Kama makahama ya Kadhi ikipitishwa kwenye Katiba, na sisi wachawi tutaomba mahakama yetu

Shy land

JF-Expert Member
Jul 28, 2013
6,024
1,960
Mimi ni mchawi naheshimu sana, imani na dini za watu japo kuwa sisi wanatudharau kwa kuwa eti tuna imani za kichawi.

Kama nilivyozoea kusema serikali ya Tanzania haiko katika utawala unashikamana na dini yoyote, kwa sababu itikadi za kidini zinaweza kuleta machafuko makubwa katika taifa letu.

Mwl. J.K. Nyerere popote pale ulipo tunakupongeza Watanzania kwa kufanikiwa kiasi kikubwa kutunyofolea dhana za kidini, ukanda pamoja na ukabila katika taifa letu, ndio maana hadi leo Watanzania tunaishi kwa amani bila shaka yoyote japo kuwa ni masikini.

Umasikini wetu ni bora zaidi kwa kuwa tuna amani katika taifa letu, wahenga walisema NI BORA KULA UGALI NA CHUMVI KWENYE AMANI, KULIKO KULA WALI NA NYAMA YA KUKU KWENYE VITA.

Hoja yangu ni kuhusu kwa wenzetu wanaodai mahakama ya Kadhi yatambuliwe na serikali na yaendeshwe kwa hela za umma hata kama sisi wachawi hatuhusiki kwenye mahakama hizo.

Kama serikali itakubaliana na madai hayo, na sisi wachawi tuko tayari kuishawishi serikali ya Tanzania kufugua mahakama zetu.
 
Bush land

Kwani rasimu ya mwisho ya katiba mpya ina kipengele hicho cha mahakama ya kadhi?
 
Last edited by a moderator:
Bush land

Wachawi hamna haki duniani kote mgekuwa mnajulikana basi usingekuwa hai
 
Last edited by a moderator:
Bush land

Kwani wachawi si mna mahakama zenu mnazopean hukumu? pia mahakama zenu hazipo fair mnakaa na kujadili hukumu hata za mtu asiekuwa mchawi, mnapitisha hukumu bila kusikiliza upande mwingine.

Mimi nahisi mkitaka kutambulika kwanza muanze kutumia ujuzi wenu kuleta changamoto za kimaendeleo, sio mnakaa na kuroga hadi mifugo, wengine wanaroga hadi maua yako.
 
Last edited by a moderator:
Huyu itakuwa katoka milembe uchawi Tanzania haukubaliki kwanza piga promo watu waukubali uchawi kisha ndo utake mahakama sawa kijana kwanza mnahakama zenu leo mnapanga mumue flani au ukamroge mtu jitokezeni muone km hatutowaua live
 
Huyu itakuwa katoka milembe uchawi Tanzania haukubaliki kwanza piga promo watu waukubali uchawi kisha ndo utake mahakama sawa kijana kwanza mnahakama zenu leo mnapanga mumue flani au ukamroge mtu jitokezeni muone km hatutowaua live

mbona tunajulikana na kila mtu anatujua.
 
yaani wewe ungekua kanda ya ziwa alafu wakakubaini ungekua usha rest in peace zamani sana..
 
Ukiamua kula miiba, basi uwe na makalio ya kuitolea miiba hiyo. Sio mnajidai ubabe wa kutaka vitu ambavyo hamtaki kulipa gharama zake!
 
Kama nyinyi ni wachawi na mupo fungueni ofisi zenu, muombe leseni na mtakuwa mnalipa kodi hapo ndo mtadai Mahkama yenu.

Kwanza sijaona faida ya wachawi hapa nchini kwetu labda husda mulizonazo
 
Back
Top Bottom