Kikwete anusurika, awang’oa wenzake

You mean vikao vya chini, hakuna kikao cha juu kuliko Mkutano Mkuu, first of all!

Second of all, you can not say Mkutano Mkuu una rubber stamp maamuzi ya Halmashauri Kuu kwa sababu Halmashauri Kuu inapeleka majina matatu, sasa Mkutano Mkuu una rubber stamp uamuzi wa jina lipi? hahahahaaa....that's extremely ridiculous.

Waandishi kwa nini msijielimishe kwanza kuhusu habari unayotaka kuchapisha gazetini?

Bahati mbaya sana wewe uko kinadharia zaidi,mimi nakwambia kinachotokezea kwenye huo mkutano wa kina Hadija kopa..ndio mana kikwete hakupitishwa kugombea urais mwaka 2005,ukifuatilia kilichotokea kwenye mkutano mkuu siku ile ndio unaweza kunielewa,halafu mkutano mkuu ukilisubiri jina unalolitaka na lisipokuwa miongoni mwa hayo matatu huo mkutano wako mkuu huwa unafanyaje?
 
WHO CARES ANYMORE ABOUT mambo ya CCM hii ya sasa ambayo majuzi imetwaliwa rasmi na mikono ya MAFISADI mara baada ya kuwaengua wazee wenye msimamo unaokaribiana japo kwa robo na ule wa Mwalimu Nyerere chamani??

Acheni CCM kife salama na hiyo mikakati ya kuzunguka mbuyu bila kumvua yeyote GAMBA LA UFISADI kama tulivyotarajia.
Hapo penye wekundu ndipo umekosea wazee gani hao ambao angalau wana misimamo inayokaribiana na Nyerere?akina Kingunge Mkapa,Mwinyi na wengineo ,ni kipi walichokifanya kuinusuru nchi katika hali tete tuliyonayo?hao wazee wamekuwa mzigo kwa wanachi wa wakawaida ,wapo kwa ajili ya matumbo yao na familia zao tu,heri waondoke tu kwanza ni wazee wanafiki wamejaa ushabiki na hawana uthubutu wa kukemee maovu kwa kuwa nao ni wazee wachafu.Mwacheni Nyerere apumzike ,wakati wote atakuwa kwenye miyo ya Watanzania
 
Da nimesoma habari hii, nimejikuta nacheka tu. Wabunge walipisha kichwa kichwa hawakujua kuwa ni kitanzi kwao du!
Naona sasa posho za wabunge zipunguzwe kwani sasa watakuwa hawafanyi kazi mbili kwa wakati mmoja kwani hizo posho za ubunge ndio walikuwa wanazitumia kwenye u NEC,sasa nimeamini ubunge unalipa kwani wabunge kwa kuwa wa NEC wanajihakikishia kuwa wabunge yaani huo mzunguko ni kama mchezo wa pia(kwa vijana wa zamani wanaijua pia),pia inazunguka mahala palepale huku ukiicharaza bakora ,unapocharaza bakora kwa spidi nayo ndio huongeza spidi,ukiacha inaanguka
 
Wassira anadaiwa kumuuliza mjumbe mwenzake wa Kamati Kuu na NEC, Abdulrahman Kinana; “Hivi hili suala la wabunge kutogombea u-NEC limefia wapi? Naye Kinana baada ya kucheka akamjibu; “aaah, mbona limeshapitishwa muda mrefu!”

tehetehete!!!! huyu alikuwa amesinzia lakini macho wazi......

Hata mie nadhani the Old man was totally asleep....tehe tehe teh teeee
 
Hili la kutenganisha madaraka ya kichama na madaraka ya kiserikali inatakiwa liwe suala la katiba ya nchi. Haitakiwi iwe kwa hiari ya chama cha siasa. Mwenyekiti, Katibu mkuu wa chama na viongozi wengine wakubwa wa chama haitakiwi wawemo ndani ya serikali ili kukeep checks and ballances. Yaani hao wakiteuliwa au Kuchaguliwa kuingia serikalini katika ngazi ya uwaziri, makamu wa rais, rais na vyeo vingine vyenye hadhi ya juu; inatakiwa wateme nafasi zao kwenye vyama vyao vya siasa!

