Kigogo yupi anamiliki Jengo hili?

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
302
06_10_kv39fs.jpg


Jengo la Victoria House lililopo pembeni ya barabara ya Ali Hassan Mwinyi jijini, Dar es Salaam linalomilikiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Patrick Rutabanzibwa alisema jana kuwa kigogo mmoja wa shirika hilo anajinufaisha nalo.
 
06_10_kv39fs.jpg


Jengo la Victoria House lililopo pembeni ya barabara ya Ali Hassan Mwinyi jijini, Dar es Salaam linalomilikiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Patrick Rutabanzibwa alisema jana kuwa kigogo mmoja wa shirika hilo anajinufaisha nalo.
Mkuu did you mean nani anajinufaisha na jengo hilo?Otherwise umeshasema linamilikiwa na NHC na hivyo basi heading yako kuwa batili....Na badala yake ingekuwa "ni kigogo gani anajinufaisha na jengo hili la NHC" nk
 
Mkuu did you mean nani anjinufaisha nalo?Otherwise umeshasema linamilikiwa na NHC na hivyo basi heading yako kuwa batili.
Sorry mkuu nilikuwa na maana ya nani anajinufaisha nalo.
 
...........stupid Tanzanian leaders!! mtu ni mtendaji mkuu wa wizara husika (katibu mkuu), NHC ipo chini yake, anajua kuna officer NHC anafanya mafyongo na anamjua huyo mtu, unasema kwenye media kuna kigogo wa NHC anafanya this and that....is that all he can say and do on the matter? he better kept quite because that aint mean anything to rectify the issue!!!!! ni matatizo ya kulindana na kujilinda! dare to something heroic!! mtoa mada nae atafute contacts za Rutabanzibwa amuulize!
 
Upuuzi mtupu. Kwa nini huyo kigogo wa NHC asiwajibishwe wakati anafahamika na wakubwa zake? Tutaendelea kulindana hadi lini? Hii inasikitisha sana.
 
Irresponsibility at the peak of tune!...Mkuu huyo alitakiwa awasilishe barua ya kushindwa kazi kwa waziri kwanza ndo aeleze upupu huu!
 
06_10_kv39fs.jpg


Jengo la Victoria House lililopo pembeni ya barabara ya Ali Hassan Mwinyi jijini, Dar es Salaam linalomilikiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Patrick Rutabanzibwa alisema jana kuwa kigogo mmoja wa shirika hilo anajinufaisha nalo.



NHC lawamani kwa rushwa

KATIBU Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Patrick Rutabanzibwa, amesema kati ya mashirika mabovu nchini, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) linaongoza na hakuna asiyejua kuwa kila anayetaka nyumba lazima atoe rushwa.

Amesema NHC inatakiwa kujua ipo kwa ajili ya kuhudumia umma na si kujinufaisha na lazima ijirekebishe kiutendaji na kukabiliana na changamoto na kufahamu zilipo mali zake.

Rutabanzibwa alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akifungua kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa NHC na kuwapongeza wafanyakazi wa shirika hilo kwa kuvumilia licha ya matatizo yanayowakabili.

"Hili ni shirika, ni kubwa sana katika Afrika Mashariki, kiutendaji mjirekebishe ili mkabiliane na changamoto zinazowakabili, mjue mali zenu ziko wapi na zikoje," aliwambia Rutabanzibwa.

Aliitaka NHC iangalie mikataba iliyonayo na sifa mbaya iliyoko katika shirika hilo iondoke, kwa kuwa hakuna asiyejua kuwa rushwa imepewa kipaumbele ili kupata nyumba ya shirika hilo.

"Lazima sifa hiyo ifutwe kwa vitendo, kuwe na taratibu za wazi za kuweka wapangaji … matumizi mabaya ya vyeo yachukuliwe hatua, kwani wanatumia nyumba za shirika kuweka wafanyabiashara wao kwa mfano Victoria House," alisema Rutabanzibwa.

Katika mfano huo wa Victoria House, alisema viongozi wa shirika hilo wamepangisha wafanyabiashara wao kwa manufaa yao na si ya shirika.

Alisema ni vyema shirika likafahamu kuwa mali hiyo si ya viongozi, bali ni ya umma na isitumike kujinufaisha binafsi, ilindwe kwa niaba ya wote.

Awali akizungumza, Mkurugenzi wa NHC, Nehemiah Mchechu, alisema sasa Shirika linapitia mikataba 76 ya biashara na watachukua uamuzi mgumu ikiwa ni pamoja na kunyang'anywa baadhi ya miradi kwa kuwa shirika liko katika hali ngumu.

Alisema kwa waliovunja mikataba na NHC watanyang'anywa nyumba ili viwanja hivyo viboreshwe zaidi na kulipatia shirika mapato na si hasara.

"Hakuna anayetaka kunyang'anywa kiwanja chake, waliovunja mkataba, yaani alikubali kujenga kwa miaka mitatu, lakini bado hajafanya chochote atanyang'anywa eneo hilo," alisema Mchechu.

Aliongeza kama wapo wenye viwanja na havijaendelezwa kwa miaka minane NHC lazima ichukue eneo hilo na utekelezaji huo utaanza kwa wenye miradi mikubwa.

"Hakuna asiyejua kuwa nyumba za NHC zina kodi ndogo, jambo ambalo linatukwamisha hata kujiendeleza na kulisababishia shirika hasara, kwa mfano kuna nyumba Singida ambapo gharama za ukarabati ni Sh milioni 33 lakini kodi ni Sh 45,000," alisema Mchechu.

NHC ilianzishwa mwaka 1962 kwa lengo la kujenga nyumba za makazi na biashara kwa ajili ya wananchi.

