Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Subiri kidogo, miradi yote tunayoiona itasimama, ndipo utajua tofauti kati ukweli na uongo. Kati ya Rais na mwimba taarabu.

Awamu zote za marais waislam nchi hii huyumba sana. Subiri tu ujionee.
Hata miradi ikiisha itakuwa sio ya Magufuli.. itakuwa ya mama, maana yeye ndo ameimalizia. Tatizo umejaa chuki ya udini. Hapo ndo upumbafu wako unapodhihirika
 
Wewe jiti takataka kabisa. Take home msg ni ipi? Usukuma bado umekutawala. Kufa uende umkumbatie Jiwe huko kaburini mbusiane
Kweli jamaa amekukwaza 😀😀

Hata hivyo kosa kubwa lililofanywa na mwendazake linaloonesha angekuwa kiongozi mpigaji ni pamoja na kujitoa kwenye Serikali ya Uwazi pamoja na kudhibiti vyombo vya habari na Upinzani (Hii ilikuwa ni ishara ya kwanza kwa watanzania).

Mwisho wa siku hakukuwa na Checks and Balance hivyo kama ikapelekea mwenye uwezo wa kuchota hela anachota huku Wakimpamba na mapambio ya kila aina, wakichagiza na Neno Wazalendo pamoja na Wanyonge 🙌😭
 
Anachojaribu kusema ni hiki

Kama Magufuli alikuwa nduli, fashisti na fisadi basi alikuwa mzuri. Mtu Fisadi anakwapua pesa halafu anapeleka umeme kila kijiji na Elimu bure nchi nzima na zahanati nchi nzima na miradi ya barabara nk hadi vichochoroni. Mistendi kibao hadi mingine inaitwa stendi ya Ndugai hilo fisadi na fashisti na nduli wananchi tunalikubali sababu lilikuwa linakwapua na kuwapelekea wanyonge miradi kibao.

Lingebaki liendelee kufisadi na kupelekea wanyonge

Haya tunasubiri msio nduli na mafashisti na msio mafisadi tuone kama spidi ya maendeleo kwa wanyonge ya hilo nduli,fashisti na fisadi tuone kama spidi hiyo mtaiweza.Tuone nani zaidi kati ya nduli fashisti na Fisadi Papa Magufuli na ambao sio nani zaidi .Wanyonge ndio watakuwa mahakimu kwa hili

Heheheheeee!! UMENENA! Kama huyo ndo FISADI KIASI HIKI NA KAFANYA MAENDELEO KIASI HIKI! BASI TANZANIA TUNAHITAJ MAFISADI WA AINA HII KWA KWELI
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji binafsi nimeshangwaza sana na bandiko lako... Je, hii posti ni matokeo ya chakula ulichokula ama?
Kubali ukatae nchi imeliwa sana na #Sukumagangs! Watu wameonewa kupitiliza ndani ya utawala wa Mtakatifu JPM wa I.
Wewe ni mwandishi mzuri... Bila shaka unafahamu kuwa Uhuru wa kutoa, kupata au kuandika habari ukiminywa wengi wanabaki gizani huku wachache wakijinufaisha!
Kubali ukatae... Mtu huwezi kujitwalia madaraka ya kujifanyia matumizi nje ya bajeti tena without checks and balances alafu mambo yakakaa sawa!

Nakumbuka miaka kadhaa ulikuwa mpinzani wa ccm na mwamasishaji wa Katiba Mpya... Zinduka rudi kwenye mstari... Mtakatifu JPM wa I keshaenda zake...!!!
 
Unaandika mithili ya layman. Kwani kuwa mpinzani lazima ujinasibishe na wapinzani unaowaita wamepotea?

Wewe binafsi ume compromise nafsi yako kwakua wengine wamepotea? Really?

Hivi misimamo na ideology za mtu huwa kwa wengine au wewe binafsi?

Kwahiyo huko nyuma ulifanya upinzani kwakua wengine walifanya?

Au kauli na matendo yako yanadhihirisha ulifanya mambo kwa chuki binafsi, chuki za kimaslahi, kikanda, kidini na kirangi? Seriously mtu mwenye upinzani wa Moyoni unaweza sema nilishindwa fanya upinzani maana sikumjua mpinzani wa kweli?

