Katibu mkuu wa CCM, ndugu Bashiru Ally acha kudanganya watanzania sio wajinga

Tairi bovu

JF-Expert Member
Sep 28, 2017
3,063
2,983
Nilifuatilia kwa kina mazungumzo yako na ndugu Tido Mhando hapo jana kupitia Azam tv hakika umedanganya na kujichanganya sana. inatia shaka hata kukuita dr. hasa ikizingatiwa kwamba wewe ni mwalimu wangu najisikia vibaya

1. Uliulizwa juu ya kusimamishwa shughuli za kisiasa ambazo zipo kisheria. ukasema zinaruhusiwa kwa wabunge na viongozi kwenye maeneo yao nawewe unafanya kwasababu unatembelea wanachama nchi nzima kwakuwa ni mpya. Sawa, mbona Maalim Seif ni mwanachama mpya wa ACT amekatazwa kufanya hivyo? mbona mashinji haruhusiwi kufanya kama ufanyavyo wewe? mbona makene haruhusiwi polepole anaruhusiwa?

2. Uliulizwa kuhusu hamahama ya wabunge kuja ccm na kwann wanagombea maeneo yaleyale na kwamba ndio utaratibu wa chama? Ukajibu kwamba ndio utaratibu na kwamba hakuna haja ya kura za maoni. Ukatolea mfano jimbo la Korogwe kwamba alichukuliwa watatu. Ulisema wanaomba kwanza kujiunga na chama kwenye matawi. Sio kweli hata kidogo. Ushahidi upo kwamba mh GEKULI na yule wa Serengeti hata maudhui ya barua zao yalishabihiana pakubwa waliomba uanachama wapi, lini na walikubaliwa wapi na lini na wakajiunga na chama lini?

3. Uliulizwa kuhusu Lowassa kurudi CCM. Ukajibu kwamba aliomba kupitia kwenye tawi huko Monduli na mlimkubalia kupitia vikao vya chama na wakati wa kujiunga alisindikizwa na mwandani wake bwana Rostam Azizi. Ukweli ni kwamba Lowassa alijiunga na CCM kwanza na kadi alienda kuchukua baadae kule Monduli ushahidi upo

4. Uliulizwa juu ya dhamira ya kupambana na rushwa na kwannini ripoti ya tume yako imekuwa siri kama ya maiti na kaburi. ukadai uliwasilisha kwenye vikao vya chama kwa masaa manne na dk 20. Ukweli ni kwa mapendekezo ya ile tume hayajawahi kutekelezwa popote na kwamba chama chako hakina nia ya dhati ya kupambana na rushwa nakupa mfano.. kwenye uchaguzi wa marudio kule Ukonga wapiga kura walipewa kati ya 100000 na 20000 ili wasipige kura wewe ulikuwepo na uliona hilo lipo wazi kabisa. Kinondoni watu walikimbia mpaka na mabox tena askari uliona na kushuhudia.

5. Uliulizwa kuhusu kuongeza muda wa kutawala kwa magufuli na msimamo wako ukajibu kuwa hataongeza muda .. ukweli ni kwamba Juma Nkamia sio mjinga na hajaamka na kuota alitumwa na mwenyekiti na baada ya kuona haiwezekani akaondoa hoja mezani.
6.uliulizwa juu ya wabunge machachari wanaoenda kinyume na misimamo ya chama wakitajwa kina nape, ukasema kwakuwa hawajapitia kwenye vyuo vya chama. wewe ulipita chuo gani cha chama ndugu Bashiru? mbona hujamtaja bwana polepole anayewatukana mpaka wabunge wenzie wa upinzani? anasema wamepatikana kwa kutoa ngono? mbona husemi Anna kilango malecela na anna Abdalla kutaja wachache walipatikanaje?

Hitimisho:

Nitaendelea kuamini kwamba serikali ya CCM ndiyo inayohusika na jaribio la kumuua Mh. Tundu Lissu na bunge ni dhaifu kwa viwango vyovyote vile... tangu lini mtu msafi akaogopa kukaguliwa?
 
Jana nimeangalia yale mahojiano,wanaosemaga ukihamia kile chama akili na ubongo vinabadilishwa wanahoja!!!

Inakera na kuskitisha mtu msomi anapoamua kujitoa ufahamu na kutetea uozo,haswa alipokuwa akitetea kuwa CCM haibebwi na NEC na vyombo vya dola,uhalali wa marufuku ya wapinzani kuzuiwa kufanya mikutano huku CCM wakifanya,uvunjaji wa kanuni na taratibu za uteuzi wa wagombea kwa wabunge wanaohamia CCM toka upinzani etc.

Itoshe tu kusema kwa unafiki-miafrika ndivyo tulivyo,Bashiru wa UDSM sio huyu wa Lumumba, wanafanana sauti na mavazi tu!!
 
