Seneta mmoja nchini Ufaransa ametaka aliyekuwa Mchezaji wa Timu ya Real Madrid, Karim Benzema, apokonywe uraia baada ya kutuhumiwa kujihusisha na kikundi cha kigaidi cha Muslim Brotherhood kutoka nchini Misri.
====
Kufuatia tuhuma za Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa, Gerald Darmanin, kuwa Karim Benzema “ana uhusiano” na kundi la kigaidi la Muslim Brotherhood, Seneta wa Ufaransa Valerie Boyer, ameibuka na kutoa kauli tata dhidi ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Real Madrid.
Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, Seneta huyo ametaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya Benzema, ikiwa tuhuma za kujihusisha na kundi la “Muslim Brotherhood” kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Ndani zitathibitishwa.
Kwenye taarifa hiyo, Seneta Boyer alisema, “Kama kauli za Waziri wa Mambo ya Ndani ni kweli, lazima Karim Benzema awekewe vikwazo”.
“Kwanza Benzema apokonywe tuzo yake ya Ballon d’Or, lakini pia, ni lazima mchezaji huyo avuliwe uraia wa Ufaransa. Hatuwezi kukubali Mfaransa mwenye uraia pacha, na kujulikana kimataifa, atuvunjie heshima na kuisaliti nchi yake kwa kiasi hiki.”
Mijadala na tuhama hizo imeibuka baada ya Benzema kukaa kimya juu shambulio la kigaidi lililohisisha mauaji ya mwalimu wa Kifaransa nje kidogo ya jiji la Paris, huku siku chache baada ya tukio hilo, mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid akitumia kurasa zake za kijamii, kupelekea salamu za pole na kuomba haki itendeke kwa Taifa la Palestina.
Sns
====
Kufuatia tuhuma za Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa, Gerald Darmanin, kuwa Karim Benzema “ana uhusiano” na kundi la kigaidi la Muslim Brotherhood, Seneta wa Ufaransa Valerie Boyer, ameibuka na kutoa kauli tata dhidi ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Real Madrid.
Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, Seneta huyo ametaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya Benzema, ikiwa tuhuma za kujihusisha na kundi la “Muslim Brotherhood” kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Ndani zitathibitishwa.
Kwenye taarifa hiyo, Seneta Boyer alisema, “Kama kauli za Waziri wa Mambo ya Ndani ni kweli, lazima Karim Benzema awekewe vikwazo”.
“Kwanza Benzema apokonywe tuzo yake ya Ballon d’Or, lakini pia, ni lazima mchezaji huyo avuliwe uraia wa Ufaransa. Hatuwezi kukubali Mfaransa mwenye uraia pacha, na kujulikana kimataifa, atuvunjie heshima na kuisaliti nchi yake kwa kiasi hiki.”
Mijadala na tuhama hizo imeibuka baada ya Benzema kukaa kimya juu shambulio la kigaidi lililohisisha mauaji ya mwalimu wa Kifaransa nje kidogo ya jiji la Paris, huku siku chache baada ya tukio hilo, mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid akitumia kurasa zake za kijamii, kupelekea salamu za pole na kuomba haki itendeke kwa Taifa la Palestina.
Sns