Seriously mtu wa kariba yako ulikuja kuwa simply brainwashed na siasa za watu aina ya akina Magufuli really?
Mkuu Lusungo ,huna haja ya kubishana na misukule.
Binadamu anayeamini katika binadamu mwenzake huyo ni msukule. Yaani kama hakuna mtu anayefanya hivi na vile,basi nawe hufanyi!!! Huo si ni usukule.
Yaani mtu anadiriki kuandika kabisa kuwa yeye ana damu ya kipinzani lakini anahisi umeanza kumtoka kisa hawapo wapinzani!!??
Really!!???
 
Sidhani kama huu CAG ni mkweli.Yani kaaamua kwa makusudi kununulika Kuiua CCM na Tanzania .ni aibu kwa kweli.Tunarudi nyuma kwa kasi ya ajabu.
Kama Mwanakijiji alivyosema kuna kitu kinaundwa.Ajabu Spika hajui kinachoundwa.in short CCM is finished ,Tanzania is finished.
Prof Assad nae alinunulika kuiua CCM,na huyu nae kanunuliwa kuiua CCM? Duh ma CAG wote Ni wapinzani! Tatizo mlizoea kusikia sifa tu. Poleni sana
 
Ukisoma mitandao ya kijamii hasa twitter utafikiri kweli hii nchi imeibiwa kila kitu na hakuna kitu kimeachwa, kumbe sio kweli.

Watu wanajifanya kushangaa ATCL kupata hasara, hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kushangaa atcl kupata hasara? By the way, ni shirika gani la serikali linalopata faida? Lipi? Mashirika yote ni hasara kila mwaka kuanzia Tanesco, TPDC, TTCL, ATCL, NHC na mengine yote, kwa nini shida iwe kwa ATCL?

Halafu watu wanataka kusema Magufuli ange eliminate rushwa ama wizi wa mali za umma 100%, hilo jambo halipo Duniani. Duniani kote, kuanzia China ambapo kosa la rushwa unaweza kuuwawa ama Marekani ambapo mifumo iko strong bado watu wanaiba na kula rushwa, tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag
IMG_20210408_210709.jpg
 
Mwandishi ni kama vile hutaki kuamini kuwa Magufuli alikuwa fisadi namba moja wa Tanzania katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Ripoti rasmi za kiuchunguzi wa pesa (CAG) za sasa zinaonyesha hivyo. Ni upigaji mtupu.

Kwanini ushangae hilo sasa wakati wakosoaji wa Magufuli walikuwa wakiyasema hayo kwa miaka mitano yote?

Ni akina nani waliohoji upotezi wa Trilioni 1.5 zilizotajwa na Professor Assad?
Kwanini Professor Assad alifukuzwa kimizengwe?

Kwanini vyombo vya habari vilizibwa midomo?

Kwanini wapinzani walipotezwa, kununuliwa, kuteswa na kuuwawa?

Kwanini wapinzani walinyimwa fursa ya kufanya siasa, kushika ikulu, kuingia bungeni, kutawala serikali za mitaa au mabaraza ya halmashauri ?

Kwanini genge la Magufuli lilikuwa likiratibu utawala wa Magufuli udumu milele?

Kwanini tender zote za miradi mikubwa ziwe siri ya Magufuli na ikulu tu?

Kwanini genge la Magufuli lilitaka kupindisha mambo kwa gharama yoyote ili kukamata kiti cha urais hata baada ya Magufuli kuwa mahututi/kufariki dunia?

Ukweli unaweza kuchelewa kujionyesha, lakini muda utaufunua ukweli wote. Muda umefika sasa kwa utawala wote wa Magufuli kupimwa upya. Tusiogope kusema ukweli hata kama ukweli huo utatufedhehesha baadhi yetu.
Je unakubaliana na mtoa mada kwamba ufisadi huu wa JPM ungeanza kufanyika kipindi cha Mkapa hadi JK Tanzania ingekuwa mbali sana ni kweli?
 
