Kero ya Kulaza kina mama chini itaisha lini: Aibu!

Ashura9

JF-Expert Member
Oct 21, 2012
739
484
Binafsi nasikitika sana ninavyozidi kusikia kwamba viongozi wengine wenye mamlaka hawawapi kipaumbele kina mama, ambao ni mama zao, wake zao, binti zao, bibi zao, shangazi zao, dada zao, wanawakosea heshima kwa kuwalaza chini sakafuni ni aibu kubwa sana kwa serikali. Pongezi kwa Mh Raisi kwa kuendelea kuliona hili kila wakati lakini jipu ni pale wasaidizi wake wanaposhindwa kulitekeleza na kutafuta mbinu za kuhakikisha hawa kina mama hawadhalilishwi hivyo

Rais Magufuli ametembelea kwa ghafla wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam, na kujionea hali ya msongamano mkubwa wa wazazi uliosababishwa na uhaba wa vitanda na nafasi finyu katika wodi hiyo. Una maana viongozi wengine hawakuona? wakurugenzi muhimbili wanafanya nini? wizara inafanya nini? watendaji wengine wote wanafanya nini? wana haki za kina mama mko wapi kupigania hili?

7.JPG

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametembelea kwa ghafla wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam, na kujionea hali ya msongamano mkubwa wa wazazi uliosababishwa na uhaba wa vitanda na nafasi finyu katika wodi hiyo.

Rais Magufuli aliyekuwa akitoka katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alikokwenda kumuona na kumjulia hali Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubery Bin Ally, amelazimika kwenda katika wodi hiyo baada ya msafara wake kusimamishwa na kundi la akina mama, waliomtaka kwenda katika wodi ya wazazi ili akajionee jinsi wazazi wanavyokabiliwa na kero mbalimbali ikiwemo ya kulala chini kutokana na kukosa vitanda.

Baada ya kujionea mwenyewe kero ya msongamano na kuzungumza baadhi wazazi waliojifungua, Rais Magufuli amewaahidi wazazi hao kuwa atashughulikia kero alizozishuhudia.

"Nimeiona hali halisi mimi mwenyewe, watu wanapata shida, watu wana mateso, na ndio maana nimeamua kuja kwa makusudi, sikuomba ruhusa ili nijionee hali ilivyo, nimejifunza mengi, ninayabeba na nitajua namna ya kuyatatua" Alisema Rais Magufuli.

Kuna haja ya kujadili kwa mapana sana hili jipu wanajamiii....
 
Halafu kuna ma genius watasema ziara za ghafla ni kutafuta umaarufu,hazisaidii.
 
Heading tu nishaanza kufikiria vingine...eti kero ya kulaza kinamama chini.....bila kufafanua kama ni hospitalini

Maana sehemu nyingine kitanda hamna utafanyaje na chini papo
 
serikali ya kisanii @work, walisema vitanda vimenunuliwa kwaiyo Muhimbili kulwaza chini ndoto
 
Mmmmmhh!! Kwaani ziilee peesaa zaa siikuu ileee hazikutosha? Aaama wodi ya kina mama ilisahaulikaa?? Aaiseee!! This is our Tz!! a peaceful land with unpeaceful poor creatures!! Ooohps!
Munkari.... wajuwa Muhimbili kuna Section nyingi na Vitanda vile vilipelekwa sehemu ingine... Hapo kwa akina mama vitaletwa baadae!!
 
Wale jamaa walinyimwa bia na nyama bure tu... Kumbe hata vitanda havikununuliwa vya million hizo 200... Mngesema tu mkwere kakausha hazina
 
serikali ya kisanii @work, walisema vitanda vimenunuliwa kwaiyo Muhimbili kulwaza chini ndoto
"Serikali ya usanii"! Ama kweli unafikira pevu! Ungefafanua. Hata wewe ni sehemu ya serikali, au!

Hapo Muhimbili kuna Mkurugenzi hadi mfagizi na mlinzi hawaoni hiyo hali! Wengi wanaenda pale kama wagonjwa au kuwajulia hali wagonjwa, hawalioni hilo!

Ati " serikali ya kisanii @work! Mh!

