Kibosile wa wastaafu wa iliyokuwa jumuiya ya Afrika mashahriki ajisalimisha polisi

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Mwenyekiti wa wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki - EAC - jana alijisalimisha kwa polisi kutokana na kutoa kauli ya uzushi na yenye kudhaniwa ilikuwa ya kichochezi pale alipodai mmoja wa wastaafu hao aliyemwagiwa maji moto yenye kuwasha sana maarufu kama "maji pilipili" alikuwa ameuawa na maji hayo.

Baada ya mzushiwa ufu huyo kuibuka na kudai maji hayo yalimpa madhara madogo tu lakini hayakumuua basi polisi walianza msako mkali wa kumtafuta kibosile yule wa EAC ili wamfikishe kwenye mahakama kwa uchochezi na uzushi.

Kibosile tajwa alijisalimisha polisi na kukiri ya kuwa taarifa zake hazikuwa sahihi na hivyo aliomba msamaha.

Haikufahamika mara moja kama polisi wataendelea na hatua zao za kumfikisha mahakamani au wamemsamehe. Lakini afande Kova ambaye ni mtu wa busara sana ninahisi atakuwa amemsamehe ili mradi asirudie tena kutoa taarifa ambazo hana uhakika nazo...............
 
Huu ni mtego ulio backfire kwa CCM....walipanga hii kitu ili Dr Slaa aingie kichwakichwa halafu wamlete huyo Mzee hadharani ili Dr AONEKANE MZUSHI
 
hivi ni kova ndiye anayetakiwa kusamehe au mahakama. mi nionavyo kazi ya polisi ni kusimamia sheria na si kufanya kazi za mahakama. huyo kibosile anatakiwa kusamehewa na mahakama; hapo ndipo haki inaweza kupatikana.
 

MWENYEKITI wa Kamati ya Wastaafu wenye madai wa iliyokuwa Jumua ya Afrika Mashariki, Nathaniel Mlaki, akisindikizwa na polisi kwenda kizimbani katika Mahakama ya Hakim Mkazi,Kisutu, Dar es Salaam, kujibu kesi ya kufanya vurugu, katika barabara ya Kivukoni, mjini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.

MLAKI.JPG


MWENYEKITI wa Kamati ya Wastaafu wenye madai wa iliyokuwa Jumua ya Afrika Mashariki, Nathaniel Mlaki, akipanda 'defender' la Polisi kwenda rumande, baada ya kushindwa masharti ya dhamana.

Mi ni likuwa naongezea msisitizo tu
 
Kapewa dhamana ya watu 2 kila mmoja kasaini dhamana ya tsh.500,000/-hivyo jamaa yupo nje kuendelea mapambano aliyotumwa na chama fulani yeye na wenzie Tamwa,Tgnp n.k
 
Back
Top Bottom