Aloysius
Member
- Mar 1, 2011
- 80
- 9
Hivi mnahabari kuwa pengine hizi kelele za kubadili katiba zinabarikiwa na Wazungu?!!! Vijana tufumbue macho, historia inamueleza mzungu kama mtu wa uchu wakututawala toka enzi kiakili na kwa kila kitu. Ona anachofanya Libya, Ivory Cost, Sudan, Somalia n.k. Kenya ni mfano mdogo; swala la "abortion" lilipenyezwa kwenye katiba pindi tu ilipobadilika ikawaacha wakenya hata wale waliotaka ibadilike midomo wazi, mpaka wakujiuliza hili ni la nani, kura ilikuwa yakusema ndio au hapana. Wakaipitisha kwakuadiwa mabadiliko yatafanyika. Je yamefanywa? Kwetu nini kitapenyezwa?!!!