Katibu wa CHADEMA Kilimanjaro Akalishwa chini katika Kongamano Moshi

Huu ni upuuzi na ujinga wa kupitiliza, hizi sherehe za miaka 50 ya uhuru kwanini tuongelee mafanikio? Ingekuwa jambo la busara kuongelea changamoto na wapi tumeshindwa na tufanyeje kwa miaka 20-50 ijayo. Hii tabia ya kutaka kusifiwa niya kijinga naniya viongozi wasiopenda kuwajibika. Kama serikali imejenga barabara hakuna maana ya kuongea manake wananchi wataona na kusema, kama kuna maji yanayotoka bombani 24/7 kwanini uongee na kuomba kusifiwa wakati hali halisi inaonekana? Tuache sifa zisizokuwa na msaada. Hakuna kiongozi yoyote anayestaili sifa, manake ni wajibu wake kutekeleza na aliomba kazi ya kuwatumikia wananchi kwa hiari yake mwenyewe, sasa akifanya alichoomba anaitaji sifa za nini? Wananchi tunalipa kodi kwa Serikali ili watimize wajibu wao kwetu, kwanini viongozi hawawasifii wananchi kila siku kwa kulipa kodi na wao wanazitafuna bila mpango?
 
NITAKUWA FAIR MEMA YA SERIKALI ILIYOTUFANYIA KWA MIAKA 50 NI HAYA:

Serikali kwa miaka 50 imeweza kuleta umeme usio wa uhakika kwa asimilia 12 ya watanzania wote na asilimia 88 wanalala gizani.

serikali yetu kwa miaka imeweza kuleta maji ya bomba kwa asimilia 14% ya watanzania wote asimilia 86 wanakunywa maji ya bwawani.

imeweza kutujengea shule za kata ambazo hazina maabara, vitabu wala waalimu ambapo asimilia zaidi ya 80 wanatoka na division zero.

serikali ktk miaka 50 wameweza kujenga asilimia 10 ya barabara za nchi nzima na asilimia 90 ya barabara zote ni mavumbi hayo ni machache ya
mafaniko makubwa ya miaka 50 ya uhuru.

Add to the list>>>
Imesaidia kujenga uchumi wa nchi kwa wachache (5%) huku wengi wakiendelea kula mlo mmoja kwa siku.

Imefanikisha kujenga wakoloni wanoishi nchini (wawekezaji) wanaoweza kuiloromea serikali na hata kuipa siku 24 na yenyewe ikafyata mkia
 
Leo kulifanyika Kongamano kubwa lililoitishwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjro Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo. Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa YMCA lilihudhuriwa na Wakuu wote wa Wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro, Viongozi na watumishi wote wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri zote, madiwani wote walimu kadhaa wa shule za msingi na za sekondari mjini Moshi, wanafunzi kadha wa shule za msingi na za sekondari, viongozi wa vyama vya siasa pamoja na viongozi wa madhehebu ya dini.

Baada ya mada kutolewa uwanja uliwekwa wazi kwa ajili ya waalikwa kuchangia katika mada kuu " MIAKA 50 YA UHURU NA CHANGAMOTO ZAKE" Katika hali ya kutatanisha Katibu wa CHADEMA mkoa wa Kilimanjaro Ndg. Basil Lema alipata nafasi ya kuchangia akiwa mtu wa tano. Baada tu ya kujitambulisha mic ilizimika ikabidi aende hadi mbele kabisa akachukua mic ya RC. Ilimchukua pungufu ya dk 1 kuanzisha hoja yake kuhusu uhuru na maendeleo ndipo ghafla RC Kalembo akasimama akasema hajatoa nafasi za watu kuhutubia. Mshereheshaji alichukua mic kutoka mkononi kwa Lema na kuita mchangiaji mwingine.


Lema alirudi kwenye kiti chake kwa aibu na kuonekana wazi kuwa amechemka na aibu zimemjaa usoni. Hii ni matokeo ya kutaka kuchafua hali ya hewa kwenye ukumbi kwa vijembe vya siasa. Inashangaza kuwa kuna watu hawaoni maendeleo ambayo Tanzania imepiga kwa miaka hii 50 ya uhuru.
Alikalishwa chini?Kwa kuambiwa akae ama alikwenda mwenyewe kukaa kama ulivyosema?
Maoni yako kuhsu tukio hilo ni wrong.Sioni sababu yoyote ya kusema aliona aibu.Miaka hamsini ya uhuru ni mingi lakini pia ni michache depending on what you are trying to compare with or explain.
Angeachiwa atoe maoni yake,ndiyo demokrasia hiyo.Miaka 50 ya uhuru ni kwa watanzania wote bila kujali vyama.Na ni wazi si wakati wa chama kimoja na hivyo watu wana haki ya kuwa na mawazo ya tofauti kuhusiana na hatua tulizopiga ama kurudi nyuma tokea tupate uhuru.Can we really be proud on where we are right now?Umeridhika?
 
nadhani mafanikio ni hya ya 50 za uhuru,1. kununua magari ya kifahari kwa kila kiongozi wa juu.2. kurithisha mashamba kwa viongozi,3. kugawana nyumba za serikali,4. kuuza mali asili za nchiniendeleee?
 
Back
Top Bottom