KadaMpinzani asema: Mnyika,Mbowe na Slaa tulieni kama maji ya kwenye mtungi !!

Jamani hivi sasa ukiingia kwenye private message compose mbona siioni? Natumaje PM? Naona reply and forward tu.

Hebu nipatie email yako basi nikutumie namba yangu tuonane jamani.

Mi ni mwanachama wa CHADEMA, najua we ni wa CCM mwenzangu, nitakuuliza vizuri masuala ya ufisadi?

Hivi kwanini kamati kuu ya CCM imejaa watuhumiwa wa ufisadi na wengine wapo kwenye orodha ya fisadi?

Hivi JK butiama ataongoza vipi kikao wakati naye yumo kwenye JK eleven? Hapatakuwa na confict of interest?

Asha

unaijua kamati kuu ya ccm ? wataje hao unaosema wapo humo.. nitumie kadampinzani@gmail.com.... utakuja kuhadithia humu !
 
Si unajua tena umalaya wa habari? Sasa ni kuwadi wa habari corruption baba.

Hata alipokuwa TZ daima si uliona mambo yake?


Ule unene wake na mashavu makubwa si haba, rizki kila kona. Si unajua wengine si rizki?

Hebu mpigie simu jamani umuulize kilichomkuta wiki hii.

Yani nilikutana na wanahabari wengine, si vicheko hivyo. Mpaka jamaa kakimbilia Bukoba kwa muda

Yani akirudi lazima nimpeleke salun

Asha

kumbe unakubali anaendeleza libeneke alilotoka nalo kwa mbowe eh ? anyway nitumie email nikupigie ukiwa na nafasi tuonane !
 
Tukitaka hii mada iwe tamu zaidi tuwalishanganishe:

Mbowe Vs Kikwete( Wenyeviti wa Vyama)
Slaa Vs Makamba(Makatibu wa Vyama)
Mnyika Vs Nchimbi( Viongozi wa Vijana wa Vyama)

Halafu ndio tujadili ugeresha wao, ukabila wao, uchafu wao- maufisadi yao na uwezo wao wa kiuongozi

Asha

Tuanze na idadi ya vitu vya udiwani/ubunge walivyoshinda kila mmoja wao baada ya kushika nafasi zao.

jee vyama vyao vimekuwa bora zaidi au vimeendelea kudumaa?
 
Tuanze na idadi ya vitu vya udiwani/ubunge walivyoshinda kila mmoja wao baada ya kushika nafasi zao.

jee vyama vyao vimekuwa bora zaidi au vimeendelea kudumaa?

Haya

Baada ya Mbowe kuwa mwenyekiti CHADEMA mwaka 2004 tu, na Slaa kuwa katibu mkuu wake. Na mnyika kujiunga nao mwaka 2005 tu. Katika uchaguzi huo viti vya ubunge vya CHADEMA viliongezeka kwa asilimia 100. Na vya udiwani kwa zaidi ya asilimia 70. Umaarufu wa CHADEMA ukakuwa kweli kweli. Lakini baada ya Kikwete kuwa Mwenyekiti na makamba katibu Mkuu huku nchimbi akiendelea kunganania Uenyekiti wa vijana harufu ya ufisadi imezidi mpaka baraza la mawaziri la chama chao limevunjika na kwa mara ya kwanza waziri mkuu amejifukuza kwa rushwa ya richmondoli. Na benki kuu ya Tanzania imepata kashfa ya karne, zile zingine zilizotokea katika vipindi cha nyuma vya Chama Cha Mafisadi(CCM) yani ni nyepesi kama soga la wakati wa kusukana na kusutana.

Sasa Chama kipi kimezidi kuwa bora na kipi kinaendelea kudumaa?

Nsakutumia namba yangu, mbona hunipigii? Na mbona nimepata failure delivery report?

