Kiboko ya vigogo

dazu

JF-Expert Member
Feb 26, 2011
365
76
Kwa wale wanajamvi wenzangu ambao ni wakongwe kidogo na wafuatiliaji wa soka, bila shaka tutakua tunakumbuka kwamba kulikua na timu ilikua inajulikana zaidi kama kiboko ya vigogo. Nayo ni Reli ya Morogoro. Kikosi chao cha miaka hiyo huwa kinanivutia hata leo, kwa jinsi kilivyokua kinatoa wakati mgumu kwa timu kongwe kama simba na yanga. Kikosi hiki golini alikua anasimama Athumani Msumari, Full beki 2 Mohamed Mtono, 3 Abdalla Mkali, 4 ni Ramadhani Kilambo, Sentahafu Gasper Lupindo, namba 6 ni Christopher Maiko, winga namba 7 ni Nassib Abbas namba 8 Yusuph Macho wakati mwingine hucheza Bonifas Njohole, Sentafowadi yupo Duncan Butinini, namba 10 David Mihambo halafu winga ya kushoto hucheza Mbui Yondan au Peter Mjata. Kikosi hiki ambacho kilikua chini ya Simkoko, Kilikua ni hatari mno hasa kinapokutana na yanga au simba.
 
Wachezaji zamani walikua wanazingatia shule, sasa hivi akisajiliwa ligi kuu na shule basi.

Kweii kabisa,lakini pia zamani ilikuwa ni kucheza kwa kujifurahisha,heshima na sifa.Siku hizi ni pesa mbele na akishanunua ki corola ndo unamkoma kabisa...,totoz na kinywaji kwenda mbele.
 
David Mihambo yuko wapi siku hizi, kuna kipindi alichezea Simba na kulikuwa na mechi kati ya Simba na Gor-mahia alinikomeshea sana wale wakenya.
 
Back
Top Bottom