Hakuna aliyefisadi kwenye utawala wa Magufuli,watu hawajaelewa tu, ilikuwa ni hela ilikuwa ikihitajika site ilitoka on time na ilifika site on time bila ya kufuata taratibu. Magufuli aliamini sheria zilizopo ni mbovu zinachelewesha maendeleo.
Ndio maana alifika sehemu Kuna mradi au uhitaji wa mradi hapo hapo aliagiza billions of money kuolewa kwa dharura ndani ya siku chache na mambo yalienda. Hospital kila wilaya, vituo vya afya, kila halmashaur Kuna lami, shule kongwe kufanyiwa ukarabati,nyuma za askar magereza kujengwa, ikulu na maofisi, mahakama n. k. Wamuache mtu huyu wa kipekee. T unakoelekea ni kugumu, Rip Magufuli.
Mungu Wangu ..!! Kama akili zenu watanzania ni kama hivi basi tutaibiwa hadi ifikapo 2150.

Miradi mikubwa na ya kimkakati ina riba kubwa iliyotokana na ucheleweshaji wa malipo hapo we unasema kinyume chake.
 
Nakubaliana nawe unaposema waziri mkuu ajiuzulu,
1.) Huyu waziri mkuu alienda bandari akashindwa kuzima matumizi mabaya (wizi) usiendelee na alipoondoka hakurudi kufatilia kinachoendelea!!
2.) Alitetea ununuzi wa madege na kushawishi uendelee huku akijua hasara tunayoingia nikubwa wastani bilioni 32 kilamwaka. Pia ya sgr hakuyafatilia!
3.) Wizara ya maliasili na utalii kutumia pesa hovyo kufanya matamasha kwa jina lamtu ili kumpa umaarufu kigwangala
tunayejua anautamani urais 2025...naye kukaa kimya.
4.) Waziri mkuu ameshindwa kumshauri vyema rais kwenye miradi yooote mikubwa kuanzia Nyerere dam,sgr,daraja busisi,kuhamia Dom ambavyo vyote tukizama kuchunguza tutaibua madudu kibao
5.) Alidanganya taifa kuhusu afya ya Rais wao na amiri jeshi mkuu! Afya yake sio siri watanzania waliompenda sana wangeambiwa ili wakeshe wakimwombea kama walivyokeshea korona.
6.) Hata kuhusu magari ya wakurugenzi alishtuliwa na msukuma nayeye kulirukia! Inamaana hajui yanayoendelea chini ya ofisi yake na hakuna hatua zawazi ninini kilifuata kurekebisha makosa!
7.) Janga la korona ameshindwa kuweka wazi msimamo wa serikali ni upi na wajibu wa wananchi ninini na serikali inapambana vipi?
8.) Kuhusu kutoroshwa madini,anategea rais wasasa aseme! Yeye alichukua hatua gani haeleweki. Alijigeuza waziri tamisemi akikagua viujenzi vya vituo vyapolisi,zahanati nk.
9.) Elimu yetu zaidi ya kuwa bure ilipaswa kwanza kuwa bora,imwandae kijana kuwa hodari wa kazi anuwai,michezo,Sanaa nk. Ajabu wakitoka vyuoni vijana wanajua zaidi kulalamika,kunywa pombe,kutongozana na kuvaa vimodo...ameshindwa kuboresha elimu yetu.
10.) Alifeli kabisa kushauri na kuchochea demokrasia,amani,utulivu,maisha bora na haki kwa wote!
Wafanyakazi wanakatishwa tamaa hamna madaraja,wafanyabiashara kodi za vitisho, ajira zashida elimu,afya nk.
Kilimo na masoko tabu,korosho yetu na pamba vimeanguka,mafuta being juu!!
Kiufupi waziri mkuu Vila kuangalia umaridadi na mwonekano anapaswa kujiuzulu maramoja amelikwamisha taifa vibaya! Aachie ofisi akaisimamie Namungo huko
Hiyo namba 9 ni bonge la point, kuanzia Ndalichako, Jofo mpaka wazir mkuu ni vilaza sana.

Elimu yetu haina msaada wowote na yenyewe yamekaa tu as if mangedere pori.

Hopeful mama ataamuru mitaala ibadilishw maana aligusia suala la kutoa licheti lisilo na msaada.

Tunataka vijana wasome stadi za kilimo, na Kazi ndo useme wajiajir.
 
