one activist
Senior Member
- Oct 13, 2012
- 114
- 14
Katika mkutano wao wa kwanza uliofanyika maeneo ya Kamficheni walipika wali na nyama kitu kilichofanya watu waliohudhuria mkutano wa chadema katika eneo la Maendeleo kuondoka mkutanoni kuwahi sahani huko, na leo katika mkutano ulioanza hivi punde magari yaliyojaza watu kutoka Uyole, Utengule na sehemu mbalimbali za nje ya Halmashauri ya jiji la Mbeya yamebeba watu na kuwarundika katika mkutano utakaofanyika Pambogo na kuhutubiwa na akina Mwigulu, Mwampamba, katibu muenezi Mbuzax nk.Hawa watu waliokula huo wali umeishia matumboni na kamwe hauwezi ukabadilisha misimamo yao mioyoni, namna hii inaonyesha ni kwa jinsi gani CCM zama zao zimefika ukingoni.