Kashifa ya wizi tbs ni aibu kwa taifa,serikali,na wizara husika

princes

Member
Sep 10, 2008
29
5
Ni siku kadhaa katika kufuatilia yanayojiri nchini,vyombo vya habari,baadhi ya viongozi
na baadhi ya kamati za bunge kwa kuonesha bidii katika kazi na uzalendo wa hali ya juu
kudhibitisha kasi zaidi.
La muhimu ni hii habari inayogonga vichwa vya habari magazetini,katika Jahazi clouds fm,10 za amplifier,
na Tv.
Ni vema tukaliangalia uzito wake na likashughulikiwa kwa kina ,Kashfa hii inayomuhusisha mkurugenzi wa Shirika la Udhibiti
wa viwango TZ -TBS Bw.Charles Ekerege,inaonesha wizi na ubadhilifu mkubwa ukiambatana na hujuma za mapato ya
kodi za viwango,kama Kamati imefika huko Hongkong na kwingine na wakadhibitisha ubadhilifu na udanganyifu
wa mabilioni ya mapato ya nchi kwa miaka kadhaa na kama ,kila gari inayopita toka huko inaonesha imegongwa muhuri
wa udhibitisho na kuingia nchini inamaana imeiingizia TZ,si chini ya laki na ushehe na leo ni magari mangapi? na miaka mingapi
imepita tangu wameanzakuweka pesa hizo kapuni kwao,ambazo hadi leo hzijulikani zilipita wapi na magari yalipita ila pesa nehii!!!
Huu ni unafiki mkubwa kwa mapato ya serikali na aibu kwa nchi,kama sekta nyeti hizo zitafumbiwa macho na kutowawajibisha
watu kama huyu mkurugenzi wa TBS,Leo hii nitashangaa kumuwajibisha mwalimu mkuu kwa kula fedha za miradi ya madarasa na vitabu vya watoto .
Tafadhali hili si suala la kufumbia macho najua ,kipindi hiki atatoa pesa nyingi ili kuua soo ,ni vema tukawek maslahi ya Taifa mbele.Kwa hiyo kwa kuwa ameitwa nahiyo kamati kukutana Dodoma na Mh .W/mkuu.tunomba waandishi wa habari tushiriki
katika hili kwa kuwa Hayo magari yasiyo na viwango na bidhaa zinazoingia kwa mtindo huo wa TBS tutapunguza ajali na magonjwa yanoyotokana na ubovu wa bidhaa.?
Maisha bora kwa wizi na udanganyifu kwa taifa??
Nawasilishaa.
 
Back
Top Bottom