Kwa wale wanaolalamika au kutofurahishwa na CAG au ripoti yake, aidha kwa makusudi au kutokuelewa, ni kuwa ripoti ya CAG (hii na zilizopita) sio ripoti za kutunga, bali ni ripoti za yaliyojiri katika mwaka wa fedha husika, Julai 2019 hadi June 2020:-

1) Jukumu la kuandaa mahesabu ni la Taasisi, Wizara, Mashirika, Halmashauri husika halafu yeye CAG (na Ofisi yake) anatoa tu maoni/tathmini ya kitaalam (kikaguzi, kiufundi na kisayansi) juu ya alicholetewa. Ni kama vile wewe ukipeleka damu au choo maabara halafu mtaalam anapima na kukupa majibu kuwa kwenye damu/choo amekuta nini, sasa hapo kosa la Lab Technician ni kukupa mrejesho au?

2) Na ndio maana ukisoma ripoti hii utaona CAG alisema kuna mashirika/taasisi hazijapeleka hesabu kwake kwa ukaguzi na hivyo huoni maoni ya CAG kuwahusu. Kwa hiyo Ripoti ya CAG isijengewe mizengwe na hisia hasi ambazo hazina mashiko wala sababu. Wamemplekea mahesabu wenyewe (kwa mujibu wa Sheria zilizopo), na yeye kwa kutumia utaalam wake akathibitisha na kutoa majibu (kwa mujibu wa Sheria za Nchi).

3) Kuhusisha Ripoti na mambo ya mwendazake au hujuma nk nayo ni hoja mfu. CAG ameagizwa kwenye Katiba na Sheria za nchi kuandaa ripoti ya mwaka ulioisha wa fedha na kuikabidhi kwa Mh Rais (aliyeko) kabla ya tarehe 31 Machi kila mwaka na kwa Bunge la JMT. Kwa hiyo hakuna hila au njama kwamba labda hayati Rais wa awamu ya Tano, Joseph Magufuli angekuwepo angekabidhiwa? Ndio, maana hilo ni takwa la Kikatiba na Kisheria na muda wake ni sasa, sio suala la hisia au utashi wa mtu hapo.

4) Wengine wamefika mbali na kuuliza je kama Mwendazake angekuwepo nini kingetokea? Je CAG angekabidhi ripoti hii? Majibu ni kwamba kwa vile kila mwaka CAG (huyu na Assad) alikuwa anaandaa na kukabidhi ripoti basi yangetokea yale yale yaliyotokea miaka 5 iliyopita. Angekabidhi tu. Tofauti nayoiona ni pengine CAG asingekuwa na uwanja mpana na huru wa kusoma ripoti yake mbele ya Magufuli kama sasa kwa Rais Samia. Bali "angeelekezwa" cha kusoma, halafu "Kitengo" na wale wa propaganda wangeendelea kutokea hapo mara moja.
NB: Hivi mnakumbuka CAG Asssad alisomea wapi ripoti yake ya mwisho? Mnakumbuka mazingira ya ndani na nje ya Bunge kumhusu CAG na Ripoti yake? Sasa ikiwa Rais na Bunge walikuwa "hostile" kiasi kile kwa nini leo idhaniwe kuwa CAG ana lake jambo au kuna mkono wa mtu nyuma ya ripoti hii?

5) Hayati Magufuli alipenda na alipewa sifa nyingi mno kwa namna ya uongozi wake, kauli zake, miradi na yote aliyoyafanya (mema na mabaya). Sasa kwa vile kanuni za maisha zinasema kila shilingi ina pande mbili, na kila kitu kina kinyume (opposite); basi kwa kadiri alivyopenda na kupokea sifa, basi kwa kadiri hiyo hiyo anastahili na atapokea lawama na hukumu ya haki katika yote aliyoyasema na kufanya. Ni haki na ni sahihi. Kuna hotuba yake aliwahi kusema hivi (NAMNUKUU):-
"....Hela ya Serikali haipotei...anaweza kupotea binadam lakini hela haipotei (kicheko/makofi).....
Na katika kipindi changu hela ya Serikali haipotei (makofi zaidi).....Na nasema ukweli kabisa, HAITAPOTEA...."
kadiri Hivyo basi, kwa kauli, ahadi, haiba na matendo yake anastahili kupokea mzigo huu, na wa mwaka 2020/21 utakaokuja mwakani.

