Kama tunaweza kuwalipa waliofukuzwa kazi kwa kuwa na vyeti feki, basi tuwalipe na wazee wetu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki stahiki zao

St. Paka Mweusi

JF-Expert Member
Sep 3, 2010
7,639
4,526
Natanguliza salamu,
Jumuiya ya Afrika ya Mashariki iliundwa mwaka 1967 na kuvunjika mwaka 1977. Baada ya kuvunjika Jumuiya hii, Serikali ya Uingereza ilitoa fedha kwa ajili ya kuwalipa pensheni zao wafanyakazi wa iliyokuwa Jumuiya hiyo. Wafanyakazi wa Kenya na Uganda walilipwa pesa zao.

Hapa kwetu Tanzania ambapo Ujamaa ulikuwa umeshika hatamu ilionekana kuwa kuwalipa wafanyakazi hao fedha hizo zitakuwa ni nyingi sana, hivyo Serikali chini ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikaamua kuzipangia pesa hizo matumizi mengine. Ikawa imeisha.

Kufikia mwishoni mwa miaka ya 90 yakaanza majadiliano ya kuunda upya Jumuiya hiyo, changamoto ikawa Tanzania na wafanyakazi wake ambao hawakulipwa stahiki zao. Makubaliano yakawa wafanyakazi hao walipwe kwanza ndiyo Jumuiya mpya ianzishwe. Kweli mchakato ulifanyika wakalipwa stahiki zao.

Cha kusikitisha ni kuwa wafanyakazi hawa walilipwa malipo waliyostahili kulipwa mwaka 1977. Serikali yetu haikujali mfumuko wa bei wala kushuka kwa thamani ya Pesa.

Unakuta mtu alilipwa 400,000/= mwaka 1999, lakini kiuhalisia thamani ya pesa hiyo haipo sawa na 400,000/= ya 1977. Laki nne ya 1977 mtu angeweza kununua nyumba nne Ilala, lakini laki nne ya 1999 mtu huyo angeweza kujenga nyumba Tegeta?

Haki iliyocheleweshwa ni haki iliyodhulumiwa, wazee hawa walidhulumiwa stahiki zao. Sasa basi tunaiomba Serikali yetu inayojali watu wake iwatazame wazee wetu hawa na kuwalipa stahiki zao kwa kuzingatia mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya pesa.

Wote wenye vyeti feki na wastaafu wa EAC walikuwa watumishi, japo hawa wenye vyeti feki walighushi vyeti ili kupata ajira isivyo halali. Kwa mtazamo wangu wanaostahili malipo stahiki kati ya makundi haya mawili ni wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Tushirikiane kupaza sauti ili wazee wetu hawa wapate stahiki zao.

Laana zingine hawa tunajitafutia wenyewe kwa dhulma zetu.

Naomba kutoa hoja.
 
Uzi huu naomba usomeke na kilio Cha sisi watu wa Mbezi Kibamba tuliodhulumiwa kwa kuvunjiwa nyumba zetu bila fidia, halafu eneo zilipovunjwa nyumba bado liko wazi.
Tunatanguliza shukrani.
 
Ila nasikia wapo walio lipwa
Walilipwa kiwango walichotakiwa kulipwa mwaka 1977.. Kilio Chao ni kulipwa kwa kuzingatia kushuka kwa thamani ya pesa na mfumuko wa bei.. Nimetoa mfano hapo juu.. Unakuta mtu alitakiwa kulipwa laki mbili wakati huo ambapo mshahara wa mfanyakazi ulikuwa Tshs 600 kwa mwezi.. Laki mbili hiyo anakuja kulipwa 2002 ambapo mshahara wa mfanyakazi wa kawaida ni laki moja kwa mwezi.. Hiyo si ni dhulma dhidi yao..??
 
Jumuia ilivyo vunjika si kila nchi ilipata share yake Kwa ajili ya kuwalipa wafanyakazi stahiki zao.

Je nchi nyingine ei Kenya, Uganda wao bado wanadaiwa na wastaafu wao au VP?

Je NI Kwa NN wanaaendelea na jumuia wakati kuna malalamiko ya wastaafu.
Serikali lipeni watu stahiki zao acheni uwizi
 
Jumuia ilivyo vunjika si kila nchi ilipata share yake Kwa ajili ya kuwalipa wafanyakazi stahiki zao.

Je nchi nyingine ei Kenya, Uganda wao bado wanadaiwa na wastaafu wao au VP?

Je NI Kwa NN wanaaendelea na jumuia wakati kuna malalamiko ya wastaafu.
Serikali lipeni watu stahiki zao acheni uwizi
 
Jumuia ilivyo vunjika si kila nchi ilipata share yake Kwa ajili ya kuwalipa wafanyakazi stahiki zao.

Je nchi nyingine ei Kenya, Uganda wao bado wanadaiwa na wastaafu wao au VP?

