Elungata
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 40,205
- 33,224
walisafiri toka misri kuhudhuria sensa bethlehemu?..hebu karudie tena kusoma.Mkuu huwa unasikilizaje taarifa hili ndilo tatizo la UDINI hukusikiliza hadi nukta ya mwisho kwasababu ulijawa na udini wa kwanini Redio Iman imefungiwa, kwa taarifa yako Redio Clouds FM imetiwa faini kwa kushabikia ushoga jambo ambalo ni kinyume na maadili ya Tanzania. Iman kama kawaida wakati wa Sensa redio hii ilihamasisha waislam wasishiriki sensa eti ni nje ya imani ya Kiislam. Biblia yangu inasema Mariam na Yusuf walisafiri toka Misri hadi Bethlehem kwenda kushiriki sensa. Redio Neema FM ilishabikia uchinjaji wa nyama kuwa ni haki ya Wakristo kuchinja jambo ambalo wale waliosikiliza walihamasika na kufanya vurugu hadi kuleta maafa. Hata hivyo Redio zote tatu wameambiwa wako huru kukata rufaa kama hawajaridhika na hukumu hiyo.
Matokeo ya rufaa ni kwamba ikiwa rufaa itashindwa ikatakiwa Iman na Neema waendelee na adhabu basi adhabu itakuwa mara mbili yake. Clouds nayo itaambulia double hiyo hiyo. Tusubiri.
My take: Nimefurahi sana redio hizi kupewa adhabu tena ninadiriki kusema kuwa adhabu walizopewa ni ndogo sana.