Hebu niandikie wewe basi

Asha
 
Haya

Baada ya Mbowe kuwa mwenyekiti CHADEMA mwaka 2004 tu, na Slaa kuwa katibu mkuu wake. Na mnyika kujiunga nao mwaka 2005 tu. Katika uchaguzi huo viti vya ubunge vya CHADEMA viliongezeka kwa asilimia 100. Na vya udiwani kwa zaidi ya asilimia 70. Umaarufu wa CHADEMA ukakuwa kweli kweli. Lakini baada ya Kikwete kuwa Mwenyekiti na makamba katibu Mkuu huku nchimbi akiendelea kunganania Uenyekiti wa vijana harufu ya ufisadi imezidi mpaka baraza la mawaziri la chama chao limevunjika na kwa mara ya kwanza waziri mkuu amejifukuza kwa rushwa ya richmondoli. Na benki kuu ya Tanzania imepata kashfa ya karne, zile zingine zilizotokea katika vipindi cha nyuma vya Chama Cha Mafisadi(CCM) yani ni nyepesi kama soga la wakati wa kusukana na kusutana.

Sasa Chama kipi kimezidi kuwa bora na kipi kinaendelea kudumaa?

Nsakutumia namba yangu, mbona hunipigii? Na mbona nimepata failure delivery report?

Hebu niandikie wewe basi

Asha

Hela za BOT zimepotea wakati Kikwete mwenyekiti au Mkapa?
Tulinganishe hizi by elections zilizofanyika baada ya uchaguzi mkuu nani kashinda zaidi?
 
Hela za BOT zimepotea wakati Kikwete mwenyekiti au Mkapa?
Tulinganishe hizi by elections zilizofanyika baada ya uchaguzi mkuu nani kashinda zaidi?


Hela zimepotea wakati JK akiwa mgombea Urais 2005 ili zimsaidie kushinda, si unakumbuka habari za Slaa na Tundu Lissu kuhusu Deep Green na Kagoda?

CHADEMA imekuwa maradufu katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa hawa jamaa watatu na wenzao wakina Zitto, sasa tusubiri 2010 ndio tuone nani kati yao atashusha idadi ya viti vya udiwani na ubunge alivyonavyo

Asha
 
Jamani hivi sasa ukiingia kwenye private message compose mbona siioni? Natumaje PM? Naona reply and forward tu.
Hebu nipatie email yako basi nikutumie namba yangu tuonane jamani.


Asha

Da Asha, pole kwa kughafirika na PMs.. nimeona nikupatie maelezo hapa chini kama yanaweza kukusaidia:

... Ukisha click kwenye link ya 'private messages' hapo juu kushoto, kwenye hiyo hiyo window utaona link ya 'send new message'kama kwenye picha hapa chini:

capturejf3.jpg


... Ukisha bonyeza hapo, window ya kutuma PM itatokeza. Jaza detail za recipient, kama kuna zaidi ya mmoja tenganisha kwa kutumia semicolon, (unaweza hata kujitumia wewe mwenyewe kama kumbukumbu) ila utakuwa unajaza nafasi bure maana hata message zote pia zinakuwa kwenye sent folder kama una search baadae.

capturejf5.jpg


.... Ukimaliza kuandika upendacho, unaweza ku-preview na kisha kubonyeza submitt message kama hapa chini:

capturejf7.jpg

Baadae, nakutangia maongezi mema kati yako na Kada!!! :)


SteveD.
 
Da Asha, pole kwa kughafirika na PMs.. nimeona nikupatie maelezo hapa chini kama yanaweza kukusaidia:

... Ukisha click kwenye link ya 'private messages' hapo juu kushoto, kwenye hiyo hiyo window utaona link ya 'send new message'kama kwenye picha hapa chini:

capturejf3.jpg


... Ukisha bonyeza hapo, window ya kutuma PM itatokeza. Jaza detail za recipient, kama kuna zaidi ya mmoja tenganisha kwa kutumia semicolon, (unaweza hata kujitumia wewe mwenyewe kama kumbukumbu) ila utakuwa unajaza nafasi bure maana hata message zote pia zinakuwa kwenye sent folder kama una search baadae.

capturejf5.jpg


.... Ukimaliza kuandika upendacho, unaweza ku-preview na kisha kubonyeza submitt message kama hapa chini:

capturejf7.jpg

Baadae, nakutangia maongezi mema kati yako na Kada!!! :)


SteveD.

