Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,808
- 6,500
Historia ya CCM imejaa maajabu ambayo kama siyo taranta ya wepesi wa kusahau waliobarikiwa Watanzania wengi kwa sasa CCM ingekuwa ni chama kilichobaki kwenye vitabu vya historia achilia mbali ya kuwa chama cha upinzani nchini.
Tarehe 7 Februari 2008 ilikuwa ni siku iliyoingia kwenye vitabu vya histoaria baada ya Waziri Mkuu wa Serikali ya CCM kwa mara ya kwanza kujiuzuru kutokana na kuhusishwa na kashfa ya ufisadi kupitia kampuni feki iliyokuwa inaitwa Richmond Development Company LLC.
Hii ilikuja baada ya Dk. Harrison Mwakyembe ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge alipoamua kutaja mambo waliyodokezwa kwenye tume na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tanesco, Marehemu Balozi Fulgence Kazaura aliposema Richmond ilikuwa mradi wa Bwana Mkubwa na Mshiriki wake mkubwa kibiashara akimaanisha Edward Lowassa na Rostam Aziz.
Repoti ya Tume ya Bunge kuhusu sakata la Richmond iko HAPA
Baada ya Kamati Teule ya Bunge kusoma taarifa yake tarehe 6 Februari 2008 kuhusu sakata la Richmond Development Company LLC, Edward Lowassa akajikuta akiwa mmoja wa maadui namba wani wa taifa.
Baadaye Februari 5, 2011 kwenye sherehe za miaka 34 ya CCM mjini Dodoma, tukasikia Mwenyekiti wa CCM-Taifa, Rais Jakaya Kikwete akiwaasa wana-CCM kwamba itabidi CCM ijivue gamba.
Tarehe 16 Julai 2011 tulishuhudia Samuel Sitta, Dkt. Harrison Mwakyembe, Nape Nnauye, Lazaro Nyalandu, Ole Sendeka, Prof David Mwakyusa , Asha Abdallah Juma na viongozi wakuu wa CCM Mkoa wa Mbeya wakijitokeza kwenye mkutano wa hadhara mkoani Mbeya katika lengo la kuufikisha ujumbe wa kujivua gamba. Hawa walikuwa vinara wa mapambano yaliyopelekea kujiuzuru kwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na kuwa public enemy number one.
Samuel Sitta, Dkt. Harrison Mwakyembe, Nape Nnauye, Lazaro Nyalandu, Ole Sendeka, Prof David Mwakyusa , Asha Abdallah Juma na viongozi wakuu wa CCM Mkoa wa Mbeya wakielekea kwenye mkutano wa hadhara, Mbeya katika lengo la kuufikisha ujumbe wa kujivua gamba.
Aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Harold Wilson aliwahi kusema, A week is a long time in politics.
Miaka minne baadaye, tunaanza kushuhudia wale waliokuwa wanataka kuwavua magamba kina Edward Lowassa na kundi lake wakiwa katika hati hati ya kuanza kuchekwa na waliokuwa wanawacheka au wako ukingoni kukosa kazi au kufukuzwa ndani ya CCM!.
Vyombo vingi vya vya habari kwa sasa hivi vinawashambulia wapinga rushwa/ufisadi ndani ya CCM kiasi kwamba hata jamii imeanza kununua hoja za vyombo vya habari kwa kuwaona wapinga rushwa/ufisadi kama ni debe tupu. Money talks hasa kwenye jamii yenye ufinyu wa uelewa!
Kuna uwezekano mkubwa wanaojiita CCM Imani/wapinga rushwa/ufisadi ndani ya CCM wako mbioni kufagiwa na kutupwa nje ya CCM na fagio la mafisadi
Wapinga rushwa/ufisadi are about to learn a stern lesson about the vigour of mafisadi!.
Mmarekani aitwaye Jim Henson aliwahi kusema, If you can't beat them. Join them.
