KAHAMA: Zaidi ya wafanyakazi 1,300 wakosa ajira baada ya mgodi wa Buzwagi kufungwa rasmi

Zurie

JF-Expert Member
Jul 6, 2014
1,835
4,671
KAHAMA: Zaidi ya wafanyakazi 1,300 wamekosa ajira, huku Kodi ya Sh. Bilioni 28 ikikosekana baada ya Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi kufungwa rasmi.

Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa mgodi huo unaomilikiwa na Acacia, umefungwa kwa kushindwa kuzaliwa kiwango cha madini hayo kilichotarajiwa.

Kufungwa kwa mgodi huo pia kumeikosesha Wilaya ya Kahama jumla ya Sh. Bilioni 1.7 zilizokuwa zikilipwa kila mwaka, ikiwa ni mrabaha.

Uongozi wa mgodi huo umeeleza kuwa uzalishaji wa dhahabu katika eneo la mgodi umeshuka kutoka gramu 1.35 hadi 1.00 (kwa kila kilo moja ya mchanga/mawe inayochimbwa) kwa mwaka jana. Mgodi huo ulianzishwa mwaka 2009 kwa mtaji wa wawekezaji unaokaribia Sh. Trilioni moja.

Tayari mgodi huo umeanza kuuza baadhi ya mali zake yakiwamo magari, mashine, majengo na vifaa vingine. Mnada mkubwa wa kuuza mali za mgodi huo utafanyika mapema mwezi Machi, 2018.
 
KAHAMA: Zaidi ya wafanyakazi 1,300 wamekosa ajira, huku Kodi ya Sh. Bilioni 28 ikikosekana baada ya Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi kufungwa rasmi.

Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa mgodi huo unaomilikiwa na Acacia, umefungwa kwa kushindwa kuzaliwa kiwango cha madini hayo kilichotarajiwa.

Kufungwa kwa mgodi huo pia kumeikosesha Wilaya ya Kahama jumla ya Sh. Bilioni 1.7 zilizokuwa zikilipwa kila mwaka, ikiwa ni mrabaha.

Uongozi wa mgodi huo umeeleza kuwa uzalishaji wa dhahabu katika eneo la mgodi umeshuka kutoka gramu 1.35 hadi 1.00, mwaka jana. Mgodi huo ulianzishwa mwaka 2009 kwa mtaji wa wawekezaji unaokaribia Sh. Trilioni moja.

Tayari mgodi huo umeanza kuuza baadhi ya mali zake yakiwamo magari, mashine, majengo na vifaa vingine. Mnada mkubwa wa kuuza mali za mgodi huo utafanyika mapema mwezi Machi, 2018.
Lazima hela iongezeke thamani huu mwezi.... alafu uchumi ukue kuelekea kwene viwanda
 
KAHAMA: Zaidi ya wafanyakazi 1,300 wamekosa ajira, huku Kodi ya Sh. Bilioni 28 ikikosekana baada ya Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi kufungwa rasmi.

Taarifa za uhakika zinaeleza kuwa mgodi huo unaomilikiwa na Acacia, umefungwa kwa kushindwa kuzaliwa kiwango cha madini hayo kilichotarajiwa.

Kufungwa kwa mgodi huo pia kumeikosesha Wilaya ya Kahama jumla ya Sh. Bilioni 1.7 zilizokuwa zikilipwa kila mwaka, ikiwa ni mrabaha.

Uongozi wa mgodi huo umeeleza kuwa uzalishaji wa dhahabu katika eneo la mgodi umeshuka kutoka gramu 1.35 hadi 1.00, mwaka jana. Mgodi huo ulianzishwa mwaka 2009 kwa mtaji wa wawekezaji unaokaribia Sh. Trilioni moja.

Tayari mgodi huo umeanza kuuza baadhi ya mali zake yakiwamo magari, mashine, majengo na vifaa vingine. Mnada mkubwa wa kuuza mali za mgodi huo utafanyika mapema mwezi Machi, 2018.
Makinikia " episode".

Sizonje atawaajiri chato airport! Wengine Lumumba n.a. bomba la mafuta!
Pole pole kimyaaa!
 
Gram 1.35 kwa mwaka????????
Na kama ni kutoka 1.35 mpaka 1.00 kwanini wasipunguze wafanyakazi, expenditure wakaendelea na Kazi. Badala yake wanafunga rasmi.
Labda wanaona faida watakayokuwa wanaipata kwa kupata gramu 1.00 ni bora wakafanye biashara hata ya kuuza chips Mkuu
 
Mji wa Kahama nao utaathirika sana kibiashara,walio wekeza biashara zao mji huo wajiandae na wao kufunga biashara.
Kama wana mikopo,waandae dhamana zao kutaifishwa kufidia mikopo hiyo,au waanze kuuza mapema.
Baadhi ya hao Wafanyakazi watauza nyumba zao kama kawaida ya wengi wao
 
Back
Top Bottom