Kifaa cha CHADEMA chakamatwa na watu 6 waliomvamia Dr. Mvungi

kofia na rangi ndio ishara huku tulipo ukivaa fulana yenye rainbow tunajua wewe LGT bwabwa hatuulizi! Hapo kuna mahusiano makubwa tu!

.utambulisho wake ni viroba original.
ImageUploadedByJamiiForums1383683507.883260.jpg
View attachment 119951
 
uliyepost hii thread, acha KUJIONESHA ZOMBIE! Tuseme wewe kwako habari ni kifaa cha CHADEMA?!!! Bila shaka ulitoka na DIV. 5 shuleni! Mbona sare za jeshi zimetajwa na kuoneshwa? Mbona kuna pesa, simu na laptop zimeporwa? vyote hivyo kwako si habari? Mbona kuna bangi na gongo imekamatwa? Yote hayo kwako si habari! Hata hujaguswa na hali ya majeruhi, duh! Natamani kukagua vyeti vyako vya shule.

Sitakulaumu sana, mfumo wetu ndio umekufikisha hapo.
 
Wangekuwa Waislam wamekamatwa na CD wangeitwa magaidi, sijui CHADEMA watasemaje Mungu mkubwa.
Ukitumia akili yako vizuri utakuwa na busara... Kwa hiyo Ustaadhi ilunga aliyefichwa unataka tusemeje?
 
Hivi vyote vimekutwa katika eneo la tukio, aidha kwa kupandikizwa au ni kweli. wahusika walikuwepo! Tatizo ni pale mzani unapoelemea CDM kuliko Jeshi! Siasa zinawafanya baadhi ya watu kutotumia akili zao vizuri!
 
Mbona kofia ndio mmekuja juu kuna nyara za nchi hapo ambazo ni sare za Jwtz mbona hamuhoji wamepata vp?
 
Kuna mambo ya muhimu ambayo huwa tunayageuzia siasa na ushaidi wake unaharibika. Mojawapo ni hili la utekaji na kujeruhi watu na wahusika wanaendelea kutesa. Ni tanzania tu ambayo tukio la kihalifu likitokea polisi tunaotegemea waje na ushahidi walioutafuta wanaanza kuingiza siasa. Ni hatari sana kwa nchi hii kuwa na polisi ambao msemaji wao anakuwa kova.! Tusiingize siasa za ccm na cdm kwenye mambo nyeti, kumbukeni huyu ni mtu wa ngapi kufanyiwa hivi? Wangapi wengine walivamiwa na kujeruhiwa na hatujui kama kuna kesi za hao wahusika? Wangapi wamemwagiwa tindikali na hakuna kesi ya maana inayoendelea zaidi ya siasa.?
 
Kukutwa na kofia ya CHADEMA haimaanishi tukio limefanywa na CHADEMA. Mambo mengine jamani hayafai kufanyiwa propaganda. You peoplea be human sometimes,msipende kuchumia tumbo wakati wote.
 
Mkuu Ritz
Chadema ni chama kigaidi kinatumia kila njia; makamanda wakipewa misuba na gongo wanaingia kazini kudhuru watu hii Chadema kaskazini ni hatari sana kwa usalama wa raia!

cc mwigulu.kinana.
 
Last edited by a moderator:
Sasa kama chadema ndio walifanya hayo, kulikuwa na haja ya kwenda na kofia yao ili wagundulike? The most logical explanation ni kwamba kama ni kweli hiyo bendela iliachwa na wahusika basi ni wazi ni wapinzani wa damu wa chadema. Ni sawa na mtu kukuibia id yako na kufanya uhalifu afu akaidondosha ili balaa lielekezwe kwako. Hakuna mantiki yoyote kwa mtu kufanya uhalifu huku amebeba vitambulisho vyake! Most likely vitambulisho atakavyokuwa navyo vitakuwa ni feki!
Bila hata kuumiza akili, tukio hili ni wazi halikufanywa na chadema.
 
Hebu tuache hizi siasa zisizo na tija tafadhalini. Kofia ya chama chochote inaweza kuvaliwa na mtu yeyote.
Kwani balozi wa china naye alikuwa ni mwan ccm????
 
CHADEMA wamechanganyikiwa , wanawaza kufaidika kwa kila jambo bila kujali madhara ya baadaye
 
Hebu tuache hizi siasa zisizo na tija tafadhalini. Kofia ya chama chochote inaweza kuvaliwa na mtu yeyote.
Kwani balozi wa china naye alikuwa ni mwan ccm????

Mkuu huo ndio ukweli, inawezekanaje ufanye maasi halafu uache kidhibiti pale? Kwa vyovyote ni hasimu wake aliye na IQ ndogo kamfanyia uhuni
 
Kifaa cha Chadema?! Waliotekeleza mauaji ya Mh.Mvungi bila shaka wanafurahi wanapoona upelelezi umeshapoteza dira kwa kuweka focus kwenye ''kifaa cha Chadema''.

Wanausalama fanyeni kazi yenu mkichanganya siasa na masuala ya uhalifu mnawapa wahalifu mwanya mkubwa sana. Kuna siku wataacha kadi ya chama fulani kwenye eneo la uhalifu na kuwapoteza maboya katika upelelezi wenu.

Mpelelezi makini ni yule asiyeongozwa na trick za mhalifu. Kwa mfano ukikuta gauni eneo la tukio na ukabaki kuaminin kuwa aliyefanya tukio ni mwanamke utakuwa unakosea sana.
 
Back
Top Bottom