Ok,alikimbia kwa sababu alijua watu watamuua ,hilo liko wazi kabisa
so wangemuua kwasababu na yeye kaua?
Ok,alikimbia kwa sababu alijua watu watamuua ,hilo liko wazi kabisa
hata mahakama ikisema hana hatia..mtoto huyu kwa jamii hachomoki...ameishapatiwa a.k.a yake as 'serial killer'
Kanumba alikuwa amelewa chakari! Kuna mtu wa nne alikuwa ndani ya nyumba! Ajabu hatajwi. Lulu alipigwa sana na marehemu. Tusimuhukumu Lulu Kosa la marehemu kuendekeza ulevi
PF3 inaweza kuandikishwa hata mtu anapokuwa hosptalini, mara nyingi hutegemea hali ya mwenye majeraha.
Mbu hivi kweli kabisa niambie relevance ya hiLi hitaji la PF3 form...
bht hakuna ni ujinga fulani tu, hili swala lilijadiliwa sana bungeni miaka ya 90 mwanzoni lakini wapi...PF3 liko tu!
ilitakiwa mtu anapatiwa huduma, hospitali wanatoa taarifa polisi, wakati anapatiwa huduma ..polisi wanakuja pale kuchukua taarifa kama majeraha ni criminal cases au la
hata mahakama ikisema hana hatia..mtoto huyu kwa jamii hachomoki...ameishapatiwa a.k.a yake as 'serial killer'
huyu mdogo wake Kanumba nani kamruhusu kutoa maelezo na lawama? kwa nini ajitoe ilihali alikuwa nyumbani? kwa nini polisi walimuacha an hawakuondoka naye?
Waberoya, hapa umeongeza chimvi kidogo. Killer? YES, but a Serial Killer? Mhhh, kwani Kanumba ni wa pili, tatu, ......?
PF3 inaweza kuandikishwa hata mtu anapokuwa hosptalini, mara nyingi hutegemea hali ya mwenye majeraha.
Umegandisha mno mawazo yako. kama mgonjwa ana hali mbaya anapokelewa Hospitali, PF-3 inafuata baadae baada ya taarifa kufika polisi. kwa kukusidia,ukiona mtu yupo serious,wengine wanampleka Hospitali na wengine wanakwenda Polisi.Watunga sheria hawajali maana wao huwa wanatibiwa wakisema tu "Mimi mbunge" hawaoni umuhimu wa kusawazisha sheria
Sijui mantiki gani inayotusukuma watanzani kutaka PF3 kwanza kabla ya tiba....
Sisi si wazima kichwani
Binafsi sijawahi kuwa mpenzi wa movie star yeyote wa bongo. Nimekuwa naangalia movie za Kanumba na wasanii wengine kupitia mabasi niendapo mikoani, na nimemfahamu huyo LULU kupitia huu msiba.
Ni wazi kabisa huyu LULU hawezi kuepuka kunyooshewa vidole kwa kuwa ndiye mtu wa mwisho aliyekuwa na marehemu angali mzima. Nenda uendako, LULU atakuwa mshukiwa wa kwanza. Hasa ukizingatia alikimbia baada ya kutoka kwenye chumba ambacho Kanumba alikuwa kaanguka akiwa kapoteza fahamu na anahitaji msaada (Naamini alikuwa amechanganyikiwa baada ya kukumbana na hali hiyo).
Ninamwonea huruma kwa shida anazopata binti huyu na jinsi saikolojia yake itakavyoharibika, ila sijui kama anastahili au hastahili. Haijalishi kama Kanumba alikuwa anacheza karate au alikuwa na umbile kubwa bado binti huyu anaweza akawa anahusika au hahusiki na kifo hiki. Poleni sana ndugu na jamaa za Kanumba na LULU ambao kwa wakati huu mnapitia kipindi kigumu sana.
But She can not escape this unless the court clear her of any wrongdoing. LULU is still guilty until proven otherwise.
Wanajua sana. ndio maana unaona wanawapokea majeruhi hata 100 wa ajali bila ya PF-3.ndio nasikia kwako mkuu......hospitalini wanajua haya??