Kuna baadhi ya wapinga rushwa na ufisadi wameanza kukubaliana na maneno ya Jim Henson!
Hii ndiyo Tanzania!
Tarehe 7 Februari 2008 ilikuwa ni siku iliyoingia kwenye vitabu vya histoaria baada ya Waziri Mkuu wa Serikali ya CCM kwa mara ya kwanza kujiuzuru kutokana na kuhusishwa na kashfa ya ufisadi kupitia kampuni feki iliyokuwa inaitwa Richmond Development Company LLC.
Hii ilikuja baada ya Dk. Harrison Mwakyembe ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati Teule ya Bunge alipoamua kutaja mambo waliyodokezwa kwenye tume na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tanesco, Marehemu Balozi Fulgence Kazaura aliposema Richmond ilikuwa mradi wa Bwana Mkubwa na Mshiriki wake mkubwa kibiashara akimaanisha Edward Lowassa na Rostam Aziz.
Repoti ya Tume ya Bunge kuhusu sakata la Richmond iko HAPA
Baada ya Kamati Teule ya Bunge kusoma taarifa yake tarehe 6 Februari 2008 kuhusu sakata la Richmond Development Company LLC, Edward Lowassa akajikuta akiwa mmoja wa maadui namba wani wa taifa.
Baadaye Februari 5, 2011 kwenye sherehe za miaka 34 ya CCM mjini Dodoma, tukasikia Mwenyekiti wa CCM-Taifa, Rais Jakaya Kikwete akiwaasa wana-CCM kwamba itabidi CCM ijivue gamba.
Tarehe 16 Julai 2011 tulishuhudia Samuel Sitta, Dkt. Harrison Mwakyembe, Nape Nnauye, Lazaro Nyalandu, Ole Sendeka, Prof David Mwakyusa , Asha Abdallah Juma na viongozi wakuu wa CCM Mkoa wa Mbeya wakijitokeza kwenye mkutano wa hadhara mkoani Mbeya katika lengo la kuufikisha ujumbe wa kujivua gamba. Hawa walikuwa vinara wa mapambano yaliyopelekea kujiuzuru kwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na kuwa public enemy number one.
Samuel Sitta, Dkt. Harrison Mwakyembe, Nape Nnauye, Lazaro Nyalandu, Ole Sendeka, Prof David Mwakyusa , Asha Abdallah Juma na viongozi wakuu wa CCM Mkoa wa Mbeya wakielekea kwenye mkutano wa hadhara, Mbeya katika lengo la kuufikisha ujumbe wa kujivua gamba.
Aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Harold Wilson aliwahi kusema, A week is a long time in politics.
Miaka minne baadaye, tunaanza kushuhudia wale waliokuwa wanataka kuwavua magamba kina Edward Lowassa na kundi lake wakiwa katika hati hati ya kuanza kuchekwa na waliokuwa wanawacheka au wako ukingoni kukosa kazi au kufukuzwa ndani ya CCM!.
Vyombo vingi vya vya habari kwa sasa hivi vinawashambulia wapinga rushwa/ufisadi ndani ya CCM kiasi kwamba hata jamii imeanza kununua hoja za vyombo vya habari kwa kuwaona wapinga rushwa/ufisadi kama ni debe tupu. Money talks hasa kwenye jamii yenye ufinyu wa uelewa!
Kuna uwezekano mkubwa wanaojiita CCM Imani/wapinga rushwa/ufisadi ndani ya CCM wako mbioni kufagiwa na kutupwa nje ya CCM na fagio la mafisadi
Wapinga rushwa/ufisadi are about to learn a stern lesson about the vigour of mafisadi!.
Mmarekani aitwaye Jim Henson aliwahi kusema, If you can't beat them. Join them.
Kuna baadhi ya wapinga rushwa na ufisadi wameanza kukubaliana na maneno ya Jim Henson!
Hii ndiyo Tanzania!