6) Katika miaka yote ya utawala wake kama Rais wa Tanzania, sikuwahi kusikia wasaidizi au washauri wake wakisifiwa wazi wazi lakini yeye alisifiwa mara zote na mahali kote, ndio tena sana tu! Sasa kwa nini mnataka wakati wa lawama na adhabu yeye apate kidogo? Ni uhalisia tu, wanaita natural course.

Hayati Magufuli aliwahi kusema yeye hashauriki....na mtu akimshauri ndio ameharibu kabisa.... sasa je hao "washauri" mnaowatuhumu leo ni akina nani? Yaani kivipi labda?? Au hamkuwa mnamsikiliza na kumwelewa hayati alichosema? Hataki ushauri. PERIOD!
Alifika mahali akasema yeye ni mwamba, jiwe, mgumu....hatishwi, hatishiki nk hizo kauli na matendo yake ndio vinaakisiwa na ripoti ya CAG. Yaani ni boga na ua lake.
Ukisoma ripoti ya CAG inataja "nika..." "mimi" "nili.." nk - CAG anafanya kitu kinaitwa uwajibikaji na haki. CAG atabeba lawama zote au atabeba sifa zote za Ripoti hii (ingawa ni timu ya wataalam wa Ofisi yake na nje waliondaa ripoti). Aliyeapa na kupewa mamlaka ndiye anayewajibika kwanza kisha wa chini yake, hivyo tusilete ngonjera na sarakasi, mhusika mkuu ni Rais wa Awamu ya Tano. Wengine wanafuatia.
Maana yake baada ya hayati Magufuli, wote waliohusika (moja kwa moja au kwa maelekezo yake) nao watawajibika, na nasisitiza wanapaswa kuwajiba WOTE.

7) Kwa nini, nauliza tena kwa nini.....

a) Magufuli alichukia kukosolewa yeye au Serikali yake?

b) Kwa nini alikataa na kuua transparency governance ambayo ni msingi wa good governance?......

c) Kwa nini alifanya mambo gizani? Kwa mfano alinunua ndege kinyume cha Sheria za Nchi na kinyume hata cha biashara ya ndege (aviation industry) ya ndege duniani. Tena alinunua CASH! Hapo anakwepaje lawama? Akateua Bodi ya Wakurugenzi wasiokuwa na ujuzi wala uzoefu na biashara ya usafiri wa ndege! Anakwepaje lawama hapo? Hizo ndege alishauriwa lakini hakusikia....hivi mnaojaribu kumtetea hayati huwa wanawazajewazaje lakini?

NB: Kwenye ripoti hii ndio nimesoma kwa mara ya kwanza, rasmi, kwamba ndege 8 zilinunuliwa kwa Shs 1 Trillion na ushee! Yaani ndege 1 kwa wastani wa Shs 125 Billion! Where is the value for money there? Was it a national priority? Isn't he accountable and guilty?

d) Kwa nini alichukia uhuru wa vyombo vya habari? Kwa nini aliminya na kusigina Katiba na Sheria za nchi katika kutekeleza matakwa yake aliyoyaita "maono" "sacrifice"?

e) Kwa nini alikuwa jeuri na mbabe mbele ya mihimili mingine ya dola? Kwa nini alikiuka sheria za manunuzi na miongozo mingine yote kuhusu miradi na uendeshaji wa Serikali?

f) Kwa nini alidanganya kuwa miradi inajengwa kwa fedha za ndani ilihali alikuwa anakopa- aliingia deni la Taifa likiwa Trilioni ngapi na ameondoka likiwa Trilioni ngapi?

g) Kwa nini aliendesha nchi kwa propaganda, uongo, vitisho na uhalifu???

h) Kwa nini hakulipa mishahara, posho, kupandisha madaraja watumishi wa Umma kwa muda wote wa utawala wake? Na kwa nini alipenda kuogopwa? Na kwa nini hakuona kuwa kimya hakimaanishi utii, na wafanyakazi wenye motisha ndogo ya kazi hawawezi kuzalisha kwa tija wala kutoa huduma bora kwa mwajiri?

i) Kwa nini alijaza watu wake wa karibu au wenye nasaba za ukabila au ukanda (upendeleo) kwenye nafasi nyingi za juu kuanzia Serikali kuu, Mashirika mpaka Serikali za Mitaa???

j) Kwa nini alipinga siasa za ushidani? Kwa nini alitesa, kupoteza na kutisha wapinzani wake wa kisiasa? Na alienda mbali mpaka akaharibu chaguzi za 2019 S/Mitaa na 2020 Uchaguzi mkuu?
Kwa nini alisababisha hasara, maumivu na usumbufu wote ule kujaribu kuhalalisha utawala wa kiimla ili kuendeleza na kuficha mambo kama yalivyoibuliwa na CAG??

