Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
Dk Slaa amshukia mama Anna Mkapa
Aidha, Dk Slaa alisema serikali kwa kujua iliamua kwa makusudi kumuuziauza kiwanda pekee cha korosho kilichopo mkoani Mtwara kwa sh. milioni 50 na kuwaacha wakazi wa mtwara wakihangaika na korosho zao pasipo kujua ni wapi watazipeleka.
Alisema kama kiwanda hicho kingeachwa wakazi wa Mtwara wasingekuwa na taabu ya kujua ni wapi pa kupeleka korosho zao. Taarifa nilizonazo kiwanda hicho alichouziwa mama Mkapa kimeondolewa mitambo yote na sasa kimebaki tupu na hakuna kinachoendelea juu ya hilo huku ninyi mkibaki na umasikini wenualisema Dk Slaa