Ok,
so wangemuua kwasababu na yeye kaua?
Mbona madkatri wanakataa kutibu watu mpaka waonyeshwe hiyo PF3?PF3 inaweza kuandikishwa hata mtu anapokuwa hosptalini, mara nyingi hutegemea hali ya mwenye majeraha.
HII NILIISOMA KULE GLOBAL NA HUWA KILA MARA NILIKUWA NIKIMWONA KANUMBA NAKUMBUKA HII NA MWISHO NILIPOSIKIA HABARI YA KIFO CHAKE NA CHANZO CHAKE STORY HII ILI- CLIK KWENYE KICHWA CHANGU
kanumba anahitaji tiba
Posted by GLOBAL on October 4, 2011 at 9:30am
View Blog
Madaktari wasema anaumwa Personality Disorder
Steven Charles Kanumba ni staa mkubwa Bongo. Jina lake kwa sasa lina hadhi ya kimataifa. Inawezekana akawa ndiye msanii kijana mwenye mvuto kijamii kuliko mwingine yeyote.
Mvuto wake unatambulika ndiyo maana makampuni mengi ya kibiashara na kijamii hupenda kumtumia kama balozi wao. Kanumba ni fahari ya Tanzania, ni kivutio cha vijana wengi wa kizazi kipya.
Lengo la makala haya ni kumshauri Kanumba. Pamoja na sifa nyingi alizonazo kuna makosa machache huwa anayafanya, hivyo anahitaji kupokea ushauri ambao utamsaidia kuepuka visa vya hapa na pale ambavyo humvunjia heshima.
MATATIZO NI NINI?
Hapa kuna baadhi ya matukio ambayo yamewahi kuripotiwa, hivyo kumchafua Kanumba, kwa hiyo anapaswa kujitenga nayo ili heshima yake ibaki kuwa juu.
MOSI: Ugomvi na aliyekuwa mpenzi wake, Wema Sepetu mpaka kufikia hatua ya kupelekana polisi.
PILI: Sylvia Shally alikuwa mpenzi wake lakini naye waligombana mpaka kufikishana polisi. Mrembo huyo alitinga ubaoni akidai Kanumba alimtishia maisha.
TATU: Alizama kwenye dimbwi la mahaba (kama alivyodai mwenyewe) na Miss Ilala 2003, Nargis Mohamed. Walipoachana, alifunguka kuwa mrembo huyo ambaye kwa sasa ni mke wa mtu, alikuwa anamtesa sana.
NNE: Anadaiwa kuwa na uhusiano wa siri na Aunt Ezekiel (ingawa wote wanakanusha), juzikati walitibuana, kisha yeye alimpa mitama mrembo huyo na kusababisha soo hilo litinge polisi.
ISHU IKOJE?
Kwa nini kila siku ugomvi na wanawake? Inakuwaje polisi na yeye kwa makosa ambayo yana alama za kimapenzi?
Daktari aliye pia bingwa wa saikolojia, Godfrey Chale aliiambia Showbiz kuwa tatizo linalomsumbua Kanumba linaitwa Personality Disorder na tiba yake ni ushauri na nasaha.
"Personality Disorder ina matawi mawili, inferior (kujihisi unyonge) na superior (kujiona unahitaji kuogopwa). Vitu hivyo hutengeneza wivu na migogoro mingi (conflicts).
"Mtu kama huyo atakuwa anajiona superior, kwa hiyo hujikuta ana chembechembe za dharau kwa kuamini ni maarufu na ni lazima mpenzi wake amnyenyekee. Ikiwa atakutana na hali tofauti, mfano akigundua mwenzi wake hafuati anavyotaka au anamsaliti, kwa kawaida hujisikia vibaya.
"Ile tabia ya kujiona superior ndiyo humfanya ashindwe kukubali matokeo hasi kutoka kwa mwenzi wake, kwani anaamini yeye ni mtu wa kunyenyekewa. Kutokana na hilo, ndiyo maana hupata kesi za kugombana au kusumbuana na wapenzi wake kwa sababu ya kutokubali matokeo," alisema Dk. Chale ambaye ana hospitali binafsi, pia hutoa ushauri wa afya kupitia magazeti ya Global Publishers.