8) Kwa haya yaliyotokea katika siku hizi 24,tangu kifo cha Magufuli, kuingia kwa Rais Samia na sasa Ripoti ya CAG - tumepata majibu yote ya maswali magumu yaliyotusumbua kwa miaka mingi. Pengine hapatakaa paweko na siku 24 za aina hii katika historia ya maisha yetu na ya taifa letu Tanzania. Yako mengi sana yaliyojitokeza na tunayopaswa kujifunza. Leo nitaangalia machache tu:-

a) Tatizo la nchi yetu ni nini hasa - ni CCM na Ujamaa, mtawalia.
Mniwie radhi niseme, Ujamaa ni sera ovu iliyo kinyume cha maumbile ya fikra na mifumo ya uzalishaji mali wa binadam. Kama unabisha soma critical history ya nchi na falme za ulimwengu toka Adam mpaka sasa. Sio suala la hisia au mapenzi, ni factuality. Ni realities za maisha ulimwenguni humu.

b) Kwa nini rushwa,ufisadi, maradhi, ujinga na umaskin vimeendelea kutusumbua kama nchi maiaka yote 60 ya Utaifa wetu? - ni kwa sababu ya ubovu na udhaifu wa katiba yetu ya sasa. Msingi wa utawala bora ni Katiba nzuri. Msingi wa Uongozi bora ni Katiba nzuri. Hapo ndio pa kuanzia kuweka tofali la kwanza la ujenzi mathubuti. Viraka viraka na hila ndio vimetupa matokeo tuliyo nayo hadi sasa, tukibadilika na kubadilisha, basi matokeo nayo yatabadilika. Tukiktaa tutabaki hapo hapo.

c) Siasa chafu. Hili halihitaji maelezo wala ufafanuzi, Awamu ya Kwanza mpaka ya Tano, siasa hazikuwa safi, zina hila na unafiki mwingi. Tujirekebishe sasa.

Kwa kumalizia, naomba Rais wa JMT Mh Samia afikiri na kutenda nje ya mfumo na utamaduni wa kulindana wa CCM. Aweke Taifa mbele, hata kama itamgharim yeye kupendwa chamani sisi wananchi wazalendo wa Tanzania tutampenda na kumuunga mkono na atafanikiwa kuliko watangulizi wake wote, ili tuondoke hapa kwenye tope na mkwamo uliojaa kashfa, umaskin na ufisadi mfano wa donda ndugu.

Niwe wazi tu. Suala la hayati Magufuli kuwa na wafuasi na mashabiki (fans and sympathizers) ni la kawaida, sio jambo geni. Historia inaonyesha hata Hitler, Mao, Mussolini, Stalin, Mobutu, Saddam, Idi Amini na wengine kama hao, nao pia walikuwa na wafuasi na wapambe, si kidogo. Walikuwa wema kwa walio wao (waliofadika nao tu), lakini waliharibu nchi na mataifa yao na ulimwengu kwa ujumla. Tuwapuuze. Tutazame mbele, kuijenga Tanzania bora kwenu na vizazi vijavyo.

Mungu Ibariki Tanznia, Mungu Mbariki Rais Mama Samia atende haki, mpe hekima na upendo na pia umlinde ili aongoze Taifa letu hili kipindi hiki kigumu cha mpito! Mungu Ibariki JF na watu wote waliosimama na kuhatarisha maisha yao kupambana na waovu, maonevu na dhuluma za Awamu ya Tano, ambao kwa namna moja au nyingine wameisaidia nchi yetu na kuvuka salama kuelekea kwenye ustawi na mafanikio, hao ni watumishi wako! Lakini usiwaache wanafiki na watesi wetu bila adhabu, ili wajifunze kutokudhihaki... lakini pia wajue kuwa Wewe ni Mtakatifu na unapenda haki, uwape kutambua na kutubu kisha wajifunze kupenda kweli na kujua kuwa hapa duniani sisi ni mawikili Wako tu na wapitaji, kama baba zetu. Tutende haki, tutende mema, tusiwe wanafiki. Amen.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli.

Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea.

Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufisadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Mwanakijiji. Acha porojo, elezea wewe yalomshinda Magu kutueleza.
1. Chato airport,how it costed us, why, kwa idhini ya Nani?
2. Report ya Tanroada 5yrs report,(Kichaka)
3. Salaries kwa watumishi.
4. Deni la taifa,lolikuwaje 2015,na Sasa likoje?
5. Ni kweli Kila kitu tumefanya kwa pesa zetu za ndani?
6. Kibadili katiba,kuvunja ukomo wa Rais, indeed Kuna mtu alotuma watu kufanya hili I guess.!!
 
Wapigaji wamerudi kwa kasi ili mambo yao yaende kazi ni moja kuua legacy yote ya mwendazake alafu waanze kupiga kama ilivyoada
Kwa sasa kazi kubwa inayofanyika ni kutunga story mbaya (ambayo si ya ukweli) na kuonyesha kuwa uongozi wa mwendazake (JPM) ulikua ni mbaya na ulididimiza nchi. Baada ya kuahalilisha hicho wanachokitunga kwa baadhi na kukieneza basi wenye malengo yao wataanza kutekeleza wanacho-plan na kukitetea kwa nguvu zote hali ya kuwa wala si kwa maslahi ya taifa. Inahitaji umakini kuwabaini. Cha msingi Mama awe nao makini sana wasijekumgeuka mbeleni.
 
Kwa sasa kazi kubwa inayofanyika ni kutunga story mbaya (ambayo si ya ukweli) na kuonyesha kuwa uongozi wa mwendazake (JPM) ulikua ni mbaya na ulididimiza nchi. Baada ya kuahalilisha hicho wanachokitunga kwa baadhi na kukieneza basi wenye malengo yao wataanza kutekeleza wanacho-plan na kukitetea kwa nguvu zote hali ya kuwa wala si kwa maslahi ya taifa. Inahitaji umakini kuwabaini. Cha msingi Mama awe nao makini sana wasijekumgeuka mbeleni.
Wanaenda kuua shirika la ndege, wanarudisha mradi wa BAGAMOYO ,wanaenda kumwaga ajira na kuongeza mishahara kupunguza machungu ili wapige vizuri mama anakazi kubwa sana
 
Kwa huyu mama bado ni mapema sana ku judge direction anayoenda,tumpe muda kidogo ili tuweze kupata tathmini ya utendaji kazi wake...
Shida sio mama kuna kundo lilikua mute ndio watakayoiendesha hii nchi
 
Anachojaribu kusema ni hiki

Kama Magufuli alikuwa nduli, fashisti na fisadi basi alikuwa mzuri. Mtu Fisadi anakwapua pesa halafu anapeleka umeme kila kijiji na Elimu bure nchi nzima na zahanati nchi nzima na miradi ya barabara nk hadi vichochoroni. Mistendi kibao hadi mingine inaitwa stendi ya Ndugai hilo fisadi na fashisti na nduli wananchi tunalikubali sababu lilikuwa linakwapua na kuwapelekea wanyonge miradi kibao.

Lingebaki liendelee kufisadi na kupelekea wanyonge

Haya tunasubiri msio nduli na mafashisti na msio mafisadi tuone kama spidi ya maendeleo kwa wanyonge ya hilo nduli,fashisti na fisadi tuone kama spidi hiyo mtaiweza.Tuone nani zaidi kati ya nduli fashisti na Fisadi Papa Magufuli na ambao sio nani zaidi .Wanyonge ndio watakuwa mahakimu kwa hili
Na kwakweli wanathibitisha kauli yake kuwa sisi ni matajiri na donor country, kama yeye anaweza kuchota matrilions na bado akafanya wonders hizi sisi ni akina nani sasa?
 
Back
Top Bottom