Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 15,335
- 24,230
King Kinya, mwandishi wa habari wa aina yake, leo katoa mpya.
Katika gazeti la Mwananchi pg 8, kibonzo, cartoon yenye utata imesheheni.
Kuna kaburi la mtu, inaelekea ni huko mikoani, maana hakuna kaburi lingine karibu, linafukiwa hilo kaburi na takataka, za watu waliokula na kushiba.
Aina ya takataka ni mifupa ya kuku, bia chupa tupu na sahani zilizotumika.
Cha kushangaza, wa mwisho anayetupa, kavaa shati la mikono mirefu, shati ya kijani!!!!
Wana JF, tufumbue hili fumbo.
Lakini wewe King Kinya wewe, ingekuwa Awamu ya Tano, Kamanda Muliro angekuhusu.