Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
Wana JF kuna sakata hapa Kenya ambapo Naibu Jaji Mkuu anatuhumiwa kumdhalilisha mfanyakazi mmoja kweny mall. Polisi wamependekeza D-CJ Ms. Nancy Baraza ashitakiwe na Mwendesha Mashitaka wa Serikali Bw. Kiriako Tobiko anasema kesho atatoa uamuzi kama Nancy Baraza afunguliwe mashtaka ama la. Mambo yote yanafanyika kwa uwazi sana. Nakimbuka kuna sakata ya Jaji Rugazia ambaye alisababisha ajali lakini sijui mwisho wake ulikuwa nini, mambo yamekuwa yakienda kimyakimya.
Wenzenu Wakenya wanafurahia katiba mpya mambo yote hadharani hakuna kuoneana aibu. Kama imechemka inachanwa live.
Jamani Katiba mpya utatulete ukombozi.
Wenzenu Wakenya wanafurahia katiba mpya mambo yote hadharani hakuna kuoneana aibu. Kama imechemka inachanwa live.
Jamani Katiba mpya utatulete ukombozi.