Asante SteveD kwa tuition nzito.

Limwanaume lenyewe liongo silitumii hiyo PM. Limenipa email address ya uongo.

Lav ya

Asha
 
Da Asha, pole kwa kughafirika na PMs.. nimeona nikupatie maelezo hapa chini kama yanaweza kukusaidia:

... Ukisha click kwenye link ya 'private messages' hapo juu kushoto, kwenye hiyo hiyo window utaona link ya 'send new message'kama kwenye picha hapa chini:

capturejf3.jpg


... Ukisha bonyeza hapo, window ya kutuma PM itatokeza. Jaza detail za recipient, kama kuna zaidi ya mmoja tenganisha kwa kutumia semicolon, (unaweza hata kujitumia wewe mwenyewe kama kumbukumbu) ila utakuwa unajaza nafasi bure maana hata message zote pia zinakuwa kwenye sent folder kama una search baadae.

capturejf5.jpg


.... Ukimaliza kuandika upendacho, unaweza ku-preview na kisha kubonyeza submitt message kama hapa chini:

capturejf7.jpg

Baadae, nakutangia maongezi mema kati yako na Kada!!! :)


SteveD.

heheeee, hapo nimecheka, eti area code ni chadema !
 
angalia maneno mekundu ! Hadi hivi sasa sijaelewa wewe na mwanakijiji mmetumia vigezo gani kujudge outcome ya ninachotaka kuandika wakati hata sijawasilisha ninachotaka kuandika LAKINI NASHANGAA PUU CONCLUSION ZIMEFIKA MEZANI WAKATI HATA KUKU HAJACHUNGUZWA.! mwake humu kweli ? kama maneno yako matatu ya katika hayo maneno mekundu yanavyosema, ungesubiri nifafanue ili muelewe na haikuwa "safi" kwako wewe kufikia uamuzi uliosema wakati hata hujaelewa nini nilichotaka kusema !

Usiyakimbie maneno yako bwana uzuri wa JF ushahidi unakuwa hapa hapa.

Yap, i said it !

Mnyika siasa zake kama Mrema, (yupo kwenye siasa kama geresha)
Slaa za kwake ni za kikabila kabila, !
Mbowe (huyu mchafu na uchafu wake hata sijui niuanzie wapi)

Haya wee mwanawane, kaeni mkao wa kula..More info to come


Siasa za Mnyika ni kama za Mrema, na siasa za Slaa ni za kikabila kikabila sasa unayakana maneno yako uliyoaandika mwenyewe! duh! acha hizo
 
babu hapo juu, KAMWE SIKUKATAA NA KAMWE SITOKATAA NILICHOSEMA.... isipokuwa nadhani hukunielewa ni kwamba, nilisema iweje unihukumu ili hali hata sijasema nilichotaka kusema ? hilo ndilo nililokuwa najaribu kusema. lakini sijakanusha ! subiri nitakachoandika then unihukumu !
 
babu hapo juu, KAMWE SIKUKATAA NA KAMWE SITOKATAA NILICHOSEMA.... isipokuwa nadhani hukunielewa ni kwamba, nilisema iweje unihukumu ili hali hata sijasema nilichotaka kusema ? hilo ndilo nililokuwa najaribu kusema. lakini sijakanusha ! subiri nitakachoandika then unihukumu !

Labda mie ngumbaru uliyoyaandika hapo yanajieleza wazi kabisa, ni bora uwe unaandika unachotaka kuandika badala ya kuandika mambo ambayo baadaye unayakana. Ukiwa na cha kuandika ambacho unataka kukituma hapa JF, basi bora utafute muda na kukiandika chote bila kuacha hata paragraph moja, vinginevyo haya ya 'sijasema nilichotaka kusema' yatakuwa yanajirudia kila kukicha.
 
