kakuruvi
JF-Expert Member
- Sep 2, 2009
- 770
- 256
Wakati umeenda wapi wana JF?
Napata uchungu nikikumbuka raha iliyokuwa inapatikana kwenye michezo wakati ule, nilisoma Tanga na wakati ule tulikuwa na timu mbili daraja la kwanza African Sports (wana Kimanumanu) na Coastal Union (El Mangush) palikuwa hapatoshi hasa watani hawa wa jadi walipokuwa wakikutana.
Nyimbo za vijembe '' KIMANUMANU KINAMANUMANUA AASEGA SEGA KAULEGEZA'' ''KIMBWA KOKO CHATEMBEA NA WAHINDI CHARINGA NINI'' washabiki maarufu akina Bwana Kaka,Power Jabir Kababayee.
Wachezaji kama Twaha Omari, Victor Mkanwa, Mhando Mdeve, Kurwa Shaaban, Yasin Napili, Juma Mgunda, Ali Maumba na wengine wengi, leo hii kumepooza, wanaopajua na waopasikia Tanga nawauliza kunani pale?
Napata uchungu nikikumbuka raha iliyokuwa inapatikana kwenye michezo wakati ule, nilisoma Tanga na wakati ule tulikuwa na timu mbili daraja la kwanza African Sports (wana Kimanumanu) na Coastal Union (El Mangush) palikuwa hapatoshi hasa watani hawa wa jadi walipokuwa wakikutana.
Nyimbo za vijembe '' KIMANUMANU KINAMANUMANUA AASEGA SEGA KAULEGEZA'' ''KIMBWA KOKO CHATEMBEA NA WAHINDI CHARINGA NINI'' washabiki maarufu akina Bwana Kaka,Power Jabir Kababayee.
Wachezaji kama Twaha Omari, Victor Mkanwa, Mhando Mdeve, Kurwa Shaaban, Yasin Napili, Juma Mgunda, Ali Maumba na wengine wengi, leo hii kumepooza, wanaopajua na waopasikia Tanga nawauliza kunani pale?