Kwa hili la kutenga ubunge na U-NEC CCM wamepatia. Bahati mbaya wanaweza kuwa wamefanya hivi kwa kumlenga mtu mmoja au kikundi fulani cha watu. Hapo itakuwa kosa kubwa. Kama hawajafanya hivyo kumlenga mtu, basi kwa falsafa hiyo hiyo ya kutenga madaraka ya chama na yale ya serikali inatakiwa waendelee hadi kwa mawaziri na rais mwenyewe. Ili chama kiisimamie serikali vizuri serikali yake, basi inatakiwa chama kiwe na watu wengine ambao hawapo serikalini. Hawa ndo watakuwa na uwezo wa kusikia kilio cha wananchi na kuhakikisha kuwa wale walioko serikalini hawaendi nje ya mstari.

Kwa sasa hivi ukisema CCM iiwajibishe serikali, haiwezekani, kwani CCM na serikali ni kitu kimoja. Chama na serikali inatakiwa vibaki tofauti na huu ndo mfumo ulivyo katika nchi zote za kibepari ambako ndo mfumo wao tunaufuata. Huu mfumo wa chama tawala kuwa ndo serikali ni mfumo wa Kikomunisti na haufai kama vile ukomunisti usivyofaa.
 
Heshima mbele mkuu,

I honestly respect that weighty point raised with regard to the fate of the deposed CCM oldguards from party mainstream politics and the way their past that seems to be constantly haunting their present and determining their future in the country's political landscape!!!!

Siku zote hapa JF uungwana wetu ni kuitikia hoja katika uzito wake kama ambavyo ulivyojaribu kuipanga vema hapo chini.

Lakini hata ukiachilia mbali hao wazee wa CCM na masizi yote usoni, ukweli bado unabaki pale pale kwamba ndani ya CCM ambapo watu kama Rostam Aziz, Mgeja, Tambwe Hizza, Lukuvi, Dr Bana, Anne Makinda, Anne Kilango, ... na Makamba eti ndio watakaoakua miongoni mwao WAZEE WAPYA wa kutegemewa na chama hicho kuchuja majina kwenye kugombea urais ...!!!!!!!!!!!!!!!

Mpaka hapo hadhi ya shughuli hii itakua imeanguka thamani sana na kubakiwa tu na genge la madalali pale kwenye meza kuu huku wakitazamana usoni ki-nafiki kumpitisha mwenye DAU KUBWA ZAIDI kukabidhiwa tiketi ya chama hicho.

Ndio, nasema hiviii, CCM bila wazee WAADILIFU pale kwenye meza kuu ni sawa na kitoeo cha samaki wa maji baridi bila kitu chumvi ndani yake licha ya kuungwa kwa sana na hizo KANUNI MPYA ZA KI-MASLAHI BINAFSI.

Uzalendo mbeeeeele kama tailakini KATIKA HAKI, USAWA, UWAZI NA UWAJIBIKAJI kwa wote!!!!!!!


Hapo penye wekundu ndipo umekosea wazee gani hao ambao angalau wana misimamo inayokaribiana na Nyerere?akina Kingunge Mkapa,Mwinyi na wengineo ,ni kipi walichokifanya kuinusuru nchi katika hali tete tuliyonayo?hao wazee wamekuwa mzigo kwa wanachi wa wakawaida ,wapo kwa ajili ya matumbo yao na familia zao tu,heri waondoke tu kwanza ni wazee wanafiki wamejaa ushabiki na hawana uthubutu wa kukemee maovu kwa kuwa nao ni wazee wachafu.Mwacheni Nyerere apumzike ,wakati wote atakuwa kwenye miyo ya Watanzania
 
..ndio mana kikwete hakupitishwa kugombea urais mwaka 2005
Sasa kama Kikwete hakupitishwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2005 nani alipitishwa, Sofia Simba?

Nakwambia nyinyi waandishi ni weupe wa kutupwa mtaroni.
 
Ubebaji wa mkoba ni jambo moja na lile swala la 'unapiga nalo hatua ukielekea wapi na kwa ufanisi upi' nalo ni jambo lingine kabisa.

Mabadiliko ndani ya CCM ya hivi sasa yana kila dalili ya UJIO WA MGOMBEA DHAIFU kwa tiketi ya chama hicho kiasi kwamba ili uso wake uje uone mwanga wa jua la hapo kesho, ni sharti kwamba wenye nguvu kwanza wakadhibitiwe chamani kiaina kama ilivyo hivi sasa.

A resounding political boomerung is on the way and in such an irreversible manner to CCM's continued life.

Dr asha rose migiro kaandaliwa kubeba mikoba ya jk kiulaini tusubili yetu macho
 
Back
Top Bottom