisema tukubali tu alikuwa anaelewa. REDET walisoma upepo na hivyo wakapiaka takwimu na matokeo yake si ndiyo hayo Mkandala ni VC na anaua chuo kikuu
 
Cpt Hadock,
Maneno yako kweli tupu lakini hayo ya Masha ni Sengerema...sidhani kaa kulikuwa namaandalizi ya kutosha dhidi ya hali halisi iliyojitokeza toka mwanzo..
Kinachofanyika hapa mkuu wangu ni kusoma hizo alama za nyakati.. Somo hapa ni kukubali matokeo ya polls hizi kisha mnajipanga kikamilifu kama wenzetu Kenya, Zimbabwe na mwingineko ambako mmomonyoko wa chama tawala ulianza ndani, wakabezana nani mbora kuliko mwingine.. wengine wakajikata kisha rais akabakia pekee au na washabiki wachache sana..Amini maneno yangu nguvu ya CCM ni Kikwete leo hii na akiporomoka aidha iwe kwa mkono wa CCM au Ufisadi, ushindi wetu..
Sioni kabisa Watanzania kujipanga nyuma ya kiongozi yeyote zaidi ya Kikwete na bahati mbaya ni kwamba hakuna mtu wa kuweza kupendekeza jina jingine Watanzania wakamkubali kama alivyofanya Nyerere wakati wa Mwinyi na Mkapa...
Na kama kweli polls zimeshuka kiasi cha kufikia asilimia 62 kwa nchi kama Tanzania ambayo wajinga tupo wengi basi kuna kila dalili tumeanza kuuona mwanga..
Hayo ya wizi wa masanduku hauwezi kushinda itakapo fikia kuna wasimamiszi wa Kimataifa na najua CCM watataka sifa ya kuonyesha demokrasia, Ukiweka na Mafisadi pembeni, haa! ndio jogoo la tatu litawika babu..
 
Mkandara i like your objectivity! Tatizo la wengi hapa ni kwamba wanataka kusikia wanayotaka kusiki tu. Ukweli ni kwamba Kikwete pekee ndio CCM kwa sasa! Mungu apishie mbali lakini JK akitoweka ghafla CCM itasambaratika vibaya sana. Hakuna comon ground inayowaunganisha viongozi wa CCM. Kuna makundi zaidi ya 10 kwa sasa. Kina Mkapa, Kina Lowassa, kina Makamba, Kina Mwakyembe, Kuna Kingunge, kina Warioba, Kina Butiku, kina Malecela, kuna wale wasiojua kinachoiendelea kama kina Chitalilo, and the list goes on!

CCM kama institution iko katika transitional period. Itategemea insight ya Kikwete sasa. Either inaweza kuzama au kuibuka na kuwa even more powerful. Ni jukumu la wapinzani ku-take advantage ya situation iliyopo sasa, right now. Wakisubiri wataachwa kwenye mataa!
 
Mkandara ndugu yangu (nikiamini wewe siyo kama jamaa zetu waotaka kuitwa waheshimiwa),
Hayo ya polls mimi siamini kabisa kwa sababu nafahamu kwa uhakika jinsi takwimu zinavyopikwa. Mimi nikiwa opposition believer halafu najaza hizo hojaji (ndio najaza) kwa sababu siwezi kutumia masaa kumi kwenda kijiji cha mbali kwani mnaposample sio watu wote kwenye wilaya moja watakuwa wa kijiji kimoja, ukiniuliza kuhusu JK nitajaza kwa kupondea sana na wewe ukiwa muumini mzuri wa CCM (sisemi ndivyo ulivyo ni mfano tu) utajaza watu wanamkubali. Sana sana kama unatakiwa kuhoji watu hamsini utafanya watu kumi wa vijiji vitatu vya karibu arobaini wengine unajazia chumbani. Sasa mawazo ya mtu mmoja yatawakilisha vipi umma wa Wadanganyika? Pia kunakuangalia eneo mathalani ukienda Pemba huwezi kusema asilimia kubwa wanashabikia kiongozi yeyote wa CCM lakini ikiwa inahusu Seif bila shaka utatarajia watu wamrembe. akili mkichwa unatunga majibu matano kwa wanao mkataa na mawili kwa wale uliowahoji.
Kuhusu nguvu ya umma Afrika hilo ni nchi chache sana labda ambako vyombo vya dola vimekinaishwa na utawala. CCm haijawahi kushinda Zanzibar lakini yako wapi Wapemba waliishiwa kumiminiwa risasi kama majambazi baada ya uchaguzi wa 2000. Waangalizi wa kimataifa ni bure kabisa hawana msaada ni mradi wa kujipatia posho tu. Hao AU sijui na akinani wengine si ndio wanasema uchaguzi ulikuwa huru na haki isipokuwa kulikuwa na kasoro ndogondogo. Angalia mfano Madagascar wananchi wmesema hawamtaki rais na yeye akaridhia tazama hawa wakoloni weusi hawataki kumtambua DJ.
Kwa hiyo basi Jk atashinda tena safari kwa zaidi ya asilimia 80 za mwaka 2005 pamoja na hizo poll kuonyesha asilimia 62. IS he a better President? It depends.
 
Capt. Hadock,
Heshima mbele, nakubaliana na mawazo yako ikiwa waliofanya maswala haya ni wajumbe wa vyama vya Upinzani au hata CCM wenyewe.. lakini hakuna kati yetu mwenye uhakika na wahusika wameufanya uchunguzi huu kwa manufaa ya chama gani. Asilimia 62 inaweza kuwa faida kwa CCM hata kama wameifanya wapinzani kwani CCM wanaweza kuongeza nguvu ya kujitangaza.. zikatumika mbinu nyingi kurudisha heshima yao hivyo aliyefanya utafiti huu akawa amewasaidia CCM.. Pia inaweza kuwa kama ulivyosema..
Pamoja na yote hayo tuchukulie kilichoandikwa ndivyo ilivyo, kumbuka tena mwaka 2005 walifanya uhcunguzi kama hivi na wakasema Kikwete alikuwa Popular kichizi, tukabisha hivi hivi na Kikwete akazoa kura za wananchi kishenzi bila riasasi mkuu wangu risasi zilikuwa kwa wabunge wala sio rais..Seis Sharif Hamad mwenyewe alimpitisha Kikwete hata kabla hajachaguliwa dhidi ya mgombea wake mwenyewe.. Haaa haaa haaa!...usifanye mchezo..

Trust me, hata mimi sikutegemea Mbowe anaweza kushindwa kwa kiasi kile pamoja na kwamba sikuwa mshabiki wa Mbowe..
Kisha mkuu wangu kuwa Popular haina maana ndio matokeo ya kura hapana haya ni mambo mawili tofauti..Lakini kufahamu kwamba upo uwezekano, kwamba kuna upenyo wa kuweza kushindana na CCM ktk kiti cha Urais nadhani hii inatupa moyo ule wa Mkapa mwaka 1995 ambapo polls pia zilikuwa chini sana pamoja na kwamba Nyerere alimpendekeza.. nakumbuka Nyerere ilimbidi kwenda karibu kila mkoa kumtangaza.. kampeni nzito ilitumika, na kama kawaida walalahoi wajamaa wakabadili kura zao... Bila mwalimu, Mkapa alikuwa nje kabisaaaa..Mrema angekuwa rais wa Tanzania 1995 kama sii mwalimu..He was popular kuliko Mkapa tena kwa mbali sana..
 
Back
Top Bottom