TAFAKARI CHUKUA HATUA
 
Ivi ni kweli JPM alikua hajui hili mpaka alipojionea mwenyewe?ivi vile vitanda tulivyoonyeshwa vikifungwa viliishia wapi nilijua kipaumbele wodi ya wazazi,duh bongo movie tupu wallahi
 
Hivi hospitali zingine za manispaa za Dar es Salaam kama Temeke, Amana, Mwananyamala na pia zile za mikoani idadi ya vitanda vilivyopo inakidhi mahitaji au bado ni tatizo? Pamoja na jitihada zinazofanywa na serikali kuhakikisha kwamba Muhimbili wanapata dawa na medical equipment za kutosha itakuwa vizuri hata katika hospitali zingine kubwa kubwa nchini viongozi wakafanya ad hoc visits zitakazopelekea kubaini mapungufu na kuyafanyia kazi.
 
BILA SHAKA MH RAIS ALIPOFIKA MUHIMBILI ALISHANGAA KWA NINI WAGONJWA WANALALA CHIni!!!!!!
 
Mmmmmhh!! Kwaani ziilee peesaa zaa siikuu ileee hazikutosha? Aaama wodi ya kina mama ilisahaulikaa?? Aaiseee!! This is our Tz!! a peaceful land with unpeaceful poor creatures!! Ooohps!
Da Munkari, FYI, wale pale mkusanyiko wa wazazi (wanawake) hao ni wakunyonyesha vichanga .... vilivyolazwa hapo ndo rest room yao !!
Ila Nasikia Raisi JPM ameamrisha jengo la utawala Muhibili kugeuzwa wodi ya wa akina mama Extension (upanuzi zaidi ili ipokee cases za uzazi)..!! atleast anajali hali za akina mama .
 
Binafsi nasikitika sana ninavyozidi kusikia kwamba viongozi wengine wenye mamlaka hawawapi kipaumbele kina mama, ambao ni mama zao, wake zao, binti zao, bibi zao, shangazi zao, dada zao, wanawakosea heshima kwa kuwalaza chini sakafuni ni aibu kubwa sana kwa serikali. Pongezi kwa Mh Raisi kwa kuendelea kuliona hili kila wakati lakini jipu ni pale wasaidizi wake wanaposhindwa kulitekeleza na kutafuta mbinu za kuhakikisha hawa kina mama hawadhalilishwi hivyo

Rais Magufuli ametembelea kwa ghafla wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam, na kujionea hali ya msongamano mkubwa wa wazazi uliosababishwa na uhaba wa vitanda na nafasi finyu katika wodi hiyo. Una maana viongozi wengine hawakuona? wakurugenzi muhimbili wanafanya nini? wizara inafanya nini? watendaji wengine wote wanafanya nini? wana haki za kina mama mko wapi kupigania hili?

7.JPG

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametembelea kwa ghafla wodi ya Wazazi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam, na kujionea hali ya msongamano mkubwa wa wazazi uliosababishwa na uhaba wa vitanda na nafasi finyu katika wodi hiyo.

Rais Magufuli aliyekuwa akitoka katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alikokwenda kumuona na kumjulia hali Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubery Bin Ally, amelazimika kwenda katika wodi hiyo baada ya msafara wake kusimamishwa na kundi la akina mama, waliomtaka kwenda katika wodi ya wazazi ili akajionee jinsi wazazi wanavyokabiliwa na kero mbalimbali ikiwemo ya kulala chini kutokana na kukosa vitanda.

Baada ya kujionea mwenyewe kero ya msongamano na kuzungumza baadhi wazazi waliojifungua, Rais Magufuli amewaahidi wazazi hao kuwa atashughulikia kero alizozishuhudia.

"Nimeiona hali halisi mimi mwenyewe, watu wanapata shida, watu wana mateso, na ndio maana nimeamua kuja kwa makusudi, sikuomba ruhusa ili nijionee hali ilivyo, nimejifunza mengi, ninayabeba na nitajua namna ya kuyatatua" Alisema Rais Magufuli.

Kuna haja ya kujadili kwa mapana sana hili jipu wanajamiii....
Kwani tatizo hilo bado lipo? Si mlisambaza picha za paka kulalia vitanda mkasema havina wagonjwa? Sasa lipi la kweli?
 
Inaelekea pale Muhimbili pana zaidi ya usanii.Kwani mh.raid hakumbuki kuwa kuna hela yeye mwenyewe alitenga kwa ajili kununulia vifaa hapo Muhimbili?Hii ni awamu ya(kwanza) ya wasanii....ukiwa muongo usiwe msahaulifu.
 
Back
Top Bottom