nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
10 DECEMBER 2012
Kadi ya CCM yamponza Slaa *Sasa ashinikizwa kujiuzulu nafasi yake *Wanachama wadai kukosa imani naye
Na Mwandishi Wetu
MJUMBE wa Mkutano Mkuu Taifa CHADEMA, mkoani Mbeya, Bw. Edo Mwamalala, amemtaka Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Willibrod Slaa, kujiuzulu wadhifa wake kwa madai ya kikidhalilisha chama chao kwa kuendelea kumiliki kadi ya CCM.
Bw. Mwamalala aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea jinsi alivyoguswa na kitendo cha Dkt. Slaa kukiri hadharani kumiliki kadi ya CCM wakati anajua dhamana kubwa aliyopewa katika chama hicho.
Alisema katiba ya chama hicho sura ya tano, ibara ya kwanza kifungu kidogo cha sita 5.1.6 kinachosema, mwanachama wa chama hicho hapaswi kuwa mwanachama wa chama kingine cha siasa baada ya kujiunga CHADEMA.
Alisema Dkt. Slaa ameanza kuwapa mashaka wanachama wa chama hicho na wengine kuamini huenda huenda yupo CHADEMA kwa kama kibaraka wa CCM anayetumiwa kwa mambo mbalimbali.
"Hivi karibuni Dkt. Slaa amekiri kumiliki kadi ya CCM na kudai kuitunza kama kumbukumbu, halii hii inaonesha bado anatumukia vyama viwili vya siasa kwa maana ya CCM na CHADEMA.
"Umefika wakati wa kiongozi huyu kuwajibishwa na chama, katika mfumo wa vyama vingi, kiongozi wa chama lazima awe mfano kwa wengine hivyo kitendo hiki kinaleta mashaka makubwa," alisema.
Alimtaka Mwenyekiti wa chama hicho Bw. Freeman Mbowe, kuchukua hatua badala ya kuliacha jambo hilo hewani na kama atashindwa kulishughulikia, viongozi wengi zaidi ndani ya chama hicho wanaweza kujitokeza na kusema wanamiliki kadi za CCM.
"Hili ni jambo la hatari sana, wanachama wataamini chama chetu kinaendeshwa na vibaraka wa CCM, haiwezekani Katibu Mkuu wa chama awe anamiliki kadi ya chama tawala.
"Wapo ambao watajitokeza kunikejeli na kudai nimetumwa lakini mfumo wa demokrasia, unatoa fursa kwa kila mtu kueleza kile anachokiona ili kujenga siasa bora nchini," alisema.
Alisema Dkt. Slaa amekosa uadilifu, sifa za kukitumikia chama hicho na kuongeza kuwa yupo tayari kuchukiwa kwa kueleza ukweli wa kile anachokiamini kama mwanachama.
Bw. Mwamalala alisema kama chama hicho kitashindwa kuchukua hatua zozote, atapeleka hoja binafsi katika Mkutano Mkuu kutaka Dkt. Slaa ajadiliwe na kuchukuliwa hatua.
"Wakati Dkt. Slaa anondoka CCM, alipaswa kuwaachia kadi yao, sisi wenye mapenzi mema na CHADEMA, hatuko tayari kuona tunaishi ndani na kadi ya chama ambacho tunataka kukiondoa madarakani katika Uchaguzi Mkuu 2015," alisema.
Kadi ya CCM yamponza Slaa *Sasa ashinikizwa kujiuzulu nafasi yake *Wanachama wadai kukosa imani naye
Na Mwandishi Wetu
MJUMBE wa Mkutano Mkuu Taifa CHADEMA, mkoani Mbeya, Bw. Edo Mwamalala, amemtaka Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Willibrod Slaa, kujiuzulu wadhifa wake kwa madai ya kikidhalilisha chama chao kwa kuendelea kumiliki kadi ya CCM.
Bw. Mwamalala aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea jinsi alivyoguswa na kitendo cha Dkt. Slaa kukiri hadharani kumiliki kadi ya CCM wakati anajua dhamana kubwa aliyopewa katika chama hicho.
Alisema katiba ya chama hicho sura ya tano, ibara ya kwanza kifungu kidogo cha sita 5.1.6 kinachosema, mwanachama wa chama hicho hapaswi kuwa mwanachama wa chama kingine cha siasa baada ya kujiunga CHADEMA.
Alisema Dkt. Slaa ameanza kuwapa mashaka wanachama wa chama hicho na wengine kuamini huenda huenda yupo CHADEMA kwa kama kibaraka wa CCM anayetumiwa kwa mambo mbalimbali.
"Hivi karibuni Dkt. Slaa amekiri kumiliki kadi ya CCM na kudai kuitunza kama kumbukumbu, halii hii inaonesha bado anatumukia vyama viwili vya siasa kwa maana ya CCM na CHADEMA.
"Umefika wakati wa kiongozi huyu kuwajibishwa na chama, katika mfumo wa vyama vingi, kiongozi wa chama lazima awe mfano kwa wengine hivyo kitendo hiki kinaleta mashaka makubwa," alisema.
Alimtaka Mwenyekiti wa chama hicho Bw. Freeman Mbowe, kuchukua hatua badala ya kuliacha jambo hilo hewani na kama atashindwa kulishughulikia, viongozi wengi zaidi ndani ya chama hicho wanaweza kujitokeza na kusema wanamiliki kadi za CCM.
"Hili ni jambo la hatari sana, wanachama wataamini chama chetu kinaendeshwa na vibaraka wa CCM, haiwezekani Katibu Mkuu wa chama awe anamiliki kadi ya chama tawala.
"Wapo ambao watajitokeza kunikejeli na kudai nimetumwa lakini mfumo wa demokrasia, unatoa fursa kwa kila mtu kueleza kile anachokiona ili kujenga siasa bora nchini," alisema.
Alisema Dkt. Slaa amekosa uadilifu, sifa za kukitumikia chama hicho na kuongeza kuwa yupo tayari kuchukiwa kwa kueleza ukweli wa kile anachokiamini kama mwanachama.
Bw. Mwamalala alisema kama chama hicho kitashindwa kuchukua hatua zozote, atapeleka hoja binafsi katika Mkutano Mkuu kutaka Dkt. Slaa ajadiliwe na kuchukuliwa hatua.
"Wakati Dkt. Slaa anondoka CCM, alipaswa kuwaachia kadi yao, sisi wenye mapenzi mema na CHADEMA, hatuko tayari kuona tunaishi ndani na kadi ya chama ambacho tunataka kukiondoa madarakani katika Uchaguzi Mkuu 2015," alisema.