Chanzo: Habari Leo
 
Lukuvi kanyesha njia -- kwamba kulindana kunaweza kuwa historia. Ni kweli Rutabanzibwa anapiga blah blah tu -- hawezi kufanya chochote kwani naye ana mazito yake. Au tumesha sahau Mkataba wa IPTL?

Hivi mnamjua mwenyekiti wa sasa wa NHC? Kama mnamjua, basi rushwa yote ya sasa ndani ya shirika hilo ina-revolve around him! Huyu bwana nadhani ni billionaire, na kisha jiuzia nyumba kadha za NHC.
 
Kwa ninavyomfaham Mheshimiwa Patric Rutabanzibwa huyo kigogo hayuko salama kabisa.
 
Lukuvi kanyesha njia -- kwamba kulindana kunaweza kuwa historia. Ni kweli Rutabanzibwa anapiga blah blah tu -- hawezi kufanya chochote kwani naye ana mazito yake. Au tumesha sahau Mkataba wa IPTL?

Hivi mnamjua mwenyekiti wa sasa wa NHC? Kama mnamjua, basi rushwa yote ya sasa ndani ya shirika hilo ina-revolve around him! Huyu bwana nadhani ni billionaire, na kisha jiuzia nyumba kadha za NHC.

Asante Mkuu Zak: Huyo ni Balozi S. D. Hemed na ninavyosikia, hilo jengo kama hajalimilikisha kwake moja kwa moja, basi ndiye anayenufaika nalo. Habari ndo hiyo!
 
Siasa za kulindana hizo nyie hamzijui siasa za "sitaki niguswe hunijui mimi ni nani" Hizo ndio zipo Bongo kwa hiyo watu wanaogopana kihivyo
 
Siasa za kulindana hizo nyie hamzijui siasa za "sitaki niguswe hunijui mimi ni nani" Hizo ndio zipo Bongo kwa hiyo watu wanaogopana kihivyo

Pengine hiyo ipo pia -- lakini hali hii ni lazima ibadilike ili kuepusha vita ya wenywewe kwa wenyewe hapa nchini. tatizo katika viongozi wa CCM ni kwamba everyone of them sees as far as the ened of his/her nose only. Hawajui kabisa kama wanapanda mbegu za uhasama.
 
...........stupid Tanzanian leaders!! mtu ni mtendaji mkuu wa wizara husika (katibu mkuu), NHC ipo chini yake, anajua kuna officer NHC anafanya mafyongo na anamjua huyo mtu, unasema kwenye media kuna kigogo wa NHC anafanya this and that....is that all he can say and do on the matter? he better kept quite because that aint mean anything to rectify the issue!!!!! ni matatizo ya kulindana na kujilinda! dare to something heroic!! mtoa mada nae atafute contacts za Rutabanzibwa amuulize!

Mkuu,

Hapa Tanzania kila mtu anayo haki ya kulalamika na hakuna mwenye wajibu wa kuchukua hatua. Kwa hiyo brother Ruta ni wale wale tu. Hii ni cha mtoto. Hebu angalia tatizo la msongamano wa magari. Bado raisi tu, siku si nyingi naye ataanza kuamka saa 10 kuwahi ili aepuke kunaswa kwenye hiyo kadhia!
 
Kama Rutabanzibwa anamjua huyo kigogo nilitegemea atakwenda mbali zaidi na kusema tayari ameshafikishwa mahakamani badala yake analalamika, yeye ndiye mtendaji mkuu wa wizara sasa analalamika kwa nani au anataka rais amsaidie kufanyakazi.
 
Kama Rutabanzibwa anamjua huyo kigogo nilitegemea atakwenda mbali zaidi na kusema tayari ameshafikishwa mahakamani badala yake analalamika, yeye ndiye mtendaji mkuu wa wizara sasa analalamika kwa nani au anataka rais amsaidie kufanyakazi.

Inatisha sana. Katibu mkuu wa wizara analalamika kuwa kuna kigogo sijui anafisadi shirika. Kama hawezi kuchukua hatua, nani atafanya hivyo? Au tuaminishwe kuwa Katibu mkuu hana mamlaka hayo?
 
Asante Mkuu Zak: Huyo ni Balozi S. D. Hemed na ninavyosikia, hilo jengo kama hajalimilikisha kwake moja kwa moja, basi ndiye anayenufaika nalo. Habari ndo hiyo!
Huyu muheshimiwa si alishastaafu? Wanashindwaje kumnyang'anya wakati wao ndo walioko kwenye ofisi?
 
Tunataka viongozi wanaothubutu kama Lukuvi. Londa alikua monster lakini Lukuvi kamgusa, na wengine waige.
 
Katibu Mkuu wa Wizara anawambia wafanyakazi wa NHC (shirika ambalo lipo chini yake) kuna kigogo anajinufanisha na jengo fulani. Yeye katibu Mkuu tayari ana hizo taarifa na madaraka anayo (au anaweza kumshauri Waziri/ Rais) badala ya kurekebisha ufisadi huo anawaambia wafanyakazi walio chini yake ili wafanye nini????
 
Tunataka viongozi wanaothubutu kama Lukuvi. Londa alikua monster lakini Lukuvi kamgusa, na wengine waige.


Huyo Lukuvi amefanya nini zaidi ya kufunga ofisi na kuwakamata Watuhumiwa; hawa watu hawajafikishwa mahakamani...sana sana wamefikishwa kituo cha Polisi...mbona mnakuwa wepesi sana kutoa sifa lukuki kabla ya kuona matunda yoyote??!!
 
Back
Top Bottom