BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
Kauli hiyo imetolewa na David Mathayo mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, katika ziara yao ya kutembelea vituo vya kuzalisha umeme mkoani Tanga, ambapo amewahakikishia watanzania kuwa hakutakuwa na mgao wa umeme ifikapo mwezi April 2024.
Naye mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi TANESCO, Balozi Meja Jenerali, Paul Kisesa Simuli amewataka wawekezaji kujipanga kuzalisha bidhaa kwa wingi utokana na serikali kujidhatiti kuhakikisha suala la mgao wa umeme linabaki kuwa historia.