Labda mie ngumbaru uliyoyaandika hapo yanajieleza wazi kabisa, ni bora uwe unaandika unachotaka kuandika badala ya kuandika mambo ambayo baadaye unayakana. Ukiwa na cha kuandika ambacho unataka kukituma hapa JF, basi bora utafute muda na kukiandika chote bila kuacha hata paragraph moja, vinginevyo haya ya 'sijasema nilichotaka kusema' yatakuwa yanajirudia kila kukicha.

bubu yasiwe makubwa ! YAISHE !
Walioelewa nafikiri wameelewa, mwenzangu na mie nadhani bado hujaelewa, lakini ndio hivyo ! nimekusikia ! LAKINI NI WAZI KWAMBA SIKUKANA KAMA ULIVYOSEMA !
 
12537j4.gif

mmmmmmh, i can see somebody rejoicing intemperately for executing a successful lure.
 
bubu yasiwe makubwa ! YAISHE !
Walioelewa nafikiri wameelewa, mwenzangu na mie nadhani bado hujaelewa, lakini ndio hivyo ! nimekusikia ! LAKINI NI WAZI KWAMBA SIKUKANA KAMA ULIVYOSEMA !

Hayawi makubwa ndugu yangu tunajadiliana kama Watanzania bila kutiana vidole vya macho na kuanza kurushiana matusi ya nguoni. Pamoja na kuwa tuna mitazamo ina tofautiana kidogo katika yanayoendelea Tanzania bado nathamini na kuheshimu sana mchango wako, kwa maana shilingi ina pande mbili hivyo ni lazima tuzijadili pande zote bila woga. KM, bado hujachelewa kuandika ulichotaka kuandika, ukipata nafasi kiweke hapa ukumbini ili tukione unaweza ukatufumbua macho wengi.

Pasaka njema wewe na familia yako.
 
We kada hebu soma vizuri hapo juu huoni nimesahau neno moja na nikaliongeza jamani? Kuniita mwanamke mwanaume si kitu kizuri jamani.

halafu we nshakwambia tuonane ukakataa. Hebu tuwasiliane kupitia ashabdala@yahoo.com, bado uko Dar es salaam? Nami bado niko mjini, sijaenda Znz. Tuonane tafadhali.

Asha

KadaMpinzani hebu nenda kwenye hiyo miadi otherwise unaweza kusababisha JF kuwa Darhotwire - mwenzako anataka kukunyesha udumejike wake.
 
babu hapo juu, KAMWE SIKUKATAA NA KAMWE SITOKATAA NILICHOSEMA.... isipokuwa nadhani hukunielewa ni kwamba, nilisema iweje unihukumu ili hali hata sijasema nilichotaka kusema ? hilo ndilo nililokuwa najaribu kusema. lakini sijakanusha ! subiri nitakachoandika then unihukumu !

Andika basi uombwe mara ngapi au bado Usalama wa Taifa hawakutungia la kusema?
 
Andika basi uombwe mara ngapi au bado Usalama wa Taifa hawakutungia la kusema?

yaani the difference between hizo posts zako ni dakika 4, you expected me to write within 4 minutes of your request ? hahaaaa, anyway acha zako wewe mimi simjui mtu yoyote wa usalama, nitaandika usihofu !
 
Andika basi uombwe mara ngapi au bado Usalama wa Taifa hawakutungia la kusema?
BI KIREMBWE aka BIKHOLE....! MBONA MANENO YANAANZA KUKUTOKA....! MTU AKITOA HOJA ILIYOENDA SHULE ANAKUWA ANATUNGIWA.....? KWA NINI ASITUNGIWE NA PCCB,MBOWE,ROSTAM,CHADEMA AU CCM.....!
 
Back
Top Bottom