Dokta Patrick Mirumbe wa Hospitali ya Capricorn alisema: "Tatizo lake ni wivu. Hiyo naweza kuzungumza kwa kifupi na tiba yake ni ushauri na nasaha. Akipata ushauri wa kutosha anaweza kubadilika na kuwa mtu safi.
KANUMBA ASHIKE NINI?
Mwanasaikolojia ambaye hutoa ushauri wake kwenye magazeti ya Global Publishers, Richard Manyota alisema kuwa jambo ambalo Kanumba anapaswa kushika ili kuepukana na vitu ambavyo vinaweza kushusha heshima yake ni kujitambua.
"Katika makundi ya saikolojia, lipo linaloitwa Legal Psychology. Hili linamtaka mtu atambue mazingira anayoishi na ufahamu wake. Kanumba anatakiwa ajijue yeye ni mtu maarufu na heshima yake ipo juu, kwa hiyo asipojitambua itakuwa tatizo sana.
"Namuomba Kanumba ajijue yeye ni nani, awe mwepesi kuepukana na shari ndogo ndogo ambazo mwisho wake huwa ni mbaya, kama kupelekana polisi. Nadhani akijitambua, akiwa mwepesi kuelewa dalili za ugomvi, ataweza kujirekebisha.
"Anaweza kwenda kwa washauri zaidi lakini hapa mimi nampa kitu muhimu zaidi na akishike. Anaweza kuishi kwa amani maisha yake yote bila migogoro. Akijitambua, hata anapoachana na wapenzi wake, amani itatawala na hakutakuwa na fujo za polisi," Manyota.
HITIMISHO
Naamini kuwa maneno ya madaktari akiyashika sawasawa pia ushauri wa mwisho wa mwanasaikolojia Manyota, bila shaka atashinda mitihani inayomkabili. Lengo ni kuona heshima yake inazidi kupaa juu na msimamo ni kwamba Kanumba bila polisi inawezekana.
IMEANDIKWA NA LUQMAN MALOTO
MY TAKE: Tujaribu kuwa tunafwata ushauri wa wataalamu pengine leo tungekuwa tunaongea tofauti
Foundation, asante kwa hoja hii. Mimi naamini katika kweli daima, na ni kweli siku zote ndio husimama. Haka kabinti katatakiwa kusema kweli. "Lulu should tell nothing but the truth" na kwa kutumia hii kanuni "Seek the truth and the truth will set you free" katakuwa huru!.
Umegandisha mno mawazo yako. kama mgonjwa ana hali mbaya anapokelewa Hospitali, PF-3 inafuata baadae baada ya taarifa kufika polisi. kwa kukusidia,ukiona mtu yupo serious,wengine wanampleka Hospitali na wengine wanakwenda Polisi.
Binafsi sijawahi kuwa mpenzi wa movie star yeyote wa bongo. Nimekuwa naangalia movie za Kanumba na wasanii wengine kupitia mabasi niendapo mikoani, na nimemfahamu huyo LULU kupitia huu msiba.
Ni wazi kabisa huyu LULU hawezi kuepuka kunyooshewa vidole kwa kuwa ndiye mtu wa mwisho aliyekuwa na marehemu angali mzima. Nenda uendako, LULU atakuwa mshukiwa wa kwanza. Hasa ukizingatia alikimbia baada ya kutoka kwenye chumba ambacho Kanumba alikuwa kaanguka akiwa kapoteza fahamu na anahitaji msaada (Naamini alikuwa amechanganyikiwa baada ya kukumbana na hali hiyo).
Ninamwonea huruma kwa shida anazopata binti huyu na jinsi saikolojia yake itakavyoharibika, ila sijui kama anastahili au hastahili. Haijalishi kama Kanumba alikuwa anacheza karate au alikuwa na umbile kubwa bado binti huyu anaweza akawa anahusika au hahusiki na kifo hiki. Poleni sana ndugu na jamaa za Kanumba na LULU ambao kwa wakati huu mnapitia kipindi kigumu sana.
But She can not escape this unless the court clear her of any wrongdoing. LULU is still guilty until proven otherwise.