Je NI Kwa NN wanaaendelea na jumuia wakati kuna malalamiko ya wastaafu.
Serikali lipeni watu stahiki zao acheni uwizi
 
Uzi huu naomba usomeke na kilio Cha sisi watu wa Mbezi Kibamba tuliodhulumiwa kwa kuvunjiwa nyumba zetu bila fidia, halafu eneo zilipovunjwa nyumba bado liko wazi.
Tunatanguliza shukrani.
Mlikuwa mmejenga kwenye viwanja halali vilivyopimwa au mlivamia tu eneo?
 
Mkuu umeelezea hoja muhimu ambayo inaonyesha ukatili wa serikali yetu, hizi fedha hazikua za serikali zilitoka kwenye kodi ya Waingereza SIO watanzania, greedness ya viongozi wetu ndio ilipelekea wasitaafu hawa wasilipwe na wanasheria makatili wakatake advantage ya kuwadhulumu zaidi wastaafu hawa kwa eti kuwatetea mahakamani, wengi wao waneshatangulia mbele ya haki bila kupata haki zao,President mkapa aliwaongopea na matokeo yake wakalipwa flat rate isiyozidi 3M regardless miaka uliyofanya kazi EAC, hii ni day light robbery kwa wazee wetu, but serikali yetu inafanya hivi huku wakielewa hakutakua na push back.
 
Ukishazeeka huku kwetu bongo, ukiwa mtumishi wa chini hakuna anaekujali, hata serikali haikuthamini, huna thamani tena, ndio maana hata vikongwe wanauwawa huko Kanda ya ziwa na mamlaka zipo kimya
 
Hapa kwetu Tanzania ambapo Ujamaa ulikuwa umeshika hatamu ilionekana kuwa kuwalipa wafanyakazi hao fedha hizo zitakuwa ni nyingi sana, hivyo Serikali chini ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikaamua kuzipangia pesa hizo matumizi mengine. Ikawa imeisha.
Naomba nikusahihishe kidogo kwa mambo mawili.

Pamoja na Jumuiya ya Afrika kuvunjika mwaka 1977, ripoti ya ugawaji wa mali na madeni ya Jumuiya hiyo haikukamilika hadi mwaka 1985.

Fedha za wastaafu wa Jumuiya hiyo zilikabidhiwa kwa serikali ya Tanzania chini ya Rais mpya Ali Hassan Mwinyi ili iwafikishie wastaafu hao.

Ni serikali hiyo ambayo badala ya kuzifikisha kwa walengwa iliunda eti kitengo ndani ya Wizara hiyo kupitia na kukokotoa upya malipo hayo.

Sijui kwa nini umeamua kumtaja Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye kwa wakati huo aliisha kung'atuka. Baba wa Taifa hakuwa fisadi.
Laana zingine hawa tunajitafutia wenyewe kwa dhulma zetu.
Ni kweli, laana ya kuwadhulumu hao wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki itaitafuna serikali ya CCM hadi ing'oke madarakani.

CCM pia iliasisiwa mwaka 1977 Jumuiya ilipovunjika na hadi leo wastaafu wachache wazee waliopo wanaendelea kuilaani CCM na serikali yake.

Adui namba wani wa taifa letu pendwa si mwingine bali CCM!
 
Unamkumbuka Ile hospitali ya Koka?
Gorofa nne. Ninachojua Ni kwamba Dar huwezi kujenga hospitali ya gorofa nne bila kuwa na vibali vyote.
ILIKUA ZAIDI YA MITA MIA

ILIBOMOLEWA MCHANA KWEUPE BILA FIDIA.
Jibu swali langu basi!
 
Natanguliza salamu,
Jumuiya ya Afrika ya Mashariki iliundwa mwaka 1967 na kuvunjika mwaka 1977. Baada ya kuvunjika Jumuiya hii, Serikali ya Uingereza ilitoa fedha kwa ajili ya kuwalipa pensheni zao wafanyakazi wa iliyokuwa Jumuiya hiyo. Wafanyakazi wa Kenya na Uganda walilipwa pesa zao.

Hapa kwetu Tanzania ambapo Ujamaa ulikuwa umeshika hatamu ilionekana kuwa kuwalipa wafanyakazi hao fedha hizo zitakuwa ni nyingi sana, hivyo Serikali chini ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikaamua kuzipangia pesa hizo matumizi mengine. Ikawa imeisha.

Kufikia mwishoni mwa miaka ya 90 yakaanza majadiliano ya kuunda upya Jumuiya hiyo, changamoto ikawa Tanzania na wafanyakazi wake ambao hawakulipwa stahiki zao. Makubaliano yakawa wafanyakazi hao walipwe kwanza ndiyo Jumuiya mpya ianzishwe. Kweli mchakato ulifanyika wakalipwa stahiki zao.

Cha kusikitisha ni kuwa wafanyakazi hawa walilipwa malipo waliyostahili kulipwa mwaka 1977. Serikali yetu haikujali mfumuko wa bei wala kushuka kwa thamani ya Pesa.

Unakuta mtu alilipwa 400,000/= mwaka 1999, lakini kiuhalisia thamani ya pesa hiyo haipo sawa na 400,000/= ya 1977. Laki nne ya 1977 mtu angeweza kununua nyumba nne Ilala, lakini laki nne ya 1999 mtu huyo angeweza kujenga nyumba Tegeta?

