Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa mjibizo kwa shambulio lililofanywa na utawala haramu wa Kizayuni dhidi ya Hospitali ya Watoto ya Al-Nasr huko Gaza, na kueleza kwamba: "watoto wa Kipalestina daima wamekuwa ni jinamizi kwa Wazayuni."
Kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim; Nasser Kanani amelaani shambulio la kinyama la utawala wa Kizayuni dhidi ya Hospitali ya Watoto ya Al-Nasr katika Ukanda wa Gaza na kusema: watoto wa Kipalestina wanajifunza alfabeti za maneno ya subira, ushujaa, muqawama na kuuawa shahidi kwa ajili ya ukombozi wa Palestina kuanzia siku za mwanzo za kuzaliwa kwao katika madrasa za mama zao, baba na kaka zao na dada zao na hilo ndilo jinamizi la kudumu linalowaandama Wazayuni.
Kanani amesisitiza kuwa: Wazayuni wanadhani kwamba ikiwa watawachinja watoto wote wa Gaza, watakuwa wameshawafuta tokea leo kwenye mbeleko za mama zao wapiganaji na wanajihadi wa kesho wa Palestina, ilhali kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, mama wa Kipalestina atamkabidhi kwa mara nyingine mtoto wake kwa mkondo wa maji ili muda si mrefu wa kesho ijayo aje kuuanganmiza utawala usio na mashiko wa Mafirauni wa Kizayuni.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim; Nasser Kanani amelaani shambulio la kinyama la utawala wa Kizayuni dhidi ya Hospitali ya Watoto ya Al-Nasr katika Ukanda wa Gaza na kusema: watoto wa Kipalestina wanajifunza alfabeti za maneno ya subira, ushujaa, muqawama na kuuawa shahidi kwa ajili ya ukombozi wa Palestina kuanzia siku za mwanzo za kuzaliwa kwao katika madrasa za mama zao, baba na kaka zao na dada zao na hilo ndilo jinamizi la kudumu linalowaandama Wazayuni.
Kanani amesisitiza kuwa: Wazayuni wanadhani kwamba ikiwa watawachinja watoto wote wa Gaza, watakuwa wameshawafuta tokea leo kwenye mbeleko za mama zao wapiganaji na wanajihadi wa kesho wa Palestina, ilhali kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, mama wa Kipalestina atamkabidhi kwa mara nyingine mtoto wake kwa mkondo wa maji ili muda si mrefu wa kesho ijayo aje kuuanganmiza utawala usio na mashiko wa Mafirauni wa Kizayuni.