Kampuni ya Barrick Gold kununua hisa za Acacia ili kuweza Kutekeleza makubaliano na Serikali ya Tanzania

Shigganza

Senior Member
May 24, 2018
160
412
Kampuni ya uchimbaji madini ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mwekezaji katika Migodi ya Bulyanhulu na North Mara kwa Ubia na Accacia imetangaza nia ya kununua hisa za kampuni ya Acacia kwa gharama ya dola za Marekani milioni 787.

Uamuzi wa Barrick unafuatia kampuni ya Acacia kutotoa ushirikiano kwa Barrick dhidi ya makubaliano ambayo imeafikiana na Serikali ya Tanzania kupitia kamati za majadiliano. Kutokana na kukosekana kwa ushirikiano huo, Barrick ambayo inamiliki kiwango kikubwa cha hisa ambacho ni theluthi mbili imeamua kununua hisa zote za Acacia ili kuiwezesha kuwa na umiliki kamili wa Migodi hiyo.

NIni kitatokea baada ya Barrick kununua hisa za Acacia? ni wazi kuwa kampuni ya Barrick itaweza kutekeleza makubaliano iliyoingia na Serikali ya Tanzania mara moja kwani kwa muda huu wote Acacia imekuwa kikwazo kikubwa.

Kwa minajili ya rejea tembelea https://www.miningweekly.com/articl...tanzania-refuses-direct-settlement-2019-05-22
 
Kama theluthi moja ya thamani nzima ya Acacia ni dola million 285 maana yake thamani halisi ya Acacia ni around dula milion 855 ...Swali is kujiuliza ni je, kwa thamani hii ya kampuni kwa maana ya jumla ya mtaji na assets n.k ina uwezo wa kulipa deni tunalowadai?
 
Kama theluthi moja ya thamani nzima ya Acacia ni dola million 285 maana yake thamani halisi ya Acacia ni around dula milion 855 ...Swali is kujiuliza ni je, kwa thamani hii ya kampuni kwa maana ya jumla ya mtaji na assets n.k ina uwezo wa kulipa deni tunalowadai?
Ndio dola milioni 300, ujue pia wanafaida ambay sio sehem ya mtaji!
 
Hii ni habari njema , tutabaki mezani na mwenye mbwa na si mlisha mbwa.
 
Hapa kuna kinachoendelea ambacho kitakuja kujilikana baadae ila wajinga wa Lumumba hawawezi kuliona hili!!

Ni hawa hawa Barrick tuliaminishwa kuwa walikuwa na sauti juu ya Accasia na watu wakajawa na matumaini kuwa tutalipwa ila hakuna walichofanya kuonyesha kuwa wana sauti juu ya Accasia katika hii issue na mpaka sasa dandana zinaendelea.

Tuendelee kusbiri na hatima ya jambo hili.
 
Hapa kuna kinachoendelea ambacho kitakuja kujilikana baadae ila wajinga wa Lumumba hawawezi kuliona hili!!

Ni hawa hawa Barrick tuliaminishwa kuwa walikuwa na sauti juu ya Accasia na watu wakajawa na matumaini kuwa tutalipwa ila hakuna walichofanya kuonyesha kuwa wana sauti juu ya Accasia katika hii issue na mpaka sasa dandana zinaendelea.

Tuendelee kusbiri na hatima ya jambo hili.
Ndiyo maana majimbo yote yanayoongozwa na Chadema umejaa ujinga ,roho za korosho ,ushirikina na uchawi.
 
Nadhan kama taifa tunapaswa kudai chetu, maadam tumeshajiridhisha past na shaka walituibia basi
 
Kamanda kilizi unaendelea kuumia
Wajinga wanaendelea kudanganywa na wanafurahia.

Mwanzoni mliaminishwa kuwa Barrick wana sauti juu ya Barrik kwasababu wana hisa nyingi kwahiyo mkawa na matumaini ila hakuna kilichotokea.Leo mmepata hii taarifa mmeanza kushangiliaa wakati hamjui nini kitakuwa hatima ya mlichokuwa mnawadai hao Accasia wakati Barrick wenyewe walikubali tu kulipa hiyo dola milioni 300 na sio deni lote alafu leo ndio mtarajie wajitwike huo mzigo wa hiyo kodi isioelezeka wakati kwenye mazungumzo walijitahidi kuwasaidiac wenzao wasilipe kwa kuona ni deni lilisolo na logic!!
 
Back
Top Bottom