Ndugu wadau naomba mnishauri nina kesi ya madai ya milioni 10. Je wakili anayenisimamia nitamlipa shilingi ngapi? Au kuna malipo fixed yasiyojali madai ni ya kiasi gani?
Naomba kuelimishwa.
kumbuka unamwajiri wakili akufanyie kazi yako 'kwa uwezo wake wote'. kama akijua hakulipwa vizuri, hatokuwa na morali ya kuifanya kazi yako kwa moyo wake wote. na hapo inaweza kula kwako, manake hutoweza kujua kama kazi yako kaifanya kwa uwezo wake wote au kabangaiza kiaina. vitu vingine ni binafsi na kumlalia mtu kama huyo hakusaidii kesi yako
Ndugu uwakili unaendeshwa kwa sheria na sheria hiyo inatoa nafasi kwa mteja na wakili kukubaliana katika malipo, kuna kesi zinaitwa contentious cases na non-contentious, kwa hii non kuna prescribed scale za kumlipa wakili na kwa kiasi kama chako (kama ni non-contentious) ni asilimia 3% ila wakili abanwi na hii asilimia, na kama ni cont...ni maelewano yako na wakili wako na hii inatofautiana kwa mawakili wote!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.