Haki iliyocheleweshwa ni haki iliyodhulumiwa, wazee hawa walidhulumiwa stahiki zao. Sasa basi tunaiomba Serikali yetu inayojali watu wake iwatazame wazee wetu hawa na kuwalipa stahiki zao kwa kuzingatia mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya pesa.

Wote wenye vyeti feki na wastaafu wa EAC walikuwa watumishi, japo hawa wenye vyeti feki walighushi vyeti ili kupata ajira isivyo halali. Kwa mtazamo wangu wanaostahili malipo stahiki kati ya makundi haya mawili ni wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Tushirikiane kupaza sauti ili wazee wetu hawa wapate stahiki zao.

Laana zingine hawa tunajitafutia wenyewe kwa dhulma zetu.

Naomba kutoa hoja.
Umeanza vizuri ila kuanza kuwaponda wenye vyeti feki haijakaa poa...ungejikita kwenye wazee tu.
 
Natanguliza salamu,
Jumuiya ya Afrika ya Mashariki iliundwa mwaka 1967 na kuvunjika mwaka 1977. Baada ya kuvunjika Jumuiya hii, Serikali ya Uingereza ilitoa fedha kwa ajili ya kuwalipa pensheni zao wafanyakazi wa iliyokuwa Jumuiya hiyo. Wafanyakazi wa Kenya na Uganda walilipwa pesa zao.

Hapa kwetu Tanzania ambapo Ujamaa ulikuwa umeshika hatamu ilionekana kuwa kuwalipa wafanyakazi hao fedha hizo zitakuwa ni nyingi sana, hivyo Serikali chini ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikaamua kuzipangia pesa hizo matumizi mengine. Ikawa imeisha.

Kufikia mwishoni mwa miaka ya 90 yakaanza majadiliano ya kuunda upya Jumuiya hiyo, changamoto ikawa Tanzania na wafanyakazi wake ambao hawakulipwa stahiki zao. Makubaliano yakawa wafanyakazi hao walipwe kwanza ndiyo Jumuiya mpya ianzishwe. Kweli mchakato ulifanyika wakalipwa stahiki zao.

Cha kusikitisha ni kuwa wafanyakazi hawa walilipwa malipo waliyostahili kulipwa mwaka 1977. Serikali yetu haikujali mfumuko wa bei wala kushuka kwa thamani ya Pesa.

Unakuta mtu alilipwa 400,000/= mwaka 1999, lakini kiuhalisia thamani ya pesa hiyo haipo sawa na 400,000/= ya 1977. Laki nne ya 1977 mtu angeweza kununua nyumba nne Ilala, lakini laki nne ya 1999 mtu huyo angeweza kujenga nyumba Tegeta?

Haki iliyocheleweshwa ni haki iliyodhulumiwa, wazee hawa walidhulumiwa stahiki zao. Sasa basi tunaiomba Serikali yetu inayojali watu wake iwatazame wazee wetu hawa na kuwalipa stahiki zao kwa kuzingatia mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya pesa.

Wote wenye vyeti feki na wastaafu wa EAC walikuwa watumishi, japo hawa wenye vyeti feki walighushi vyeti ili kupata ajira isivyo halali. Kwa mtazamo wangu wanaostahili malipo stahiki kati ya makundi haya mawili ni wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Tushirikiane kupaza sauti ili wazee wetu hawa wapate stahiki zao.

Laana zingine hawa tunajitafutia wenyewe kwa dhulma zetu.

Naomba kutoa hoja.
Ukimleta paka mweusi wazee wataamka na kuyapata malipo yao🥱
 
Naomba nikusahihishe kidogo kwa mambo mawili.

Pamoja na Jumuiya ya Afrika kuvunjika mwaka 1977, ripoti ya ugawaji wa mali na madeni ya Jumuiya hiyo haikukamilika hadi mwaka 1985.

Fedha za wastaafu wa Jumuiya hiyo zilikabidhiwa kwa serikali ya Tanzania chini ya Rais mpya Ali Hassan Mwinyi ili iwafikishie wastaafu hao.

Ni serikali hiyo ambayo badala ya kuzifikisha kwa walengwa iliunda eti kitengo ndani ya Wizara hiyo kupitia na kukokotoa upya malipo hayo.

Sijui kwa nini umeamua kumtaja Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye kwa wakati huo aliisha kung'atuka. Baba wa Taifa hakuwa fisadi.

Ni kweli, laana ya kuwadhulumu hao wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki itaitafuna serikali ya CCM hadi ing'oke madarakani.

CCM pia iliasisiwa mwaka 1977 Jumuiya ilipovunjika na hadi leo wastaafu wachache wazee waliopo wanaendelea kuilaani CCM na serikali yake.

Adui namba wani wa taifa letu pendwa si mwingine bali CCM!
Asante kwa kunirekebisha mkuu.. Maana habari hii nimeelezewa na mstaafu wa Jumuia hiyo.. Binafsi ikaniuma ndio nikaileta hapa..
 
Back
Top Bottom