Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 551
- 1,117
Shida ya umeme ilipofikia sasa mkoa wa mtwara si pazuri, leo ni siku ya nne umeme hauwaki mchana unawaka usiku tu, tena hiyo usiku unaweza kusema labda kaachiwa mtoto achezee kidogo umewaka kidogo umekata ili mradi kero tu, Tulitangaziwa kuwa umeletwa mtambo wa megawati 20 kumaliza tatizo mpka march 30 tatizo lingeisha, kumbe wameenda kuchukua mtambo mbovu wa ubungo wakatuletea sisi tusumbuane nao yaani wanatuchukuliaje? Tunamuomba naibu waziri mkuu na waziri wa nishati kama serikali imeshindwa kutuletea mtambo mpya (maana nasikia kuna mitano imezimwa huko) basi watutafutie mwekezaji wa kuja wekeza huku awauzie umeme tanesco na wala sio jambo la aibu kutafuta muwekezaji ukishindwa jambo bali ndiyo busara,kwasababu wanaoteseka ni wanchi wa hali ya chini wauza juici, waranda mbao, wachomea vyuma, vinyoz na mfano wao unawakatia umeme siku nne unatarajia waishi vipi? gesi tunayo imejaa kuliko maji kwanini tuteseke na umeme watu wa mtwara? Tutafutieni muwekezeji wa kuja kumaliza hii kero jamani kama mumeshindwa kututafutia mtambo mpya musituchulie poa, yaan utafikiri umeme wenyewe wa msaada kumbe tuna nunua nao ila ndio mateso.