Ccm imekosa watu makini na hili ni anguko lao japo wanahisi wapo sahihi ila wao ni kama kimbunga kilichokosa mwelekeo na watu wanajua ni wapi wataepukia licha ya kila kitu kutawaliwa na wao
 
1. Ndugu Bashiru yupo sahihi kwa maana ya kwamba Kiongozi lazima atambulike na anaowangoza na serikali yake. Yeye kama kiongozi wa chama kilichoshika madaraka lazima ajulikane vema kwa viongozi wa serikali na anazunguka kufanya tathmini wa utekelezaji wa ilani , bila hivyo chama kitashindwa kuisimamia Serikali ipasavyo.

2. Bashiru sio mwenye maamuzi ndani ya CCM, ni vikao vya chama ndio vinaamua utekelezaji na uwajibikaji na kama kikao hakijaketi maana bado kuna uchunguzi wa kina unafanyika ili kikao kiketi na waliofanya hivyo wawajibike. tusimlaumu Magufuli na bashiru kwa kuwa utaratibu wankufanya hivyo upo na wenyewe hawawezi kwenda kinyume.

3. kama nimemuelewa vizuri katibu mkuu ni kwamba, hata kama kungekuwa na kura za maoni uwezekano wa huyo mtu kuchaguliwa tena ni mkubwa sana hivyo ni vema kufupisha zoezi hilo kuepusha mambo ambayo yanaweza kujitokeza kama rushw. CCM imekuwa mpya kwa maana ya kwamba , chaguo la watu ndio chaguo la chama na kama mtu alichaguliwa ubunge na watu basi watu hao watamchagua kirahisi kuliko mpya.

4. Ndugu Bashiru anaujua utaratibu ndani ya chama ulivyo mgumu hasa wa kufanya maamuzi ambao unahitaji makubaliano ya pamoja kupitia vikao rasmi. kwa kuliona kama mtendaji mkuu wa chama , ameona kuongeza muda ni ngumu sana.

5. unless uwe unahusika na mipango ya Lowassa ndio tuamini hiki usemacho. Lowasa sio mgeni juu ya taratibu za kurudi upya ndani ya CCM , hivyo atakuwa kazifuata na kukubaliwa toka kwenye tawi lako.
 
Yani hapo ujamtetea hata kidogo,unataka unacho fikiria wewe ndio iwe katiba ya CCM.
 
Bashiri atakwambia hiyo ndio siasa.

Na kuhusu Tido, hayo maswali yake ndio humgharimu lakini naona hajajifunza bado.
 
1. Ndugu Bashiru yupo sahihi kwa maana ya kwamba Kiongozi lazima atambulike na anaowangoza na serikali yake. Yeye kama kiongozi wa chama kilichoshika madaraka lazima ajulikane vema kwa viongozi wa serikali na anazunguka kufanya tathmini wa utekelezaji wa ilani , bila hivyo chama kitashindwa kuisimamia Serikali ipasavyo.

2. Bashiru sio mwenye maamuzi ndani ya CCM, ni vikao vya chama ndio vinaamua utekelezaji na uwajibikaji na kama kikao hakijaketi maana bado kuna uchunguzi wa kina unafanyika ili kikao kiketi na waliofanya hivyo wawajibike. tusimlaumu Magufuli na bashiru kwa kuwa utaratibu wankufanya hivyo upo na wenyewe hawawezi kwenda kinyume.

3. kama nimemuelewa vizuri katibu mkuu ni kwamba, hata kama kungekuwa na kura za maoni uwezekano wa huyo mtu kuchaguliwa tena ni mkubwa sana hivyo ni vema kufupisha zoezi hilo kuepusha mambo ambayo yanaweza kujitokeza kama rushw. CCM imekuwa mpya kwa maana ya kwamba , chaguo la watu ndio chaguo la chama na kama mtu alichaguliwa ubunge na watu basi watu hao watamchagua kirahisi kuliko mpya.

4. Ndugu Bashiru anaujua utaratibu ndani ya chama ulivyo mgumu hasa wa kufanya maamuzi ambao unahitaji makubaliano ya pamoja kupitia vikao rasmi. kwa kuliona kama mtendaji mkuu wa chama , ameona kuongeza muda ni ngumu sana.

5. unless uwe unahusika na mipango ya Lowassa ndio tuamini hiki usemacho. Lowasa sio mgeni juu ya taratibu za kurudi upya ndani ya CCM , hivyo atakuwa kazifuata na kukubaliwa toka kwenye tawi lako.
mwita ni mwanachama wa tawi gani? aliomba lini? alikubaliwa lini na alitangaza lini kuhama
 
haahaa bashiru toka alambishwe hana jipya. mapovu mengi kutetea ugali lakini hakuna jpya
 
Kama nitafanikiwa kuona chama kingine kinapata fursa ya kuongoza nchi nitavaa suti wakati wote. sitatembea uchi!
 
Hv Bar she ru alianza lini kuwa mwanasisiem? Au alipata uanachama papo hapo akapewa na u KM? muda mwingi alikuwa mtumishi wa umma mwenye kujua tafadhari
 
Back
Top Bottom